< Psalmorum 140 >

1 Psalmus David, in finem. Eripe me Domine ab homine malo: a viro iniquo eripe me.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, niokoe, kutoka kwa watu waovu; nilinde na watu wenye jeuri,
2 Qui cogitaverunt iniquitates in corde: tota die constituebant praelia.
ambao hupanga mipango mibaya mioyoni mwao, na kuchochea vita siku zote.
3 Acuerunt linguas suas sicut serpentes: venenum aspidum sub labiis eorum.
Wao hufanya ndimi zao kali kama za nyoka, sumu ya nyoka iko midomoni mwao.
4 Custodi me Domine de manu peccatoris: et ab hominibus iniquis eripe me. Qui cogitaverunt supplantare gressus meos:
Ee Bwana, niepushe na mikono ya waovu; nilinde na watu wenye jeuri wanaopanga kunikwaza miguu yangu.
5 absconderunt superbi laqueum mihi: Et funes extenderunt in laqueum: iuxta iter scandalum posuerunt mihi.
Wenye kiburi wameficha mtego wa kuninasa, wametandaza kamba za wavu wao, wametega mitego kwenye njia yangu.
6 Dixi Domino: Deus meus es tu: exaudi Domine vocem deprecationis meae.
Ee Bwana, ninakuambia, “Wewe ni Mungu wangu.” Ee Bwana, usikie kilio changu na kunihurumia.
7 Domine, Domine virtus salutis meae: obumbrasti super caput meum in die belli:
Ee Bwana Mwenyezi, Mwokozi wangu mwenye nguvu, unikingaye kichwa changu siku ya vita:
8 Ne tradas me Domine a desiderio meo peccatori: cogitaverunt contra me, ne derelinquas me, ne forte exaltentur.
Ee Bwana, usiwape waovu matakwa yao, usiache mipango yao ikafanikiwa, wasije wakajisifu.
9 Caput circuitus eorum: labor labiorum ipsorum operiet eos.
Vichwa vya wanaonizunguka vifunikwe na shida zinazosababishwa na midomo yao.
10 Cadent super eos carbones, in ignem deiicies eos: in miseriis non subsistent.
Makaa ya mawe ya moto na yawaangukie! Na watupwe motoni, katika mashimo ya matope, wasiinuke tena kamwe.
11 Vir linguosus non dirigetur in terra: virum iniustum mala capient in interitu.
Wasingiziaji wasifanikiwe katika nchi; maafa na yawawinde watu wenye jeuri.
12 Cognovi quia faciet Dominus iudicium inopis: et vindictam pauperum.
Najua kwamba Bwana huwapatia maskini haki, na kuitegemeza njia ya mhitaji.
13 Verumtamen iusti confitebuntur nomini tuo: et habitabunt recti cum vultu tuo.
Hakika wenye haki watalisifu jina lako, na waadilifu wataishi mbele zako.

< Psalmorum 140 >