< Jozuego 9 >
1 A gdy usłyszeli wszyscy królowie, którzy byli za Jordanem na górach, i na równinach, i nad wszystkiem brzegiem morza wielkiego przeciw Libanowi, Hetejczyk, i Amorejczyk, i Chananejczyk, Ferezejczyk, Hewejczyk, i Jebuzejczyk;
Basi ikawa wafalme wote waliokuwa magharibi mwa Yordani waliposikia juu ya haya yote, wale waliokuwa katika nchi ya vilima, upande wa magharibi mwa vilima na katika pwani yote ya hiyo Bahari Kuu, hadi kufikia Lebanoni (wafalme wa Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi),
2 Zebrali się pospołu, aby walczyli przeciw Jozuemu, i przeciw Izraelowi, jednomyślnie.
wakajiunga pamoja ili kupigana vita dhidi ya Yoshua na Israeli.
3 Ale obywatele Gabaon, usłyszawszy, co uczynił Jozue Jerychowi i Hajowi,
Hata hivyo, watu wa Gibeoni waliposikia juu ya hayo yote Yoshua aliyowatendea watu wa Yeriko na Ai,
4 Postąpili sobie i oni chytrze, a poszedłszy zmyślili się być posłami, i wzięli wory stare na osły swe, i łagwie winne stare, i potarte, i łatane;
nao wakaamua kufanya hila: Wakajifanya kama wajumbe wakiwa na punda waliobebeshwa mizigo wakiwa na magunia yaliyochakaa na viriba vya mvinyo vikuukuu vyenye nyufa zilizozibwa.
5 I obuwie stare i łatane na nogi swoje, i szaty stare na się, a wszystek chleb, co go z sobą nabrali w drogę, suchy był i spleśniały.
Walivaa miguuni mwao viatu vilivyoraruka na kushonwa kisha wakavaa nguo kuukuu. Chakula chao kilikuwa mkate uliokauka na kuingia koga.
6 Tedy przyszli do Jozuego, do obozu w Galgal, i rzekli do niego, i do mężów Izraelskich: Z ziemiśmy dalekiej przyszli; przetoż teraz uczyńcie z nami przymierze.
Ndipo wakamwendea Yoshua kambini huko Gilgali wakamwambia yeye pamoja na watu wa Israeli, “Tumetoka katika nchi ya mbali, fanyeni mkataba nasi.”
7 Ale odpowiedzieli mężowie Izraelscy Hewejczykowi: Podobno ty mieszkasz między nami, a jakoż z tobą możemy uczynić przymierze?
Basi watu wa Israeli wakawaambia hao Wahivi, “Lakini huenda mnakaa karibu nasi, twawezaje basi kufanya mapatano nanyi?”
8 A oni rzekli do Jozuego: Słudzy twoi jesteśmy. I rzekł do nich Jozue: Coście wy zacz, a skądeście przyszli?
Wakamwambia Yoshua, “Sisi ni watumishi wako.” Yoshua akawauliza, “Ninyi ni nani, nanyi mnatoka wapi?”
9 I odpowiedzieli mu: Z ziemi dalekiej bardzo przyszli słudzy twoi w imieniu Pana, Boga twego; bośmy słyszeli sławę jego, i wszystko, co uczynił w Egipcie;
Nao wakamjibu: “Watumishi wako wametoka nchi ya mbali sana kwa ajili ya umaarufu wa Bwana Mungu wenu. Kwa kuwa tumesikia taarifa zake: hayo yote aliyofanya huko Misri,
10 I wszystko, co uczynił dwom królom Amorejskim, którzy byli za Jordanem, Sehonowi królowi Hesebon, i Ogowi królowi Basan, którzy mieszkali w Astarot.
pia yale yote aliyowatendea wafalme wawili wa Waamori mashariki ya Yordani; huyo Sihoni mfalme wa Heshboni na Ogu mfalme wa Bashani, aliyetawala huko Ashtarothi.
11 I rozkazali nam starsi nasi, i wszyscy obywatele ziemi naszej, mówiąc: Nabierzcie sobie żywności na drogę, a idźcie przeciwko nim, i mówcie im: Słudzy wasi jesteśmy, przetoż teraz uczyńcie z nami przymierze.
Basi wazee wetu na wale wote wanaoishi katika nchi yetu walituambia, ‘Chukueni chakula cha safari; nendeni mkakutane na watu hao na kuwaambia, “Sisi tu watumishi wenu, fanyeni mapatano nasi.”’
12 Ten chleb nasz ciepłyśmy na drogę wzięli z domów naszych tego dnia, gdyśmy wyszli, abyśmy szli do was; a teraz oto wysechł, i popleśniał.
Mkate huu wetu ulikuwa wa moto tulipoufunga siku tulipoanza safari kuja kwenu, lakini sasa angalia jinsi ulivyokauka na kuota ukungu.
13 I te łagwie winne, któreśmy byli napełnili, były nowe, a oto się popękały; także te szaty nasze, i obuwie nasze zwiotszały dla bardzo dalekiej drogi.
Viriba hivi vya mvinyo vilikuwa vipya tulipovijaza, lakini ona jinsi vilivyo na nyufa. Nguo zetu na viatu vimechakaa kwa ajili ya safari ndefu.”
