< 詩篇 66 >
Mpigieni Mungu kelele za shangwe, nchi yote;
Imbeni utukufu wa jina lake; mzitukuze sifa zake.
3 かみに告まつれ 汝のもろもろの功用はおそるべきかな大なる力によりてなんぢの仇はなんぢに畏れしたがひ
Mwambieni Mugu, “Matendo yako yanatisha kama nini! Kwa ukuu wa nguvu zako maadui zako watajisalimisha kwako.
4 全地はなんぢを拝みてうたひ名をほめうたはんと (セラ)
Nchi yote watakuabudu wewe na watakuimbia wewe; wataliimbia jina lako.” (Selah)
5 來りて神のみわざをみよ 人の子輩にむかひて作たまふことはおそるべきかな
Njoni na mtazame kazi za Mungu; yeye anatisha katika matendo yake awatendeayo wanadamu.
6 神はうみをかへて乾ける地となしたまへり ひとびと歩行にて河をわたりき その處にてわれらは神をよろこべり
Aligeuza bahari kuwa nchi kavu; wao walitembea kwa mguu juu ya mto; huko tulishangilia katika yeye.
7 神はその大能をもてとこしへに統治め その目は諸國をみたまふ そむく者みづからを崇むべからず (セラ)
Yeye anatawala milele kwa nguvu zake; macho yake yanachunguza mataifa; waasi wasijivune. (Selah)
8 もろもろの民よ われらの神をほめまつれ神をほめたたふる聲をきこえしめよ
Mtukuzeni Mungu, enyi watu wa mataifa yote, sauti ya sifa zake isikike.
9 神はわれらの霊魂をながらへしめ われらの足のうごかさるることをゆるしたまはず
Yeye atuwekaye hai, naye hairuhusu miguu yetu iteleze.
10 神よなんぢはわれらを試みて白銀をねるごとくにわれらを錬たまひたればなり
Kwa maana wewe, Mungu, umetupima sisi, wewe umetupima kama inavyopimwa fedha.
11 汝われらを網にひきいれ われらの腰におもき荷をおき
Wewe ulituingiza sisi kwenye wavu; uliweka mzigo mzito viunoni mwetu.
12 人々をわれらの首のうへに騎こえしめたまひき われらは火のなか水のなかをすぎゆけり されど汝その中よりわれらをひきいたし豊盛なる處にいたらしめたまへり
Wewe uliwafanya watu wasafiri juu ya vichwa vyetu; tulipita motoni na majini, lakini ukatuleta mahali pa wazi palipo salama.
13 われ燔祭をもてなんぢの家にゆかん 迫りくるしみたるときにわが口唇のいひいでわが口ののべし誓をなんぢに償はん
Nitaingia nyumbani mwako nikiwa na sadaka ya kuteketezwa; nitakulipa viapo vyangu
14 われ燔祭をもてなんぢの家にゆかん 迫りくるしみたるときにわが口唇のいひいでわが口ののべし誓をなんぢに償はん
ambavyo midomo yangu iliahidi na kinywa changu kiliongea nilipokuwa katika dhiki.
15 われ肥たるものを燔祭とし牡羊を馨香として汝にささげ牡牛と牡山羊とをそなへまつらん (セラ)
Nitakutolea sadaka ya kuteketezwa ya wanyama wanene pamoja na harufu nzuri ya kondoo waume; Nitatoa ng'ombe na mbuzi. (Selah)
16 神をおそるる人よ みな來りてきけ われ神のわがたましひのために作たまへることをのべん
Njoni, msikie, ninyi nyote mnao mwabudu Mungu, nami nitatangaza yale yeye aliyoitendea roho yangu.
17 われわが口をもて神によばはり また舌をもてあがむ
Nilimlilia kwa kinywa changu, naye alipendezwa na ulimi wangu.
18 然るにわが心にしれる不義あらば主はわれにききたまふまじ
Kama ningelikuwa na dhambi ndani ya moyo wangu, Bwana asingenisikiliza.
19 されどまことに神はききたまへり聖意をわがいのりの聲にとめたまへり
Lakini Mungu hakika amesikia; amesikia sautiya kuomba kwangu.
20 神はほむべきかな わが祈をしりぞけず その憐憫をわれよりとりのぞきたまはざりき
Atukuzwe Mungu, ambaye hakuyakataa maombi yangu wala kuweka uaminifu wa agano lake mbali nami.