< Psalmi 31 >

1 Dāvida dziesma. Dziedātāju vadonim. Uz tevi, Kungs, es paļaujos, nepamet mani kaunā mūžīgi, izglāb mani caur Tavu taisnību.
Kwa kiongozi wa muziki. Zaburi ya Daudi. In wewe, Yahwe, nakimbilia usalama; usiniache niaibishwe. Katika haki yako uniokoe.
2 Atgriez Savu ausi pie manis, izglāb mani drīz, esi man par stipru patvērumu, par stipru pili man palīdzēt.
Unisikie; uniokoe haraka; uwe mwamba wangu wa usalama, ngome ya kuniokoa.
3 Jo Tu esi mans akmens kalns un mana stiprā pils, un Tava Vārda dēļ ved un vadi mani.
Kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu; kwa hiyo kwa ajili ya jina lako, uniongoze na unielekeze.
4 Izved mani no tīkla, ko tie priekš manis paslēpuši, jo Tu esi mans stiprums.
Unitoe katika mtego ambao wameuficha kwa ajili yangu, kwa kuwa wewe ni usalama wangu.
5 Tavā rokā es pavēlu savu garu, Tu mani esi atpestījis, Kungs, Tu stiprais patiesības Dievs.
Mikononi mwako naikabidhi roho yangu; nawe utaniokoa, Yahwe, mwenye kuaminika.
6 Es ienīstu tos, kas dodas uz blēņu mācībām, bet es paļaujos uz To Kungu.
Ninawachukia wale wanaotumikia miungu isiyo na maana, bali ninaamini katika Yahwe.
7 Es priecāšos un līksmošos par Tavu žēlastību, ka Tu uzlūko manas bēdas, un vērā lieci manu dvēseli bailēs,
Nitafurahi na kushangilia katika uaminifu wa agano lako, kwa kuwa uliyaona mateso yangu; wewe uliijua dhiki ya moyo wangu.
8 Un nenodod mani ienaidnieka rokā; Tu manām kājām lieci stāvēt plašā vietā.
Wewe haujaniweka kwenye mkono wa maadui zangu. Nawe umeiweka miguu yangu mahali pa wazi papana.
9 Esi man žēlīgs, ak Kungs! Jo man ir bail', no skumības ir sarucis mans vaigs, mana dvēsele un mana miesa.
Uniurumie, Yahwe, kwa maana niko katika dhiki; macho yangu yanafifia kwa huzuni pamoja na moyo wangu na mwili wangu.
10 Jo mana dzīvība ir nonīkusi caur noskumšanu un mani gadi caur nopūšanos, mans spēks caur manu noziegumu ir sakritis, un mani kauli ir sanīkuši.
Kwa kuwa maisha yangu yamechoshwa kwa huzuni na miaka yangu kwa kuugua kwangu. Nimekuwa dhaifu kwa sababu ya dhambi zangu, na mifupa yangu inachakaa.
11 Caur visiem saviem pretiniekiem es esmu par kaunu tapis saviem kaimiņiem, un saviem pazīstamiem par biedēkli; kas mani uz ielām redz, tie bēg no manis.
Kwa sababu ya maadui zangu wote, watu wananibeza; majirani zangu wanaishangaa hali yangu, na wale wanao nifahamu wanashtuka. Wale wanionao mitaani hunikimbia.
12 Es sirdīs esmu aizmirsts kā mironis, esmu tapis kā sadauzīts trauks.
Nimesahaulika kama mtu aliye kufa ambaye hakuna mtu anaye mfikiria. Niko kama chungu kilicho pasuka.
13 Jo es dzirdu no daudziem lamāšanās: bailība ir visapkārt; kad tie kopā sarunājās pret mani, tie domā paņemt manu dzīvību.
Kwa maana nimesikia minong'ono ya wengi, habari za kutisha kutoka pande zote kwa pamoja wamepanga njama kinyume na mimi. Wao wanapanga njama ya kuniua.
14 Bet es cerēju uz Tevi, Kungs; es saku tā: Tu esi mans Dievs.
Bali mimi ninakuamini wewe, Yahwe; Ninasema, “Wewe ni Mungu wangu.”
15 Mani laiki stāv Tavā rokā; izglāb mani no manu ienaidnieku rokas un no tiem, kas mani vajā.
Hatima yangu iko mikononi mwako. Uniokoe mikononi mwa maadui zangu na wale wanao nifukuzia.
16 Liec Savam vaigam spīdēt pār Savu kalpu, atpestī mani caur Tavu žēlastību.
Nuru ya uso wako imuangazie mtumishi wako; uniokoe katika uaminifu wa agano lako.
17 Kungs, neliec man kaunā palikt, jo es Tevi piesaucu; lai bezdievīgie paliek kaunā un top klusināti ellē. (Sheol h7585)
Usiniache niaibishwe, Yahwe; kwa maana ninakuita wewe! Waovu waaibishwe! Na wanyamaze kimya kuzimuni. (Sheol h7585)
18 Lai mēmas paliek melkuļu lūpas kas bezkaunīgi runā pret taisno ar lepnību un nicināšanu.
Na inyamazishwe midomo midanganyifu ambayo husema maneno mabaya kuhusu watu wenye haki huku wakiwa na kiburi na dharau.
19 Cik liels ir Tavs labums, ko Tu esi glabājis tiem, kas Tevi bīstas, un sataisījis tiem, kas cilvēku priekšā uz Tevi paļaujas.
Uzuri wako ni wa namna gani nao umeuhifadhii kwa ajili ya wale wanao kuheshimu sana, ambao wewe huufanya kwa ajili ya wale ambao hukimbilia kwako kwa ajili ya usalama mbele ya watoto wote wa wanadamu!
20 Tu tos slēpi Sava vaiga ēnā priekš cilvēku dumpjiem, Tu tos glabā kā namā priekš rējēju mēlēm.
Katika makao ya uwepo wako, wewe huwaficha mbali na njama za watu. Wewe huwaficha mahali salama na ndimi zenye vurugu.
21 Slavēts lai ir Tas Kungs, jo Viņš brīnišķi man parādījis Savu žēlastību tā kā stiprā pilsētā.
Atukuzwe Yahwe, kwa maana yeye alinionesha maajabu ya uaminifu wa agano lake mahali nilipoishi.
22 Gan es sacīju savās bailēs: es esmu atmests no Tava vaiga; taču Tu klausīji manas sirds lūgšanas balsi, kad es Tevi piesaucu.
Ingawa kwa haraka zangu nilisema, “Nimeondolewa machoni pako,” bali wewe ulisikia kusihi kwangu nilipokulilia wewe.
23 Mīlējiet To Kungu, visi Viņa svētie; Tas Kungs pasargā tos ticīgos, un atmaksā papilnam tam, kas dara pārgalvību.
Enyi wafuasi waaminifu, mpendeni Yahwe, Yahwe huwalinda waaminifu, lakini huwalipa wakaidi ipasavyo.
24 Esiet droši un stipri savā sirdī, visi, kas cerējiet uz To Kungu.
Iweni imara na jasiri, ninyi nyote mnao mwamini Mungu kuwasaidia.

< Psalmi 31 >