14 A tak wzięli oni mężowie Izraelscy z onej żywności ich, a ust się Pańskich nie pytali.
Basi watu wa Israeli wakavikagua vyakula vyao bila kupata shauri kutoka kwa Bwana.
15 Tedy z nimi uczynił Jozue pokój, i postanowił z nimi przymierze, aby ich zachował przy żywocie; także przysięgły im książęta zgromadzenia.
Ndipo Yoshua akafanya mapatano ya amani pamoja nao kuwaacha waishi, nao viongozi wa kusanyiko wakathibitisha kwa kiapo.
16 Ale po trzech dniach po uczynieniu z nimi przymierza, usłyszeli, że blisko ich byli, a iż w pośrodku ich mieszkali.
Siku ya tatu baada ya hao kufanya mapatano na Wagibeoni, Waisraeli wakapata habari kuwa hao watu ni jirani zao waliokuwa wanaishi karibu nao.
17 A ruszywszy się synowie Izraelscy przyciągnęli do miast ich dnia trzeciego, a miasta ich te były: Gabaon, i Kafira, i Beerot, i Karyjatyjarym.
Ndipo wana wa Israeli wakasafiri na siku ya tatu wakafika kwenye miji yao ya Gibeoni, Kefira, Beerothi na Kiriath-Yearimu.
18 I nie wytracili ich synowie Izraelscy; albowiem przysięgły im były książęta zgromadzenia przez Pana, Boga Izraelskiego, skąd szemrało wszystko zgromadzenie przeciw książętom.
Lakini Waisraeli hawakuwashambulia kwa kuwa viongozi wa kusanyiko walikuwa wamewaapia kwa Bwana, Mungu wa Israeli. Kusanyiko lote likanungʼunika dhidi ya hao viongozi,
19 I rzekły wszystkie książęta do całego zgromadzenia: Myśmy im przysięgli przez Pana, Boga Izraelskiego; przetoż teraz nie możemy się ich tknąć.
lakini viongozi wote wakawajibu, “Tumeshawaapia kwa Bwana, Mungu wa Israeli, kwa hiyo hatuwezi kuwagusa sasa.
20 To im uczynimy, a zachowamy je żywo, iżby nie przyszło na nas rozgniewanie dla przysięgi, którąśmy im przysięgli.
Hivi ndivyo tutakavyowafanyia: Tutawaacha waishi, ili ghadhabu isije juu yetu kwa kuvunja kiapo tulichowaapia.”
21 Nadto rzekły do nich książęta: Niech żyją, a niech rąbią drwa, i niech noszą wodę wszystkiemu zgromadzeniu; i przestali na tem, jako im powiedziały książęta.
Wakaendelea kusema, “Waacheni waishi, lakini wawe wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya jamii yote.” Hivyo ahadi waliyoweka viongozi kwao ikawa hivyo.
22 Potem wezwał ich Jozue, i rzekł do nich, mówiąc: Przeczżeście nas oszukali, powiadając: Dalekimiśmy od was bardzo, a wy w pośrodku nas mieszkacie?
Kisha Yoshua akawaita Wagibeoni na kuwaambia, “Kwa nini mmetudanganya kwa kutuambia, ‘Tunaishi mbali nanyi,’ wakati ambapo ninyi mnaishi karibu nasi?
23 A tak teraz przeklęci jesteście, i nie ustaną z was słudzy, i rąbiący drwa, i noszący wodę do domu Boga mego.
Sasa mko chini ya laana: Daima mtakuwa wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu.”
24 Którzy odpowiedzieli Jozuemu, i rzekli: Zapewne oznajmiono było sługom twoim, jako był rozkazał Pan, Bóg twój, Mojżeszowi słudze swemu, aby wam dał wszystkę ziemię, a iżby wygładził wszystkie mieszkające w tej ziemi przed twarzą waszą; przetoż baliśmy się bardzo o żywot nasz przed wami, i uczyniliśmy tę rzecz.
Wakamjibu Yoshua, “Watumwa wako waliambiwa waziwazi jinsi Bwana Mungu wenu alivyomwamuru mtumishi wake Mose kuwapa ninyi nchi hii yote na kuwaangamiza wakazi wake wote toka mbele zenu. Kwa hiyo tuliogopa mno kwa ajili ya uhai wetu kwa sababu yenu, ndiyo maana tukafanya neno hili.
25 A teraz otośmy w rękach twoich; coć się dobrego i słusznego widzi uczynić z nami, uczyń.
Sasa tupo mikononi mwako. Tufanyieni lolote mnaloona kuwa jema na haki kwako.”
26 I uczynił im tak, a wybawił je z rąk synów Izraelskich, że ich nie pobili.
Kwa hiyo Yoshua akawaokoa mikononi mwa Waisraeli, nao hawakuuawa.
27 I postanowił je Jozue dnia onego, aby rąbali drwa, i nosili wodę zgromadzeniu, i do ołtarza Pańskiego aż do tego dnia, na miejscu, które by obrał.
Siku hiyo Yoshua akawafanya Wagibeoni wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya jamii na kwa ajili ya madhabahu ya Bwana mahali pale ambapo Bwana angepachagua. Hivyo ndivyo walivyo hadi hivi leo.