< Job 18 >
1 Respondens autem Baldad Suhites, dixit:
Bildadi Mshuhi akajibu:
2 Usque ad quem finem verba iactabitis? intelligite prius, et sic loquamur.
“Je, ni lini utafika mwisho wa maneno haya? Uwe mwenye busara, nasi ndipo tutakapoweza kuongea.
3 Quare reputati sumus ut iumenta, et sorduimus coram vobis?
Kwa nini sisi tunafikiriwa kama wanyama, na kuonekana wajinga machoni pako?
4 Qui perdis animam tuam in furore tuo, numquid propter te derelinquetur terra, et transferentur rupes de loco suo?
Wewe unayejirarua mwenyewe vipande vipande katika hasira yako, je, dunia iachwe kwa ajili yako wewe? Au ni lazima miamba iondolewe mahali pake?
5 Nonne lux impii extinguetur, nec splendebit flamma ignis eius?
“Taa ya mwovu imezimwa, nao mwali wa moto wake umezimika.
6 Lux obtenebrescet in tabernaculo illius, et lucerna, quae super eum est, extinguetur.
Mwanga hemani mwake umekuwa giza; taa iliyo karibu naye imezimika.
7 Arctabuntur gressus virtutis eius, et praecipitabit eum consilium suum.
Nguvu za hatua zake zimedhoofishwa; shauri lake baya litamwangusha.
8 Immisit enim in rete pedes suos, et in maculis eius ambulat.
Miguu yake imemsukumia kwenye wavu, naye anatangatanga kwenye matundu ya wavu.
9 Tenebitur planta illius laqueo, et exardescet contra eum sitis.
Tanzi litamkamata kwenye kisigino; mtego utamshikilia kwa nguvu.
10 Abscondita est in terra pedica eius, et decipula illius super semitam.
Kitanzi kimefichwa ardhini kwa ajili yake; mtego uko kwenye njia yake.
11 Undique terrebunt eum formidines, et involvent pedes eius.
Vitisho vimemtia hofu kila upande, na adui zake humwandama kila hatua.
12 Attenuetur fame robur eius, et inedia invadat costas illius.
Janga linamwonea shauku; maafa yako tayari kwa ajili yake aangukapo.
13 Devoret pulchritudinem cutis eius, consumat brachia illius primogenita mors.
Nayo yatakula sehemu ya ngozi yake; mzaliwa wa kwanza wa mauti atakula maungo yake.
14 Avellatur de tabernaculo suo fiducia eius, et calcet super eum, quasi rex, interitus.
Atangʼolewa kutoka usalama wa hema lake, na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho.
15 Habitent in tabernaculo illius socii eius, qui non est, aspergatur in tabernaculo eius sulphur.
Moto utakaa katika hema lake; moto wa kiberiti utamwagwa juu ya makao yake.
16 Deorsum radices eius siccentur, sursum autem atteratur messis eius.
Mizizi yake chini itakauka na matawi yake juu yatanyauka.
17 Memoria illius pereat de terra, et non celebretur nomen eius in plateis.
Kumbukumbu lake litatoweka katika dunia, wala hatakuwa na jina katika nchi.
18 Expellet eum de luce in tenebras, et de orbe transferet eum.
Ameondolewa nuruni na kusukumiwa gizani, naye amefukuzwa mbali atoke duniani.
19 Non erit semen eius, neque progenies in populo suo, nec ullae reliquiae in regionibus eius.
Hana mtoto wala mzao miongoni mwa watu wake, wala aliyenusurika mahali alipoishi.
20 In die eius stupebunt novissimi, et primos invadet horror.
Watu wa magharibi watashangaa yaliyompata; watu wa mashariki watapatwa na hofu.
21 Haec sunt ergo tabernacula iniqui, et iste locus eius, qui ignorat Deum.
Hakika ndivyo yalivyo makao ya mtu mwovu; ndivyo palivyo mahali pake mtu asiyemjua Mungu.”