< Matei 13 >

1 Ligono lilolo, Yesu awukili munyumba yila akahamba kutama mumhana ya nyanja.
Siku iyo hiyo Yesu akatoka nje ya nyumba, akaketi kando ya bahari.
2 Msambi uvaha wa vandu wamtindili hati Yesu akakwela muwatu, akatama. Vandu voha vayimili mumhana ya nyanja,
Umati mkubwa mno wa watu ukakusanyika kumzunguka, hata ikabidi aingie katika chombo na kuketi humo, nao watu wote wakawa wamesimama ukingoni mwa bahari.
3 namwene Yesu akavajovela mambu ga mahele kwa miluhumu. “Myuwanila, mundu mmija mbeyu ahambili kumija mbeyu.
Ndipo akawaambia mambo mengi kwa mifano, akisema: “Mpanzi alitoka kwenda kupanda mbegu zake.
4 Peamijili, mbeyu zingi zikagwilila munjila, na hidege yikabwela yikahola.
Alipokuwa akitawanya mbegu, nyingine zilianguka kando ya njia, nao ndege wakaja na kuzila.
5 Zingi zakagwilila pamatalau pangali kuvya na ludaka neju. Zalolikini zimeli kanyata ndava ludaka lwavi lwamahele lepi.
Nyingine zilianguka kwenye ardhi yenye mwamba isiyo na udongo wa kutosha. Zikaota haraka, kwa kuwa udongo ulikuwa haba.
6 Lilanga palaumili, lachonili ndava mikiga yaki yakamwili lepi muludaka, zikanyala.
Lakini jua lilipozidi, mimea ikanyauka na kukauka kwa kuwa mizizi yake haikuwa na kina.
7 Mbeyu zingi zagwilili mumikongo ya minga, ndi mikongo ya minga yikamela na kuzihinya.
Mbegu nyingine zilianguka kwenye miiba, nayo miiba hiyo ikakua, ikaisonga hiyo mimea.
8 Zingi zagwili paludaka lwa bwina, zameli na kupambika, yingi mbeyu miya yimoja na yingi mbeyu sitini na yingi mbeyu selasini.”
Mbegu nyingine zilianguka kwenye udongo mzuri ambapo zilitoa mazao, nyingine mara mia moja, nyingine mara sitini, na nyingine mara thelathini.
9 Yesu akajova, myuwana nyenye mwemuvi na makutu.
Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”
10 Vawuliwa va Yesu vamhambili, vakamkota, “Ndava kyani wijova na vandu kwa miluhumu?”
Wanafunzi wake wakamwendea, wakamuuliza, “Kwa nini unasema na watu kwa mifano?”
11 Yesu akavayangula, “Nyenye mpewili uhotola wa kumanya umfiyu wa Unkosi wa kunani kwa Chapanga, nambu vene vapewili lepi.
Akawajibu, “Ninyi mmepewa kuzifahamu siri za Ufalme wa Mbinguni, lakini wao hawajapewa.
12 Muni mundu mweavi na chindu yati iyonjokesewa neju, nambu mundu angali kuvya na chindu hati cheavi nachu yati chinyagiwa.
Kwa maana yule aliye na kitu atapewa zaidi, naye atakuwa navyo tele. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyangʼanywa.
13 Muni nijova nawu kwa miluhumu, ndava vilolokesa nambu vilola lepi viyuwana nambu vimanya lepi.
Hii ndiyo sababu nasema nao kwa mifano: “Ingawa wanatazama, hawaoni; wanasikiliza, lakini hawasikii, wala hawaelewi.
14 Kwa vene gatimili malovi gala geajovili Isaya mweavi mlota wa Chapanga, kuyuwana yati mwiyuwana, nambu yati mwimanya lepi, kulola yati mwilola, nambu yati mwiwona lepi,
Kwao unatimia ule unabii wa Isaya aliposema: “‘Hakika mtasikiliza lakini hamtaelewa; na pia mtatazama lakini hamtaona.
