< Psalmorum 50 >

1 psalmus Asaph Deus deorum Dominus locutus est et vocavit terram a solis ortu usque ad occasum
Zaburi ya Asafu. Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana, asema na kuiita dunia, tangu mawio ya jua hadi mahali pake liendapo kutua.
2 ex Sion species decoris eius
Kutoka Sayuni, penye uzuri mkamilifu, Mungu anaangaza.
3 Deus manifeste veniet Deus noster et non silebit ignis in conspectu eius exardescet et in circuitu eius tempestas valida
Mungu wetu anakuja na hatakaa kimya, moto uteketezao unamtangulia, akiwa amezungukwa na tufani kali.
4 advocabit caelum desursum et terram discernere populum suum
Anaziita mbingu zilizo juu, na nchi, ili aweze kuwahukumu watu wake:
5 congregate illi sanctos eius qui ordinant testamentum eius super sacrificia
“Nikusanyieni watu wangu waliowekwa wakfu, waliofanya agano nami kwa dhabihu.”
6 et adnuntiabunt caeli iustitiam eius quoniam Deus iudex est diapsalma
Nazo mbingu zinatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ni hakimu.
7 audi populus meus et loquar tibi Israhel et testificabor tibi Deus Deus tuus ego sum
“Sikieni, enyi watu wangu, nami nitasema, ee Israeli, nami nitashuhudia dhidi yenu: Mimi ndimi Mungu, Mungu wenu.
8 non in sacrificiis tuis arguam te holocausta autem tua in conspectu meo sunt semper
Sikukemei kwa sababu ya dhabihu zako, au sadaka zako za kuteketezwa, ambazo daima ziko mbele zangu.
9 non accipiam de domo tua vitulos neque de gregibus tuis hircos
Sina haja ya fahali wa banda lako, au mbuzi wa zizi lako.
10 quoniam meae sunt omnes ferae silvarum iumenta in montibus et boves
Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
11 cognovi omnia volatilia caeli et pulchritudo agri mecum est
Ninamjua kila ndege mlimani, nao viumbe wa kondeni ni wangu.
12 si esuriero non dicam tibi meus est enim orbis terrae et plenitudo eius
Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, kwa maana ulimwengu ni wangu, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
13 numquid manducabo carnes taurorum aut sanguinem hircorum potabo
Je, mimi hula nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi?
14 immola Deo sacrificium laudis et redde Altissimo vota tua
Toa sadaka za shukrani kwa Mungu, timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana,
15 et invoca me in die tribulationis et eruam te et honorificabis me diapsalma
na uniite siku ya taabu; nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”
16 peccatori autem dixit Deus quare tu enarras iustitias meas et adsumis testamentum meum per os tuum
Lakini kwake mtu mwovu, Mungu asema: “Una haki gani kunena sheria zangu au kuchukua agano langu midomoni mwako?
17 tu vero odisti disciplinam et proiecisti sermones meos retrorsum
Unachukia mafundisho yangu na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
18 si videbas furem currebas cum eo et cum adulteris portionem tuam ponebas
Unapomwona mwizi, unaungana naye, unapiga kura yako pamoja na wazinzi.
19 os tuum abundavit malitia et lingua tua concinnabat dolos
Unakitumia kinywa chako kwa mabaya na kuuongoza ulimi wako kwa hila.
20 sedens adversus fratrem tuum loquebaris et adversus filium matris tuae ponebas scandalum
Wanena daima dhidi ya ndugu yako na kumsingizia mwana wa mama yako.
21 haec fecisti et tacui existimasti inique quod ero tui similis arguam te et statuam contra faciem tuam
Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya, ukafikiri Mimi nami ni kama wewe. Lakini nitakukemea na kuweka mashtaka mbele yako.
22 intellegite nunc haec qui obliviscimini Deum nequando rapiat et non sit qui eripiat
“Yatafakarini haya, ninyi mnaomsahau Mungu, ama sivyo nitawararua vipande vipande, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwaokoa:
23 sacrificium laudis honorificabit me et illic iter quod ostendam illi salutare Dei
Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi, naye aiandaa njia yake ili nimwonyeshe wokovu wa Mungu.”

< Psalmorum 50 >