< Proverbi 16 >

1 Le disposizioni dell'animo [son] dell'uomo; Ma la risposta della lingua [è] dal Signore.
Mipango ya moyo ni ya mtu, bali Yehova hutoa jawabu kutoka kwenye ulimi wake.
2 Tutte le vie dell'uomo gli paiono pure; Ma il Signore pesa gli spiriti.
Njia zote za mtu ni safi kwenye macho yake mwenyewe, bali Yehova huipima mioyo.
3 Rimetti le tue opere nel Signore, E i tuoi pensieri saranno stabiliti.
Kabidhi kwa Yehova kazi zako zote na mipango yako itafanikiwa.
4 Il Signore ha fatto ogni cosa per sè stesso; Eziandio l'empio per lo giorno del male.
Yehova alifanya kila kitu kwa kusudi lake, hata waovu kwa ajili ya siku ya taabu.
5 Chiunque è altiero d'animo [è] abbominevole al Signore; D'ora in ora egli non resterà impunito.
Yehova anamchukia kila mtu mwenye moyo wa majivuno, ingawa wanasimama imara, hawakosi kupata adhabu.
6 L'iniquità sarà purgata con benignità, e [con] verità; E per lo timor del Signore l'uomo si ritrae dal male.
Kwa agano la uaminifu na udhamini uovu husafishwa na kwa kumcha Yehova watu hujitenga na ubaya.
7 Quando il Signore gradisce le vie dell'uomo, Pacifica con lui eziandio i suoi nemici.
Njia za mtu zinapompendeza Yehova, huwafanya hata adui zake huyo mtu wawe na amani naye.
8 Meglio [vale] poco con giustizia, Che grandi entrate senza dirittura.
Bora kitu kidogo pamoja na haki, kuliko mapato makubwa pamoja na udhalimu.
9 Il cuor dell'uomo delibera della sua via; Ma il Signore dirizza i suoi passi.
Katika moyo wake mtu hunuia njia yake, bali Yehova huziongoza hatua zake.
10 Indovinamento [è] nelle labbra del re; La sua bocca non falla nel giudicio.
Mshauri yupo katika midimo ya mfalme, katika hukumu kinywa chake hakisemi kwa udanganyifu.
11 La stadera, e le bilance giuste [son] del Signore; Tutti i pesi del sacchetto [son] sua opera.
Vipimo vya kweli hutoka kwa Yehova; uzito wote kwenye gunia ni kazi yake.
12 Operare empiamente [è] abbominevole ai re; Perciocchè il trono sarà stabilito per giustizia.
Wafalme wanapofanya mambo maovu, hicho ni kitu cha kudharauliwa, kwa maana utawala huimarishwa kwa kutenda haki.
13 Le labbra giuste [son] quelle che i re gradiscono; Ed essi amano chi parla dirittamente.
Mfalme hufurahia midomo ambayo husema haki na anampenda mwenye kusema waziwazi.
14 L'ira del re [son] messi di morte; Ma l'uomo savio la placherà.
Hasira ya mfalme ni mjumbe wa mauti lakini mtu mwenye busara atajaribu kutuliza hasira yake.
15 Nella chiarezza della faccia del re [vi è] vita; E la sua benevolenza [è] come la nuvola della pioggia della stagione della ricolta.
Katika nuru ya uso wa mfalme ni uzima na fadhila yake ni kama wingu linaloleta mvua ya masika.
16 Quant'[è] egli cosa migliore acquistar sapienza che oro! E [quant'è] egli cosa più eccellente acquistar prudenza che argento!
Ni bora kiasi gani kupata hekima kuliko dhahabu. Kuchagua kupata ufahamu ni zaidi kuliko fedha.
17 La strada degli [uomini] diritti [è] di stornarsi dal male; Chi osserva la sua via guarda l'anima sua.
Njia kuu ya watu waadilifu hujitenga na ubaya; mwenye kuyahifadhi maisha yake huilinda njia yake.
18 La superbia [viene] davanti alla ruina, E l'alterezza dello spirito davanti alla caduta.
Kiburi hutangulia kabla ya uharibifu na moyo wa kujivuna kabla ya maangamizi.
19 Meglio [è] essere umile di spirito co' mansueti, Che spartir le spoglie con gli altieri.
Ni bora kunyenyekea miongoni mwa watu masikini kuliko kugawana ngawira pamoja watu wenye kiburi.
20 Chi è intendente nella parola troverà bene; E beato chi si confida nel Signore.
Mwenye kutafakari yaliyofundishwa hupata kilicho chema na wenye kumtumaini Yehova watafurahi.
21 Il savio di cuore sarà chiamato intendente; E la dolcezza delle labbra aggiugnerà dottrina.
Mwenye hekima moyoni anaitwa ufuhamu na utamu wa hotuba huongeza uwezo wa kufundisha.
22 Il senno [è] una fonte di vita in coloro che ne son dotati; Ma l'ammaestramento degli stolti [è] stoltizia.
Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwake ambaye nayo, bali adhabu ya wapumbavu ni upumbavu wao.
23 Il cuor del[l'uomo] savio rende avveduta la sua bocca, E aggiunge dottrina alle sue labbra.
Moyo wa mtu mwenye hekima hutoa busara katika kinywa chake na huongeza ushawishi katika midomo yake.
24 I detti soavi [sono] un favo di miele, Dolcezza all'anima, e medicina alle ossa.
Maneno yenye kufaa ni sega la asali -matamu kwenye nafsi na huponya mifupa.
25 Vi è tal via che pare diritta all'uomo, Il fine della quale [son] le vie della morte.
Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, bali mwisho wake ni njia ya mauti.
26 L'anima di chi si affatica si affatica per lui stesso; Perciocchè la sua bocca lo preme.
Hamu ya kibarua humfanyia kazi; njaa yake humsihi kuendelea.
27 L'uomo scellerato apparecchia del male; E in su le sue labbra [vi è] come un fuoco ardente.
Mtu duni huchimba madhara na usemi wake ni kama moto unaounguza.
28 L'uomo perverso commette contese; E chi va sparlando disunisce gli amici.
Mtu mkaidi huchochea mafarakano na umbeya huwafarakanisha marafiki.
29 L'uomo violento seduce il suo compagno, E lo conduce per una via [che] non [è] buona.
Mtu wa vurugu humdanganya jirani yake na kumwongoza kwenye mapito ambayo si mema.
30 Chi chiude gli occhi macchinando perversità, Dimena le labbra [quando] ha compiuto il male.
Yule anayekonyeza kwa jicho anapanga njama za mambo ya ukaidi; wenye kuandama midomo yao watapitisha mabaya.
31 La canutezza [è] una corona gloriosa; Ella si troverà nella via della giustizia.
Mvi ni taji ya utukufu; hupatikana kwa kuishi katika njia ya haki.
32 Meglio vale chi è lento all'ira, che il forte; E [meglio vale] chi signoreggia il suo cruccio, che un prenditor di città.
Ni bora kukawia kuwa na hasira kuliko kuwa shujaa na mwenye kutawala roho yake ni imara zaidi kuliko yule anayeuteka mji.
33 La sorte è gittata nel grembo; Ma dal Signore [procede] tutto il giudicio di essa.
Kura hurushwa kwenye mkunjo, bali maamuzi hutoka kwa Yehova.

< Proverbi 16 >