15 muni mitima ya vandu ava yitopa. Vagadindii makutu gavi, vagubiki mihu gavi. Kuvya lepi, yavaloli na mihu gavi, yavayuwini na makutu gavi, yavamanyalili muluhala lwavi, na kumuwuyila Bambu, na nene nganivalamisi.
Kwa kuwa mioyo ya watu hawa imekuwa migumu; hawasikii kwa masikio yao, na wamefumba macho yao. Wasije wakaona kwa macho yao, na wakasikiliza kwa masikio yao, wakaelewa kwa mioyo yao, na kugeuka nami nikawaponya.’
16 Nambu mmotisiwa nyenye, muni mihu ginu gilola na makutu ginu giyuwana.
Lakini heri macho yenu kwa sababu yanaona, na heri masikio yenu kwa sababu yanasikia.
17 Nikuvajovela chakaka, vamlota va Chapanga vamahele na vandu va Chapanga vamahele vanogili kugalola gala gemgaloli nambu vagaloli lepi, na kuyuwana gala gemyuwini nambu nakuyuwana.”
Amin, nawaambia, manabii wengi na wenye haki walitamani kuona yale mnayoyaona lakini hawakuyaona, na walitamani kusikia yale mnayoyasikia lakini hawakuyasikia.
18 “Hinu, nyenye myuwana ndava ya luhumu lwenulu lwa mmija mbeyu.
“Sikilizeni basi maana ya ule mfano wa mpanzi:
19 Yeyoha mweiyuwana lilovi la Unkosi wa Chapanga changamanya, iwanangana ngati mbeyu zezagwili munjila, ndi yula mhakau ibwela na kutola chechimijiwi mumtima waki.
Mtu yeyote anaposikia neno la Ufalme naye asilielewe, yule mwovu huja na kunyakua kile kilichopandwa moyoni mwake. Hii ndiyo ile mbegu iliyopandwa kando ya njia.
20 Mbeyu zezagwili mulitalau ndi luhumu wa mundu yula mweiyuwana lilovi lenilo na bahapo akulipokela kwa luheku.
Ile mbegu iliyopandwa kwenye sehemu yenye mawe ni mtu yule ambaye hulisikia neno na mara hulipokea kwa furaha.
21 Nambu nakuyingila mugati yaki ndava avi lepi na mikiga, lilovi lenilo litama mulukumbi luhupi na pegihumila man'gaiso na kuhengiwa uhakau ndava ya lilovi la Chapanga, kanyata igwa.
Lakini kwa kuwa hana mizizi yenye kina ndani yake, lile neno hudumu kwa muda mfupi tu. Kisha dhiki au mateso yanapoinuka kwa ajili ya lile neno, yeye mara huchukizwa.
22 Mewawa na mbeyu yeyagwili pagati ya mikongo ya minga, ndi luhumu lwa mundu mweiyuwana lilovi lenilo, nambu mambu ga pamulima apa na mnogo wa kugana vindu vyamahele vikulitindila lilovi lenilo na ipambika lepi matunda ndi kuhenga gala gakumganisa Chapanga. (aiōn g165)
Ile mbegu iliyopandwa katika miiba ni yule mtu alisikiaye neno, lakini masumbufu ya maisha haya na udanganyifu wa mali hulisonga lile neno na kulifanya lisizae matunda. (aiōn g165)
23 Nambu mbeyu yeyagwilili muludaka lwabwina ndi luhumu wa mundu mweiyuwana lilovi na kulimanya, ndi yipambika matunda, yimonga matunda miya na yingi matunda sitini na yingi matunda selasini.”
Lakini ile mbegu iliyopandwa kwenye udongo mzuri ni yule mtu ambaye hulisikia neno na kulielewa. Naye hakika huzaa matunda, akizaa mara mia, au mara sitini, au mara thelathini ya mbegu iliyopandwa.”
