< Matei 12 >
1 Lukumbi ulo, Yesu avi mukupita mumigunda Ligono la Kupumulila, Hinu, vawuliwa vaki njala yavavinili, vakatumbula kudenya nganu na kuyogola ngele zaki na kulya.
Wakati huo Yesu alipitia kwenye mashamba ya nafaka siku ya Sabato. Wanafunzi wake walikuwa na njaa, nao wakaanza kuvunja masuke ya nafaka na kuyala.
2 Vafalisayu pevagaweni genago, vakamjovela Yesu, “Lola, vawuliwa vaku vihenga lijambu lelibesiwi kuhenga pa Ligono la Kupumulila.”
Lakini Mafarisayo walipoona jambo hili, wakamwambia, “Tazama! Wanafunzi wako wanafanya jambo lisilo halali kufanywa siku ya Sabato.”
3 Yesu akayangula, “Wu, mwangasoma cheahengili Daudi na vayaki njala peyamvinili?
Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma alichofanya Daudi na wenzake walipokuwa na njaa?
4 Mwene ayingili mu Nyumba ya Chapanga na kulya mabumunda gala gegavikwi palongolo ya Chapanga. Mwene hati vayaki kawaka mweayidakiliwi kulya mabumunda genago. Mabumunda ago gaganikiwi kuliliwa na vamteta va Chapanga ndu.
Aliingia katika nyumba ya Mungu, akala mikate iliyowekwa wakfu, yeye na wenzake, jambo ambalo halikuwa halali kwao kufanya, isipokuwa makuhani peke yao.
5 Amala mwangasoma muchitabu cha Malagizu kuvya kila Ligono la Kupumulila vamteta va Chapanga vakugadenya malagizu ga Musa mu Nyumba ya Chapanga kuni vihololewa lepi kuvya vahokili?
Au hamjasoma katika Sheria kwamba siku ya Sabato makuhani huvunja sheria ya Sabato Hekaluni lakini hawahesabiwi kuwa na hatia?
6 Nambu hinu nikuvajovela kuvya penapa avi mkulu kuliku Nyumba ya Chapanga.
Nawaambia wazi kwamba, yeye aliye mkuu kuliko Hekalu yupo hapa.
7 Kuvya mumanyalila mana ya malovi aga ‘Nigana lipyana, nigani lepi teta zinu.’ Ngamuvahamwili lepi vandu vangahoka.
Kama mngekuwa mmejua maana ya maneno haya, ‘Nataka rehema, wala si dhabihu,’ msingewalaumu watu wasio na hatia,
8 Muni Mwana wa Mundu ndi Bambu wa Ligono la Kupumulila.”
kwa maana Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato.”
9 Yesu akawuka penapo, akahamba munyumba ya kukonganekela Vayawudi.
Yesu akaondoka mahali hapo, akaingia ndani ya sinagogi lao,
10 Kwavi na mundu mmonga mweagogodili chiwoko. Hinu, vandu vamkotili Yesu, “Wu, Malagizu giyidakila kumlamisa mundu pa Ligono la Kupumulila?” Vamlingili ndava vapatayi njila ya kumtakila.
na huko alikuwepo mtu aliyepooza mkono. Wakitafuta sababu ya kumshtaki Yesu, wakamuuliza, “Je, ni halali kuponya siku ya Sabato?”
11 Nambu Yesu akavajovela, “Wu, yani pagati yinu mweavi na limbelele laki, ligwilili muligodi, wu, akulihumisa lepi Ligono la Kupumulila?
Yesu akawaambia, “Ni nani miongoni mwenu, mwenye kondoo wake ambaye huyo kondoo akitumbukia shimoni siku ya Sabato hatamtoa?
12 Mundu itopeswa neju kuliku limbelele! Hinu ndi yiyidakiliwa kuhenga matendu gabwina pa Ligono la Kupumulila.”
Mtu ana thamani kubwa kuliko kondoo. Kwa hiyo ni halali kutenda mema siku ya Sabato.”
13 Kangi Yesu akamjovela mundu yula, “Talambula chiwoko chaku.” Mwene akachitalambula, ndi chalamili ngati chiwoko chingi chila.
Ndipo akamwambia yule mtu, “Nyoosha mkono wako.” Akaunyoosha, nao ukaponywa ukawa mzima kama ule mwingine.
