< 욥기 40 >

1 여호와께서 또 욥에게 말씀하여 가라사대
Bwana akamwambia Ayubu:
2 변박하는 자가 전능자와 다투겠느냐 하나님과 변론하는 자는 대답할지니라
“Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
3 욥이 여호와께 대답하여 가로되
Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
4 나는 미천하오니 무엇이라 주께 대답하리이까 손으로 내 입을 가릴 뿐이로소이다
“Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
5 내가 한두번 말하였사온즉 다시는 더하지도 아니하겠고 대답지도 아니하겠나이다
Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
6 여호와께서 푹풍 가운데서 욥에게 말씀하여 가라사대
Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
7 너는 대장부처럼 허리를 묶고 내가 네게 묻는 것을 대답할지니라
“Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
8 네가 내 심판을 폐하려느냐 스스로 의롭다 하려 하여 나를 불의 하다 하느냐
“Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
9 네가 하나님처럼 팔이 있느냐 하나님처럼 우렁차게 울리는 소리를 내겠느냐
Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
10 너는 위엄과 존귀로 스스로 꾸미며 영광과 화미를 스스로 입을지니라
Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
11 너의 넘치는 노를 쏟아서 교만한 자를 발견하여 낱낱이 낮추되
Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
12 곧 모든 교만한 자를 발견하여 낮추며 악인을 그 처소에서 밟아서
mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
13 그들을 함께 진토에 묻고 그 얼굴을 싸서 어둑한 곳에 둘지니라
Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
14 그리하면 네 오른손이 너를 구원할 수 있다고 내가 인정하리라
Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
15 이제 소 같이 풀을 먹는 하마를 볼지어다 내가 너를 지은 것같이 그것도 지었느니라
“Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
16 그 힘은 허리에 있고 그 세력은 배의 힘줄에 있고
Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
17 그 꼬리 치는 것은 백향목이 흔들리는 것같고 그 넓적다리 힘줄은 서로 연락되었으며
Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
18 그 뼈는 놋관 같고 그 가릿대는 철장 같으니
Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
19 그것은 하나님의 창조물 중에 으뜸이라 그것을 지은 자가 칼을 주었고
Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
20 모든 들 짐승의 노는 산은 그것을 위하여 식물을 내느니라
Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
21 그것이 연 줄기 아래나 갈 밭 가운데나 못속에 엎드리니
Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
22 연 그늘이 덮으며 시내 버들이 둘렀구나
Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
23 하수가 창일한다 할지라도 그것이 놀라지 않고 요단강이 불어 그입에 미칠지라도 자약하니
Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
24 그것이 정신 차리고 있을 때에 누가 능히 잡을 수 있겠으며 갈고리로 그 코를 꿸 수 있겠느냐
Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?

< 욥기 40 >