< I Koryntian 4 >

1 Niech więc każdy uważa nas za sługi Chrystusa i szafarzy tajemnic Boga.
Mtu na atuone sisi kuwa ni watumishi wa Kristo tuliokabidhiwa siri za mungu.
2 A od szafarzy wymaga się, aby każdy [z nich] okazał się wierny.
Kinachotakiwa kwa yeyote yule aliyekabidhiwa kazi ni kuwa mwaminifu.
3 Mnie jednak najmniej zależy na tym, czy będę przez was sądzony, czy przez sąd ludzki. Nawet sam siebie nie sądzę.
Kwangu mimi si kitu nikihukumiwa na ninyi, au na mahakama ya kibinadamu; wala sijihukumu.
4 Niczego bowiem w sobie nie dostrzegam, jednak nie jestem przez to usprawiedliwiony, lecz tym, który mnie sądzi, jest Pan.
Dhamiri yangu hainishtaki kwa jambo lolote, lakini hiyo haionyeshi kwamba sina lawama. Bwana ndiye anayenihukumu.
5 Dlatego nie sądźcie przed czasem, dopóki nie przyjdzie Pan, który oświetli to, co ukryte w ciemności, i ujawni zamiary serc. Wtedy każdy otrzyma pochwałę od Boga.
Basi, msihukumu kabla ya wakati wake acheni mpaka Bwana atakapokuja. Yeye atayafichua mambo ya giza yaliyofichika, na kuonyesha wazi nia za mioyo ya watu. Ndipo kila mmoja atapata sifa anayostahili kutoka kwa Mungu.
6 To wszystko zaś, bracia, odniosłem do samego siebie i do Apollosa ze względu na was, abyście się nauczyli na naszym przykładzie nie wykraczać ponad to, co jest napisane, żeby jeden nie pysznił się drugim przeciw innemu.
Ndugu, hayo yote niliyosema juu ya Apolo na juu yangu, ni kielelezo kwenu: kutokana na mfano wangu mimi na Apolo nataka mwelewe maana ya msemo huu: “Zingatieni yaliyoandikwa.” Kati yenu pasiwe na mtu yeyote anayejivunia mtu mmoja na kumdharau mwingine.
7 Kto bowiem czyni cię różnym? Cóż masz, czego byś nie otrzymał? A jeśli otrzymałeś, to dlaczego się chlubisz, jakbyś nie otrzymał?
Nani amekupendelea wewe? Una kitu gani wewe ambacho hukupewa? Na ikiwa umepewa, ya nini kujivunia kana kwamba hukukipewa?
8 Już jesteście nasyceni, już jesteście bogaci, bez nas królujecie. I obyście królowali, abyśmy i my z wami królowali.
Haya, mmekwisha shiba! Mmekwisha kuwa matajiri! Mmekuwa wafalme bila ya sisi! Naam, laiti mngekuwa kweli watawala, ili nasi pia tuweze kutawala pamoja nanyi.
9 Bo uważam, że Bóg nas, apostołów, wyznaczył jako ostatnich, jakby na śmierć skazanych. Staliśmy się bowiem widowiskiem dla świata, aniołów i ludzi.
Nafikiri Mungu ametufanya sisi mitume tuwe watu wa mwisho kabisa, kama watu waliohukumiwa kuuawa, maana tumekuwa tamasha mbele ya ulimwengu wote, mbele ya malaika na watu.
10 My jesteśmy głupi dla Chrystusa, ale wy mądrzy w Chrystusie, my jesteśmy słabi, ale wy mocni, wy szanowani, a my wzgardzeni.
Sisi ni wapumbavu kwa ajili ya Kristo, lakini ninyi ni wenye busara katika kuungana na Kristo! Sisi ni dhaifu, ninyi ni wenye nguvu. Ninyi mnaheshimika, sisi tunadharauliwa.
11 Aż do tej chwili cierpimy głód i pragnienie, jesteśmy nadzy, policzkowani i tułamy się;
Mpaka dakika hii, sisi tuna njaa na kiu, hatuna nguo, twapigwa makofi, hatuna malazi.
12 I trudzimy się, pracując własnymi rękami. Gdy nas znieważają – błogosławimy, gdy nas prześladują – znosimy;
Tena twataabika na kufanya kazi kwa mikono yetu wenyewe. Tukitukanwa, tunawatakia baraka; tukidhulumiwa, tunavumilia;
13 Gdy nam złorzeczą – modlimy się [za nich]. Staliśmy się jak śmiecie tego świata, [jak] odpadki u wszystkich, aż do tej chwili.
tukisingiziwa, tunajibu kwa adabu. Mpaka sasa tumetendewa kama uchafu wa dunia; na kwa kila mtu sisi ni takataka!
14 Nie piszę tego po to, aby was zawstydzić, ale napominam [was] jako moje umiłowane dzieci.
Siandiki mambo haya kwa ajili ya kuwaaibisha ninyi, bali kwa ajili ya kuwafundisheni watoto wangu wapenzi.
15 Choćbyście bowiem mieli dziesięć tysięcy wychowawców w Chrystusie, to jednak nie [macie] wielu ojców. Ja bowiem przez ewangelię zrodziłem was w Chrystusie Jezusie.
Maana hata kama mnao maelfu ya walezi katika maisha yenu ya Kikristo, baba yenu ni mmoja tu, kwani katika maisha ya Kikristo mimi ndiye niliyewazaeni kwa kuihubiri Habari Njema.
16 Proszę was więc, bądźcie moimi naśladowcami.
Kwa hiyo, nawasihi: fuateni mfano wangu.
17 Dlatego to posłałem do was Tymoteusza, który jest moim umiłowanym synem i wiernym w Panu. On wam przypomni moje drogi w Chrystusie, jak nauczam wszędzie, w każdym kościele.
Ndiyo maana nimemtuma Timetheo kwenu. Yeye ni mtoto wangu mpenzi na mwaminifu katika Bwana. Atawakumbusheni njia ninayofuata katika kuishi maisha ya Kikristo; njia ninayofundisha kila mahali katika makanisa yote.
18 A niektórzy wbili się w pychę, jakbym nie miał przyjść do was.
Baadhi yenu wameanza kuwa na majivuno wakidhani kwamba sitakuja tena kwenu.
19 Lecz przyjdę do was wkrótce, jeśli Pan zechce, i poznam nie słowa pysznych, ale [ich] moc.
Lakini, Bwana akipenda, nitakuja kwenu upesi; na hapo ndipo nitakapojionea mwenyewe, sio tu kile wanachoweza kusema hao wenye majivuno, bali pia kila wanachoweza kufanya.
20 Królestwo Boże bowiem [przejawia się] nie w słowie, ale w mocy.
Maana Utawala wa Mungu si shauri la maneno matupu, bali ni nguvu.
21 Co chcecie? Czy mam przyjść do was z rózgą, czy z miłością i w duchu łagodności?
Mnapendelea lipi? Nije kwenu na fimbo, ama nije na moyo wa upendo na upole?

< I Koryntian 4 >