14 Nambu Vafalisayu vakahuma kuvala na kujovesana, ndava ya mpangu wa kumkoma Yesu.
Lakini Mafarisayo wakatoka nje, wakafanya shauri baya juu ya Yesu jinsi watakavyoweza kumuua.
15 Nambu Yesu amanyalili mpangu wula, akawuka pandu pala. Msambi wa vandu wamlandili, akavalamisa vana matamu voha.
Lakini Yesu alipoyatambua mawazo yao, akaondoka mahali hapo. Watu wengi wakamfuata, naye akawaponya wagonjwa wao wote,
16 Avabesili vakotoka kuvajovela vandu mambu gaki,
akiwakataza wasiseme yeye ni nani.
17 muni lilovi la ajovili Mlota Isaya litimilayi.
Hii ilikuwa ili litimie lile neno lililonenwa kwa kinywa cha nabii Isaya kusema:
18 “Lola, mtumisi mwenimuhagwili, chiganu changu, mweanihekesa neju mtima wangu. Nikuuvika mpungu wangu panani yaki, namwene yati ikokosa uhamula wangu kwa milima yoha.
“Tazama mtumishi wangu niliyemchagua, mpendwa wangu, ninayependezwa naye. Nitaweka Roho wangu juu yake, naye atatangaza haki kwa mataifa.
19 Angahutana, amala kuywanga, mewa lwami lwaki nakuyuwanika munjila
Hatagombana wala hatapiga kelele, wala hakuna atakayesikia sauti yake njiani.
20 Mlahi weupondiki akuwudenya lepi, na utambi wewihuma lyohi wijimika lepi, mbaka kuhamula kwekuganikiwa kulongosa,
Mwanzi uliopondeka hatauvunja, na utambi unaofuka moshi hatauzima, mpaka atakapoifanya haki ishinde.
21 Vandu voha va milima yoha vakumhuvalila mwene.”
Katika Jina lake mataifa wataweka tumaini lao.”
22 Penapo vandu vamletili Yesu mundu ngalola mewa avi ngajova mweatalaliwi na mzuka. Yesu akamlamisa hati akahotola kujova na kulola.
Kisha wakamletea mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu, na alikuwa kipofu na bubu. Yesu akamponya, hata akaweza kusema na kuona.
23 Msambi woha wa vandu wewavi penapo ukakangasa na kujova, “Wu, mwenuyu lepi mwana wa Daudi?”
Watu wote wakashangaa na kusema, “Je, yawezekana huyu ndiye Mwana wa Daudi?”
24 Nambu Vafalisayu pevayuwini genago, vakajova, “Mundu uyu ivinga mizuka kwa uhotola wa Belizebuli mkulu wa mizuka.”
Lakini Mafarisayo waliposikia jambo hili wakasema, “Mtu huyu anatoa pepo wachafu kwa uwezo wa Beelzebuli, mkuu wa pepo wachafu.”
25 Yesu amanyili maholo gavi akajova, “Unkosi wowoha weulekangini chikundi chikundi wewitovana wene, wangahotola kusindimala mewawa na muji amala vandu va nyumba yimonga vevalekangini chikundi chikundi yati vigwa.”
Yesu alijua walichokuwa wakiwaza, hivyo akawaambia, “Kila ufalme ukigawanyika dhidi yake wenyewe huangamia. Hali kadhalika kila mji au watu wa nyumba moja waliogawanyika dhidi yao wenyewe hawawezi kusimama.
26 Ngati Setani akavinga mizuka yaki, akujing'anamukila mwene. Hinu unkosi waki usindimala wuli?
Kama Shetani akimtoa Shetani, atakuwa amegawanyika yeye mwenyewe. Basi ufalme wake utawezaje kusimama?
27 Ngati nyenye mwijova nene nikuyivinga mizuka kwa makakala ga Belizebuli, wu, valanda vinu vivinga kwa makakala ga yani? Ndava ya genago vandu vinu ndi vevakuvahamula nyenye!
Nami kama natoa pepo wachafu kwa nguvu za Beelzebuli, watu wenu je, wao hutoa pepo wachafu kwa uwezo wa nani? Hivyo basi, wao ndio watakaowahukumu.
