< I Koryntian 3 >

1 I ja, bracia, nie mogłem do was mówić jak do [ludzi] duchowych, ale jak do cielesnych, jak do niemowląt w Chrystusie.
Ndugu, mimi sikuweza kusema nanyi kama watu mlio na huyo Roho. Nilipaswa kusema nanyi kama watu wa kidunia, kama watoto wachanga katika maisha ya Kikristo.
2 Karmiłem was mlekiem, a nie [stałym] pokarmem, bo jeszcze nie mogliście go [przyjąć], a nawet teraz jeszcze nie możecie;
Ilinibidi kuwalisheni kwa maziwa, na si kwa chakula kigumu, kwani hamkuwa tayari kukipokea. Hata sasa hamko tayari.
3 Gdyż jeszcze jesteście cieleśni. Skoro bowiem [jest] między wami zazdrość, kłótnie i podziały, to czyż nie jesteście cieleśni i nie postępujecie na sposób ludzki?
Maana bado mu watu wa kidunia. Je, si kweli kwamba bado uko wivu na magombano kati yenu? Mambo hayo yanaonyesha wazi kwamba ninyi bado ni watu wa kidunia, mnaishi mtindo wa kidunia.
4 Skoro ktoś mówi: Ja jestem Pawła, a inny: Ja Apollosa, to czyż nie jesteście cieleśni?
Mmoja wenu anaposema, “Mimi ni wa Paulo”, na mwingine, “Mimi ni wa Apolo”, je, hiyo haionyeshi kwamba mnaishi bado kama watu wa dunia hii tu?
5 Kim bowiem jest Paweł? Kim Apollos? Tylko sługami, przez których uwierzyliście, a to tak, jak każdemu dał Pan.
Apolo ni nani? na Paulo ni nani? Sisi ni watumishi tu ambao tuliwaleteeni ninyi imani. Kila mmoja wetu anafanya kazi aliyopewa na Bwana.
6 Ja siałem, Apollos podlewał, ale Bóg dał wzrost.
Mimi nilipanda mbegu, Apolo akamwagilia maji; lakini aliyeiotesha mbegu ni Mungu.
7 Tak więc ani ten, który sieje, ani ten, który podlewa, nic nie znaczą, tylko Bóg, który daje wzrost.
Wa maana si yule aliyepanda mbegu, au yule aliyemwagilia maji; wa maana ni Mungu aliyeiwezesha mbegu kuota.
8 Ten zaś, który sieje, i ten, który podlewa, stanowią jedno, a każdy otrzyma swoją zapłatę stosownie do swojej pracy.
Yule aliyepanda na yule aliyemwagilia maji wote ni sawa, ingawa kila mmoja atapokea tuzo lake kufuatana na jitihada yake mwenyewe.
9 Jesteśmy bowiem współpracownikami Bożymi; wy jesteście Bożą rolą i Bożą budowlą.
Maana sisi ni ndugu, wafanyakazi pamoja na Mungu; na ninyi ni shamba lake; ninyi ni jengo lake.
10 Według łaski Boga, która została mi dana, jak mądry budowniczy położyłem fundament, a inny na nim buduje. Jednak każdy niech uważa, jak na nim buduje.
Kwa msaada wa neema aliyonipa Mungu, nimefaulu, kama mwashi stadi mwenye busara, kuweka msingi ambao juu yake mtu mwingine anajenga. Basi, kila mmoja awe mwangalifu jinsi anavyojenga juu yake.
11 Nikt bowiem nie może położyć innego fundamentu niż ten, który jest położony, którym jest Jezus Chrystus.
Hakuna mtu awezaye kuweka msingi mwingine badala ya ule uliokwisha wekwa, yaani Yesu Kristo.
12 A czy ktoś na tym fundamencie buduje [ze] złota, srebra, z drogich kamieni, drewna, siana [czy ze] słomy;
Juu ya msingi huo mtu anaweza kujenga kwa dhahabu, fedha au mawe ya thamani; anaweza kutumia miti, majani au nyasi.
13 Dzieło każdego będzie jawne. Dzień [ten] bowiem to pokaże, gdyż przez ogień zostanie objawione i ogień wypróbuje, jakie jest dzieło każdego.
Iwe iwavyo, ubora wa kazi ya kila mmoja utaonekana wakati Siku ile ya Kristo itakapoifichua. Maana, Siku hiyo itatokea na moto, na huo moto utaipima na kuonyesha ubora wake.
14 Jeśli czyjeś dzieło budowane na tym [fundamencie] przetrwa, ten otrzyma zapłatę.
Ikiwa alichojenga mtu juu ya huo msingi kitaustahimili huo moto, atapokea tuzo;
15 Jeśli [zaś] czyjeś dzieło spłonie, [ten] poniesie szkodę. Lecz on sam będzie zbawiony, tak jednak, jak przez ogień.
lakini kama alichojenga kitaunguzwa, basi, atapoteza tuzo lake; lakini yeye mwenyewe ataokolewa kana kwamba ameponyoka kutoka motoni.
16 Czyż nie wiecie, że jesteście świątynią Boga i że Duch Boży w was mieszka?
Je, hamjui kwamba ninyi ni hekalu la Mungu, na kwamba Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?
17 A jeśli ktoś niszczy świątynię Boga, tego zniszczy Bóg, bo świątynia Boga jest święta, a wy nią jesteście.
Basi, mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu; maana hekalu la Mungu ni takatifu, na hekalu hilo ni ninyi wenyewe.
18 Niech nikt nie oszukuje samego siebie. Jeśli komuś spośród was wydaje się, że jest mądry na tym świecie, niech się stanie głupim, aby stał się mądrym. (aiōn g165)
Msijidanganye! Mtu yeyote miongoni mwenu akijidhania mwenye hekima mtindo wa kidunia, heri awe mjinga kusudi apate kuwa na hekima ya kweli. (aiōn g165)
19 Mądrość bowiem tego świata jest głupstwem u Boga. Bo jest napisane: On chwyta mądrych w ich przebiegłości.
Maana, hekima ya kidunia ni upumbavu mbele ya Mungu. Kwani Maandiko Matakatifu yasema: “Mungu huwanasa wenye hekima katika ujanja wao.”
20 I znowu: Pan zna myśli mądrych [i wie], że są marnością.
Na tena: “Bwana ajua kwamba mawazo ya wenye hekima hayafai.”
21 Niech się więc nikt nie chlubi ludźmi. Wszystko bowiem jest wasze:
Basi, mtu asijivunie watu. Maana kila kitu ni chenu.
22 Czy Paweł, czy Apollos, czy Kefas, czy świat, czy życie, czy śmierć, czy [to, co] teraźniejsze, czy [to, co] przyszłe – wszystko [jest] wasze;
Paulo, Apolo na Kefa, ulimwengu, maisha na kifo; mambo ya sasa na ya baadaye, yote ni yenu.
23 Wy zaś jesteście Chrystusa, a Chrystus Boga.
Lakini ninyi ni wa Kristo naye Kristo ni wa Mungu.

< I Koryntian 3 >