24 Yesu avajovili vandu luhumu lungi, “Unkosi wa kunani kwa Chapanga uwanangini na mundu mweamijili mbeyu yabwina mumgunda waki.
Yesu akawaambia mfano mwingine, akasema: “Ufalme wa Mbinguni unaweza kufananishwa na mtu aliyepanda mbegu nzuri katika shamba lake.
25 Hinu vandu pavagonili abwelili mundu likoko na kumija masindi pagati ya nganu na kuwuka.
Lakini wakati kila mtu alipokuwa amelala, adui yake akaja na kupanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.
26 Penapo nganu peyameli na kutumbula kuholomola njechela, mewawa masindi gakahumila.
Ngano ilipoota na kutoa masuke, magugu nayo yakatokea.
27 Vatumisi va mkolo mgunda vamhambili na kumjovela mwene, ‘Bambu, chakaka wamijili mbeyu zabwina kumgunda waku. Hinu masindi gahumili koki?’
“Watumishi wa yule mwenye shamba wakamjia na kumwambia, ‘Bwana, si tulipanda mbegu nzuri shambani mwako? Basi, magugu yametoka wapi?’
28 Mwene akavayangula, ‘Mundu likoko ndi mweahengili genago.’ Ndi vatumisi vaki vakamkota wigana tete tikatupulai masindi?
“Akawajibu, ‘Adui ndiye alifanya jambo hili.’ “Wale watumishi wakamuuliza, ‘Je, unataka twende tukayangʼoe?’
29 Mwene akavayangula, ‘Lepi,’ Pangi pemwitupula masindi, yati mwitupula na nganu mewa.
“Lakini akasema, ‘Hapana, msiyangʼoe, kwa maana wakati mkingʼoa magugu mnaweza mkangʼoa na ngano pamoja nayo.
30 Mlekayi vikula pamonga mbaka lukumbi lwa kubena. Lukumbi lwenulo ndi yati nikuvajovela vabenaji, vayola hoti masindi na kugakunga malundu ga kuyocha motu, na nganu mbenai na kuyivika pachibana changu.”
Acheni ngano na magugu vikue vyote pamoja mpaka wakati wa mavuno. Wakati huo nitawaambia wavunaji wayakusanye magugu kwanza, wayafunge matita matita ili yachomwe moto; kisha wakusanye ngano na kuileta ghalani mwangu.’”
31 Yesu avajovili vandu luhumu lungi, “Unkosi wa kunani kwa Chapanga uwanangini na mbeyu yidebe yeyikemiwa haladali mundu ayitolili, na kumija kumgunda waki.
Akawaambia mfano mwingine, akasema, “Ufalme wa Mbinguni ni kama punje ya haradali, ambayo mtu aliichukua, akaipanda shambani mwake.
32 Yene yivya yidebe kuliku mbeyu zoha, nambu yikamela na yikula kuvya mkongo uvaha kuliku mimea yoha, hati hidege yibwela na kujenga hisakanilu, mumambanda gaki.”
Ingawa mbegu hiyo ni ndogo kuliko mbegu zote, lakini inapokua ni mmea mkubwa kuliko yote ya bustanini, nao huwa mti mkubwa, hadi ndege wa angani wanakuja na kutengeneza viota katika matawi yake.”
33 Yesu avajovili luhumu lungi, “Unkosi wa kunani kwa Chapanga uwanangini na mau mmonga mweagegili ngemeku, akahangisana na uhembe madebe gavili na lapinga, na uhembe woha watutumwiki.”
Akawaambia mfano mwingine, “Ufalme wa Mbinguni unafanana na chachu ambayo mwanamke aliichukua akaichanganya katika kiasi kikubwa cha unga mpaka wote ukaumuka.”
34 Yesu aujovili msambi wa vandu genago goha kwa miluhumu, kawaka chindu cheajovili changali miluhumu,
Yesu alinena mambo haya yote kwa makutano kwa mifano. Wala hakuwaambia lolote pasipo mfano.
