< 1 Timoti 2 >

1 Kutumbula hoti mumjovela Chapanga chemwigana, mumyupa Chapanga, muvayupila vandu vangi na mumsengusa Chapanga ndava ya vandu voha.
Awali ya yote, nasihi kwamba dua, sala, maombezi na shukrani zifanyike kwa ajili ya watu wote:
2 Muyupa ndava ya vankosi na vandu voha vevana uhotola, muni mtama matamilu changali kulyunga na uteke pamonga na luhala lwa Chapanga na matendu gabwina.
kwa ajili ya wafalme na wale wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi kwa amani na utulivu, katika uchaji wote wa Mungu na utakatifu.
3 Lijambu lenili labwina na lakumganisa Chapanga msangula witu,
Jambo hili ni jema, tena linapendeza machoni pa Mungu Mwokozi wetu,
4 mweigana vandu voha vasanguliwayi na vaumanya uchakaka.
anayetaka watu wote waokolewe na wafikie kuijua kweli.
5 Muni avili Chapanga mmonga, na mewa avili mmonga mweakuvatepulanisa vandu na Chapanga, mundu mwenuyo ndi Kilisitu Yesu,
Kwa maana kuna Mungu mmoja na mpatanishi mmoja kati ya Mungu na wanadamu, yaani mwanadamu Kristo Yesu,
6 mweajiwusili mwene kuvasangula vandu voha. Wenuwu wavi ulangisu, lukumbi lwabwina pawahikili, kuvya Chapanga igana kuvasangula vandu voha.
aliyejitoa mwenyewe kuwa fidia kwa ajili ya wanadamu wote: jambo hili lilishuhudiwa kwa wakati wake ufaao.
7 Ndava yeniyo nene natumwili kuvya namtumu na muwula wa vandu vangali Vayawudi, niukokosa ujumbi wa sadika na uchakaka. Nijova chakaka, lepi udese!
Nami kwa kusudi hili nimewekwa niwe mhubiri na mtume (nasema kweli katika Kristo wala sisemi uongo), mwalimu wa watu wa Mataifa katika imani na kweli.
8 Ndi popoha pemwikonganeka kuyupa Chapanga nigana vagosi vayupayi, vagosi vevajiwusili kujivika chakaka kwa Chapanga na vevihotola kukwesa mawoko gavi changali ligoga amala ndindani.
Nataka kila mahali wanaume wasali wakiinua mikono mitakatifu pasipo hasira wala kugombana.
9 Mewawa, nikuvagana vadala vangolongondi na kuwala nyula za utopesa lepi ndava ya kujinyambisa lepi kwa mitindu ya kukangasa kutiva mayunju, amala kujinyambisa kwa vindu vyabwina, lulu amala nyula za mashonga gamahele,
Vivyo hivyo nataka wanawake wajipambe kwa adabu na kwa heshima katika mavazi yanayostahili, si kwa kusuka nywele, kuvalia dhahabu, lulu au mavazi ya gharama kubwa,
10 nambu kujinyambisa kwavi kuganikiwa kuvya mumatendu gabwina ngati chayikuvagana vadala vevakumyidakila Chapanga.
bali kwa matendo mazuri kama iwapasavyo wanawake wanaokiri kuwa wanamcha Mungu.
11 Vadala viganikiwa kutama nuu na utopesa lukumbi pevakujiwula lilovi la Chapanga.
Mwanamke na ajifunze kwa utulivu na kwa utiifu wote.
12 Nene nigana lepi mdala amuwula amala amlongosa mgosi, iganikiwa kutama nuu.
Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha au kuwa na mamlaka juu ya mwanaume. Mwanamke inampasa kukaa kimya.
13 Muni Adamu awumbiwi hoti, kangi ndi Eva.
Kwa maana Adamu aliumbwa kwanza, kisha Eva.
14 Ndi lepi Adamu mweakongiwi, nambu mdala mweakongiwi na kudenya mhilu wa Chapanga.
Wala si Adamu aliyedanganywa, bali ni mwanamke aliyedanganywa akawa mkosaji.
15 Nambu vadala yati viveleka bwina ngati vasindimili musadika na uganu na ungolongondi.
Lakini mwanamke ataokolewa kwa kuzaa kwake, kama wakiendelea kudumu katika imani, upendo na utakatifu, pamoja na kuwa na kiasi.

< 1 Timoti 2 >