28 Nambu ngati nivinga mzuka kwa makakala ga Mpungu wa Chapanga, ndi mumanya kuvya Unkosi wa Chapanga umali kuvabwelela.
Lakini kama mimi ninatoa pepo wachafu kwa Roho wa Mungu, basi Ufalme wa Mungu umekuja juu yenu.
29 “Ihotola wuli mundu kuizangila nyumba ya mundu mweavi na makakala na kumnyaga vindu vyaki, changali hoti kumkunga mundu ana makakala mwenuyo? Kangi ndi ahotola kumnyaga vindu vyaki.”
“Au tena, mtu awezaje kuingia katika nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuteka nyara mali zake asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu? Akishamfunga, ndipo hakika anaweza kuteka nyara mali zake.
30 “Mundu yeyoha mweanganilanda nene, akunibela, na mundu yeyoha mweangayola pamonga na nene, idandasa.
“Mtu asiyekuwa pamoja nami yu kinyume nami, na mtu ambaye hakusanyi pamoja nami, hutawanya.
31 Ndava yeniyo nikuvajovela, vandu yati vilekekeswa kumbudila kwavi Chapanga na maligu gavi goha, nambu yati ilekekeswa lepi yula mweakumliga Mpungu Msopi.
Kwa hiyo nawaambia, kila dhambi na kufuru watu watasamehewa, lakini mtu atakayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
32 Kangi, mundu yeyoha mweijova lilovi la kumbela Mwana wa Mundu yati ilekekeswa, nambu mundu yeyoha mweijova lilovi la kumbela Mpungu Msopi, ilekekeswa lepi pamulima uwu hati pamulima weubwela.” (aiōn )
Mtu yeyote atakayesema neno dhidi ya Mwana wa Adamu atasamehewa, lakini yeyote anenaye neno dhidi ya Roho Mtakatifu hatasamehewa, iwe katika ulimwengu huu au katika ulimwengu ujao. (aiōn )
33 “Mkongo wakavya wabwina na matunda gaki yati givya gabwina mewawa, mkongo wakavya uhakau na matunda gaki givya gahakau mewa. Ndi mkongo umanyikana ndava ya matunda gaki.
“Ufanye mti kuwa mzuri, nayo matunda yake yatakuwa mazuri. Au ufanye mti kuwa mbaya, na matunda yake yatakuwa mabaya. Kwa maana mti hutambulika kwa matunda yake.
34 Nyenye mwachiveleku cha liyoka! Mwihotola wuli kujova mambu gabwina kuni mwavene mwavahakau? Muni mundu ijova gala gegamemili mumtima waki.
Enyi uzao wa nyoka! Mnawezaje kunena mambo mema, wakati ninyi ni waovu? Kwa maana kinywa cha mtu huyanena yale yaliyoujaza moyo wake.
35 Mundu mbwina iwusa mambu gabwina muchibana chaki chabwina, mewawa mundu mhakau iwusa mambu gahakau muchibana chaki chihakau.”
Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka hazina ya mambo mema yaliyohifadhiwa ndani yake, naye mtu mwovu hutoa yaliyo maovu kutoka hazina ya mambo maovu yaliyohifadhiwa ndani yake.
36 “Hinu nikuvajovela, ligono la uhamula kila mundu yati ihamuliwa kwa kila lilovi lihakau leajovili.
Lakini nawaambia, katika siku ya hukumu watu watatoa hesabu kuhusu kila neno lisilo maana walilonena.
37 Muni malovi gaku wamwene yati wiyidakiliwa umganisi Chapanga, na kwa malovi gaku wamwene yati wihamuliwa kuvya uhokili.”
Kwa maana kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa.”
38 Kangi pagati ya vawula va malagizu na Vafalisayu vamjovili Yesu, “Muwula tigana kulola ulangisu kuhuma kwa veve.”
Kisha baadhi ya Mafarisayo na walimu wa sheria wakamwambia, “Mwalimu, tunataka kuona ishara kutoka kwako.”
39 Mwene akayangula, “Chiveleku chihakau changali sadika! Mwigana ulangisu, yati mwipata lepi ulangisu, nambu ndi wulawula wa Yona mweavi mlota wa Chapanga.
Lakini yeye akawajibu, “Kizazi kiovu na cha uzinzi kinaomba ishara! Lakini hakitapewa ishara yoyote isipokuwa ile ishara ya nabii Yona.
