< Psalmorum 81 >

1 in finem pro torcularibus Asaph exultate Deo adiutori nostro iubilate Deo Iacob
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Asafu. Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu; mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!
2 sumite psalmum et date tympanum psalterium iucundum cum cithara
Anzeni wimbo, pigeni matari, pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.
3 bucinate in neomenia tuba in insigni die sollemnitatis nostrae
Pigeni baragumu za pembe za kondoo dume wakati wa Mwandamo wa Mwezi, na wakati wa mwezi mpevu, katika siku ya Sikukuu yetu;
4 quia praeceptum Israhel est et iudicium Dei Iacob
hii ni amri kwa Israeli, agizo la Mungu wa Yakobo.
5 testimonium in Ioseph posuit illud cum exiret de terra Aegypti linguam quam non noverat audivit
Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu alipotoka dhidi ya Misri, huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa.
6 devertit ab oneribus dorsum eius manus eius in cofino servierunt
Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao; mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
7 in tribulatione invocasti me et liberavi te exaudivi te in abscondito tempestatis probavi te apud aquam Contradictionis diapsalma
Katika shida yako uliniita nami nikakuokoa, nilikujibu katika mawingu yenye ngurumo; nilikujaribu katika maji ya Meriba.
8 audi populus meus et contestabor te Israhel si audias me
“Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya: laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!
9 non erit in te deus recens nec adorabis deum alienum
Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu; msimsujudie mungu wa kigeni.
10 ego enim sum Dominus Deus tuus qui eduxi te de terra Aegypti dilata os tuum et implebo illud
Mimi ni Bwana Mungu wako, niliyekutoa nchi ya Misri. Panua sana kinywa chako nami nitakijaza.
11 et non audivit populus meus vocem meam et Israhel non intendit mihi
“Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza; Israeli hakutaka kunitii.
12 et dimisi illos secundum desideria cordis eorum ibunt in adinventionibus suis
Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao wafuate mashauri yao wenyewe.
13 si populus meus audisset me Israhel si in viis meis ambulasset
“Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza, kama Israeli wangalifuata njia zangu,
14 pro nihilo forsitan inimicos eorum humiliassem et super tribulantes eos misissem manum meam
ningaliwatiisha adui zao kwa haraka, na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao!
15 inimici Domini mentiti sunt ei et erit tempus eorum in saeculo
Wale wanaomchukia Bwana wangalinyenyekea mbele zake, na adhabu yao ingedumu milele.
16 et cibavit illos ex adipe frumenti et de petra melle saturavit illos
Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora, na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”

< Psalmorum 81 >