< Psalmorum 111 >
1 alleluia reversionis Aggei et Zacchariae confitebor tibi Domine in toto corde meo in consilio iustorum et congregatione
Msifuni Bwana. Nitamtukuza Bwana kwa moyo wangu wote, katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko.
2 magna opera Domini exquisita in omnes voluntates eius
Kazi za Bwana ni kuu, wote wanaopendezwa nazo huzitafakari.
3 confessio et magnificentia opus eius et iustitia eius manet in saeculum saeculi
Kazi zake zimejaa fahari na utukufu, haki yake hudumu daima.
4 memoriam fecit mirabilium suorum misericors et miserator Dominus
Amefanya maajabu yake yakumbukwe, Bwana ni mwenye neema na huruma.
5 escam dedit timentibus se memor erit in saeculum testamenti sui
Huwapa chakula wale wanaomcha, hulikumbuka agano lake milele.
6 virtutem operum suorum adnuntiabit populo suo
Amewaonyesha watu wake uwezo wa kazi zake, akiwapa nchi za mataifa mengine.
7 ut det illis hereditatem gentium opera manuum eius veritas et iudicium
Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki, mausia yake yote ni ya kuaminika.
8 fidelia omnia mandata eius confirmata in saeculum saeculi facta in veritate et aequitate
Zinadumu milele na milele, zikifanyika kwa uaminifu na unyofu.
9 redemptionem misit populo suo mandavit in aeternum testamentum suum sanctum et terribile nomen eius
Aliwapa watu wake ukombozi, aliamuru agano lake milele: jina lake ni takatifu na la kuogopwa.
10 initium sapientiae timor Domini intellectus bonus omnibus facientibus eum laudatio eius manet in saeculum saeculi
Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, wote wanaozifuata amri zake wana busara. Sifa zake zadumu milele.