40 Ngati Yona cheatamili magono gadatu kilu na muhi mulileme la somba yivaha, mewawa Mwana wa Mundu yati itama mugati ya ndima magono gadatu muhi na kilu.
Kwa maana kama vile Yona alivyokuwa ndani ya tumbo la nyangumikwa siku tatu, usiku na mchana, vivyo hivyo Mwana wa Adamu atakuwa katika moyo wa nchi siku tatu, usiku na mchana.
41 Ligono la uhamula vandu va ku Ninawi yati viyima pamonga na chiveleku ichi na kuchihamula, ndava muni vene vamali kumng'anamukila Chapanga lukumbi Yona peavakokosili. Hinu apa avi mkulu kuliku Yona!
Siku ya hukumu watu wa Ninawi watasimama pamoja na kizazi hiki na kukihukumu; kwa maana wao walitubu waliposikia mahubiri ya Yona. Na tazama, hapa yupo yeye aliye mkuu kuliko Yona.
42 Nkosi wa chidala wa muji wa Sheba yati ihumila Kwelitipama lilanga lukumbi lwa uhamula wa chiveleku ichi, namwene yati akuchihamula kuvya chihokili. Muni mwene agendili kuhuma kutali, abwelili kuhuma kumulima waki, kuyuwana malovi ga luhala ga Solomoni, kumbi apa avi mkulu kuliku Solomoni.”
Malkia wa Kusini atasimama wakati wa hukumu na kukihukumu kizazi hiki. Kwa kuwa yeye alikuja kutoka miisho ya dunia ili kuisikiliza hekima ya Solomoni. Na hapa yupo aliye mkuu kuliko Solomoni.”
43 “Mzuka ngati uvingiwi kwa mundu, ulyungalyunga kulugangatu kulonda pandu pa kupumulila. Akupapata lepi pandu,
“Pepo mchafu amtokapo mtu, hutangatanga katika sehemu zisizo na maji akitafuta mahali pa kupumzika, lakini hapati.
44 Kangi akujijovela, ‘Niwuya kavili kunyumba yangu mwenihumili.’ Peiwuya akuyikolela nyumba yila yivii waka yifyagiliwi na kupambwa.
Ndipo husema, ‘Nitarudi kwenye nyumba yangu nilikotoka.’ Naye arudipo huikuta ile nyumba ikiwa tupu, imefagiliwa na kupangwa vizuri.
45 Kangi ihamba kuyitola mizuka yingi saba, hihakau neju kuliku mwene, yoha ibwela kuyingila kwa mundu yula. Mundu yula ivya mhakau neju kuliku peatumbwili. Hinu ndi yati yivya kwa chiveleku ichi chihakau.”
Kisha huenda na kuwaleta pepo wachafu wengine saba wabaya kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo. Nayo hali ya mwisho ya yule mtu huwa ni mbaya kuliko ile ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kiovu.”
46 Yesu peavi akona ilongela na vandu, lola, nyina waki na valongo vaki vakahika na kuyima kuvala, vagana kulongela nayu.
Wakati alikuwa angali anazungumza na makutano, mama yake na ndugu zake wakasimama nje wakitaka kuongea naye.
47 Hinu mundu mmonga akamjovela, “Yuwanila nyina waku na valongo vaku vavi kuvala, vigana kulongela na veve.”
Ndipo mtu mmoja akamwambia, “Tazama, mama yako na ndugu zako wamesimama nje, wanataka kuongea na wewe.”
48 Nambu Yesu akamyangula mundu yula “Nyina wangu ndi yani? Na valongo vangu ndi vayani?”
Lakini yeye akamjibu na kumwambia yule mtu, “Mama yangu ni nani, nao ndugu zangu ni nani?”
49 Kangi akatalambula chiwoko chaki na kuvalangisa vawuliwa vaki, akajova, “Ava ndi nyina wangu na valongo vangu!
Akawanyooshea mkono wanafunzi wake, akasema, “Hawa hapa ndio mama yangu na ndugu zangu!
50 Muni mundu yeyoha mweihenga geigana Dadi wangu mweavili kunani, mwenuyo ndi mlongo wangu mlumbu wangu na nyina wangu.”
Kwa maana yeyote afanyaye mapenzi ya Baba yangu wa mbinguni, huyo ndiye ndugu yangu, na dada yangu na mama yangu.”