35 Muni lijambu leajovili mlota wa Chapanga litimilayi, “Yati nijova nawu kwa luhumu, yati nikuvajovela mambu gegafiyiki kutumbula kuwumbwa kwa mulima.”
Hii ilikuwa ili kutimiza lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii aliposema: “Nitafungua kinywa changu niseme nao kwa mifano; nitahubiri mambo yaliyofichika tangu kuumbwa kwa misingi ya ulimwengu.”
36 Kangi Yesu avalagili vandu vala, akayingila munyumba. Vawuliwa vaki vamhambalili vakamjovela, “Utidandaulila luhumu lwa masindi kumgunda.”
Kisha Yesu akaagana na makutano, akaingia nyumbani. Wanafunzi wake wakamjia wakamwambia, “Tueleze maana ya ule mfano wa magugu shambani.”
37 Yesu akavayangula, “Mmija mbeyu zabwina ndi Mwana wa Mundu
Akawaambia, “Aliyepanda mbegu nzuri ni Mwana wa Adamu.
38 Mgunda wula ndi pamulima. Mbeyu zabwina zila ndi vandu vala unkosi ndi wavi. Nambu masindi gala ndi vandu va yula Mhakau.
Shamba ni ulimwengu na mbegu nzuri ni wana wa Ufalme. Magugu ni wana wa yule mwovu.
39 Mundu likoko yula mweamijili masindi ndi Setani. Mabenu ndi mwishu wa mulima uwu, vabenaji ndi Vamitumu va kunani kwa Chapanga. (aiōn g165)
Yule adui aliyepanda magugu ni ibilisi. Mavuno ni mwisho wa dunia, nao wavunaji ni malaika. (aiōn g165)
40 Ngati chavitupula masindi na kugayocha motu, ndi yati cheyivya pamwishu wa mulima uwu. (aiōn g165)
“Kama vile magugu yangʼolewavyo na kuchomwa motoni, ndivyo itakavyokuwa wakati wa mwisho wa dunia. (aiōn g165)
41 Mwana wa Mundu yati akuvatuma Vamitumu vaki va Chapanga vavayola kuhuma ku Unkosi waki voha vevibudisa vandu kwa Chapanga na vevavi na matendu gahakau,
Mwana wa Adamu atawatuma malaika zake, nao watakusanya kutoka Ufalme wake kila kitu kinachosababisha dhambi na watenda maovu wote.
42 na kuvataga mulitanulu la motu ukali kwenuko yati vivemba na kuyaga minu.
Nao watawatupa katika tanuru la moto ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.
43 Kangi, vandu vevihenga matendu gabwina palongolo ya Chapanga yati ving'asima ngati lilanga muunkosi wa Dadi wavi. Hinu mweavi na makutu ndi ayuwana!”
Ndipo wenye haki watangʼaa kama jua katika Ufalme wa Baba yao. Yeye aliye na masikio, na asikie.
44 “Unkosi wa kunani kwa Chapanga uwanangana ngati vindu vya mashonga gamahele vyevifiyiki kumgunda. Mundu mmonga ayiwene, akafiya kavili. Ahekili neju, hati akahamba kugulisa vyoha vyeavi navyu na akagula mgunda wula.”
“Ufalme wa Mbinguni unafanana na hazina iliyofichwa shambani, ambayo mtu mmoja alipoiona akaificha tena. Kisha katika furaha yake, akaenda akauza vyote alivyokuwa navyo, akalinunua lile shamba.”
45 “Kavili Unkosi wa kunani kwa Chapanga uwanangana na mgulisa vindu mweilonda chindu cha mashonga gamahele neju chechikemelewa lulu.
“Tena, Ufalme wa Mbinguni unafanana na mfanyabiashara aliyekuwa akitafuta lulu safi.
46 Peapatili lulu yimonga yeyiguliswa kwa mashonga gamahele neju, akahamba, kugulisa vyoha vyeavi navyu na kugula chindu chila.”
