< Yakobo 4 >
1 Ngondo na kukomana kwinu kuhuma koki? Kwihuma muminogo yinu yihakau ndi zezikomana mugati ya higa zinu.
Ni kitu gani kinachosababisha mapigano na ugomvi miongoni mwenu? Je, haya hayatokani na tamaa zenu zinazoshindana ndani yenu?
2 Mnogela neju vindu na ndava muni mwipata lepi nambu mujitendekili hati kukoma. Mwilola wihu kupata vindu vyevavi navyu vangi nambu mukuvipata lepi ndi muvi na luhonda na komana. Mpata lepi chemwigana muni mukumuyupa lepi Chapanga.
Mnatamani lakini hampati, kwa hiyo mwaua. Mwatamani kupata lakini hampati vile mnavyotaka, kwa hiyo mnajitia katika magomvi na mapigano. Mmepungukiwa kwa sababu hammwombi Mungu.
3 Kavili, pemwiyupa mupata lepi ndava muni mwiyupa kwa maholo gahakau, mwiyupa ndava ya kuyukutisa mnogo winu.
Mnapoomba hampati kwa sababu mnaomba kwa nia mbaya, ili mpate kuvitumia hivyo mtakavyopata kwa tamaa zenu.
4 Nyenye ndi vandu mwangasadikika ngati vakemi. Mwimanya lepi kuvya nkozi wa mulima uwu ndi kuvya likoko wa Chapanga? Mundu yoyoha mweigana kuvya nkozi wa mulima ivya likoko wa Chapanga.
Ninyi wanaume na wanawake wazinzi, hamjui ya kwamba urafiki na dunia ni uadui na Mungu? Kwa hiyo mtu yeyote anayetaka kuwa rafiki wa dunia hufanyika adui wa Mungu.
5 Mkoto kuholalela kuvya Mayandiku Gamsopi gijova malovi gawaka, pegijova, “Mpungu mweavikiwi na Chapanga avi na wihu uvaha ndava yitu ya Mpungu Msopi mweamvikii mugati yitu.”
Au mwadhani kwamba Andiko lasema bure kuwa huyo Roho ambaye Mungu amemweka ndani yetu hututamani kiasi cha kuona wivu?
6 Nambu, ubwina wetipewa na Chapanga una makakala neju, ngati chegijova Mayandiku, “Chapanga akuvatova vevimeka nambu akuvapela vangolongondi ubwina waki.”
Lakini yeye hutupatia neema zaidi. Hii ndiyo sababu Andiko husema: “Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema.”
7 Hinu, mujivika pahi ya Chapanga, mumbela Setani ndi yati akuvatila.
Basi mtiini Mungu. Mpingeni ibilisi, naye atawakimbia.
8 Mvya papipi na Chapanga, ni mwene yati ibwela papipi na nyenye. Msanja mawoko ginu nyenye mwemkumbudila Chapanga! Mjinyambisa mitima yinu vahomela nyenye!
Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu ninyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu ninyi wenye nia mbili.
9 Mvya ngolongondi, mvemba na kuwombeleza, luheku lwinu luvya kuvemba, kuheka kwinu kuvya ungolongondi.
Huzunikeni, ombolezeni na kulia. Kicheko chenu na kigeuzwe kuwa kuomboleza, na furaha yenu kuwa huzuni.
10 Mvya ngolongondi palongolo ya BAMBU, na mwene yati akuvakwiha.
Jinyenyekezeni mbele za Bwana, naye atawainua.
11 Valongo, mkoto kulungamilana nyenye kwa nyenye. Mwakumjova mlongo waki na kumhamula, akuijova na kuihamula malagizu. Ngati ukuyihamula malagizu hinu veve ukuyidakila lepi nambu ukuyihamula.
Ndugu, msineneane mabaya ninyi kwa ninyi. Mtu yeyote anayesema mabaya dhidi ya ndugu yake au kumhukumu anasema dhidi ya sheria na kuihukumu. Unapoihukumu sheria, basi huishiki sheria bali umekuwa hakimu wa kuihukumu hiyo sheria.
12 Chapanga mwene ndi mwavikili malagizu na kuhamula vandu. Ndi mwene ndu mweihotola kusangula vandu na kukoma. Hinu, veve ndi yani hati uvahamula vayaku?
Yuko Mtoa sheria mmoja tu na yeye peke yake ndiye Hakimu, ndiye awezaye kuokoa au kuangamiza. Lakini wewe ni nani hata umhukumu jirani yako?
13 Hinu, myuwanila mwemjova, “Lelu amala chilau yati tihamba kumuji nunuyu na kutama kwenuko mwaka woha kugulisa vindu na kupata mashonga.”
Basi sikilizeni ninyi msemao, “Leo au kesho tutakwenda katika mji huu ama ule tukae humo mwaka mmoja, tufanye biashara na kupata faida.”
14 Nyenye mmanyili lepi gegihumila chilau muwumi winu! Nyenye ngati lyohi lelihumalila lukumbi ndu na kuyaga.
Lakini hamjui hata litakalotukia kesho. Maisha yenu ni nini? Ninyi ni ukungu ambao huonekana kwa kitambo kidogo kisha hutoweka.
15 Mganikiwa kujova naha. “BAMBU akagana yati titama na kukita chenichi amala chila.”
Badala yake, inawapasa kusema, “Kama Bwana akipenda, tutaishi na kufanya hili ama lile.”
16 Nambu hinu mwimeka na kujilumba. Kumeka kwenuko ndi uhakau.
Kama ilivyo sasa, mnajisifu na kujigamba. Kujisifu kwa namna hiyo ni uovu.
17 Nambu, mundu yoyoha mweamanyili lijambu labwina leiganikiwa kukitwa, nambu ikita lepi ndi akumbudila Chapanga.
Basi mtu yeyote anayejua jema limpasalo kutenda, lakini asilitende, mtu huyo anatenda dhambi.