Alipoipata lulu moja ya thamani kubwa, alikwenda akauza vyote alivyokuwa navyo akainunua.”
47 “Mewawa Unkosi wa kunani kwa Chapanga uwanangana na ngwanda wa somba weujwigiwi munyanja, kulova somba ndalindali.
“Tena, Ufalme wa Mbinguni ni kama wavu wa kuvua samaki uliotupwa baharini ukavua samaki wa kila aina.
48 Paumemili, valova somba vahutili pandumba, vakatama na kuhagula somba zabwina na kuvika mumadengu gavi, na somba zezawolili vakataga.
Ulipojaa, wavuvi wakavuta pwani, wakaketi na kukusanya samaki wazuri kuwaweka kwenye vyombo safi, lakini wale samaki wabaya wakawatupa.
49 Chenichi ndi cheyivya pamwishu wa mulima uwu, Vamitumu va kunani kwa Chapanga yati vihumila na kupangula vandu vabwina na vandu vahakau, (aiōn g165)
Hivi ndivyo itakavyokuwa wakati wa mwisho wa dunia. Malaika watakuja na kuwatenganisha watu waovu na watu wenye haki. (aiōn g165)
50 kangi yati vakuvataga vandu vahakau mulitanulu la motu, kwenuko ndi yati vivemba na kuyaga minu.”
Nao watawatupa hao waovu katika tanuru la moto ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.”
51 Yesu akavakota, “Wu, mukugamanya mambu goha aga?” Vakamyangula, “Ena.”
Yesu akauliza, “Je, mmeyaelewa haya yote?” Wakamjibu, “Ndiyo.”
52 Mwene akavajovela, “Hinu ndi kila muwula wa malagizu mweajiwulili kuuvala unkosi wa kunani kwa Chapanga, iwanangana ngati mkolo nyumba mweiwusa vindu muchibana vya mashonga gamahele vyamupya na vyakadeni.”
Akawaambia, “Basi kila mwalimu wa sheria aliyefundishwa elimu ya Ufalme wa Mbinguni ni kama mwenye nyumba anayetoa kutoka ghala yake mali mpya na mali ya zamani.”
53 Yesu peamali kujova miluhumu yeniyo awukili pandu pala,
Yesu alipomaliza kutoa mifano hii, akaondoka.
54 akahamba kumuji wavi. Akatumbula kuwula vandu munyumba za kukonganekela Vayawudi, vevamyuwini vakakangasa, vakajova, “Mwenuyu apatili koki luhala ulu?” Na uhotola wa kuhenga gachinamtiti?
Alipofika mji wa kwao, akawafundisha watu katika sinagogi lao. Nao wakastaajabu, wakauliza, “Mtu huyu amepata wapi hekima hii na uwezo huu wa kufanya miujiza?”
55 Wu, mwenuyu lepi mwana wa yula mhongola mikongo? Na nyina waki ikemiwa lepi Maliya na valongo vaki, lepi Yakobo na Yosefu na Simoni na Yuda?
“Huyu si yule mwana wa seremala? Mama yake si yeye aitwaye Maria, nao ndugu zake si Yakobo, Yosefu, Simoni na Yuda?
56 Valumbu vaki voha nakutama pamonga na tete? Hinu agapatili koki mambu ago goha?
Nao dada zake wote, hawako hapa pamoja nasi? Mtu huyu amepata wapi basi mambo haya yote?”
57 Vabeli kumpokela, nambu Yesu akavajovela, “Mlota wa Chapanga itopeswa kila pandu, nambu nakutopeswa pamuji wa kunyumba yaki mwene!”
Wakachukizwa naye. Lakini Yesu akawaambia, “Nabii hakosi heshima, isipokuwa katika nchi yake na nyumbani kwake.”
58 Hinu ndava ya kubela kumsadika kwavi, Yesu nakuhenga gachinamtiti yamahele kula.
Naye hakufanya miujiza mingi huko kwa sababu ya kutokuamini kwao.

< Matei 13 >