< Salmi 109 >

1 Dio della mia lode, non tacere, Al maestro del coro. Di Davide. Salmo.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, ambaye ninakusifu, usiwe kimya,
2 poiché contro di me si sono aperte la bocca dell'empio e dell'uomo di frode; parlano di me con lingua di menzogna.
kwa maana watu waovu na wadanganyifu wamefungua vinywa vyao dhidi yangu; wasema dhidi yangu kwa ndimi za udanganyifu.
3 Mi investono con parole di odio, mi combattono senza motivo.
Wamenizunguka kwa maneno ya chuki, wananishambulia bila sababu.
4 In cambio del mio amore mi muovono accuse, mentre io sono in preghiera.
Wanachonilipa badala ya urafiki wangu ni kunishtaki, lakini mimi ninawaombea.
5 Mi rendono male per bene e odio in cambio di amore.
Wananilipiza mabaya kwa mema, chuki badala ya urafiki wangu.
6 Suscita un empio contro di lui e un accusatore stia alla sua destra.
Agiza mtu mwovu ampinge, mshtaki asimame mkono wake wa kuume.
7 Citato in giudizio, risulti colpevole e il suo appello si risolva in condanna.
Anapohukumiwa, apatikane na hatia, nayo maombi yake yamhukumu.
8 Pochi siano i suoi giorni e il suo posto l'occupi un altro.
Siku zake za kuishi na ziwe chache, nafasi yake ya uongozi ichukuliwe na mtu mwingine.
9 I suoi figli rimangano orfani e vedova sua moglie.
Watoto wake na waachwe yatima, mke wake na awe mjane.
10 Vadano raminghi i suoi figli, mendicando, siano espulsi dalle loro case in rovina.
Watoto wake na watangetange wakiomba, na wafukuzwe kwenye magofu ya nyumba zao.
11 L'usuraio divori tutti i suoi averi e gli estranei faccian preda del suo lavoro.
Mtu anayemdai na ateke vyote alivyo navyo, matunda ya kazi yake yatekwe nyara na wageni.
12 Nessuno gli usi misericordia, nessuno abbia pietà dei suoi orfani.
Asiwepo mtu yeyote wa kumtendea mema wala wa kuwahurumia yatima wake.
13 La sua discendenza sia votata allo sterminio, nella generazione che segue sia cancellato il suo nome.
Uzao wake na ukatiliwe mbali, majina yao yafutike katika kizazi kifuatacho.
14 L'iniquità dei suoi padri sia ricordata al Signore, il peccato di sua madre non sia mai cancellato.
Maovu ya baba zake na yakumbukwe mbele za Bwana, dhambi ya mama yake isifutwe kamwe.
15 Siano davanti al Signore sempre ed egli disperda dalla terra il loro ricordo.
Dhambi zao na zibaki daima mbele za Bwana, ili apate kukatilia mbali kumbukumbu lao duniani.
16 Perché ha rifiutato di usare misericordia e ha perseguitato il misero e l'indigente, per far morire chi è affranto di cuore.
Kwa maana kamwe hakuweza kutenda wema, bali alimfukuza mnyonge na mhitaji, aliwafanyia jeuri wahitaji na waliovunjika moyo.
17 Ha amato la maledizione: ricada su di lui! Non ha voluto la benedizione: da lui si allontani!
Alipenda kulaani, nayo laana ikampata; hakupenda kubariki, kwa hiyo baraka na ikae mbali naye.
18 Si è avvolto di maledizione come di un mantello: è penetrata come acqua nel suo intimo e come olio nelle sue ossa.
Alivaa kulaani kama vazi lake, nayo laana ikamwingia mwilini mwake kama maji, kwenye mifupa yake kama mafuta.
19 Sia per lui come vestito che lo avvolge, come cintura che sempre lo cinge.
Na iwe kama joho alilozungushiwa, kama mshipi aliofungiwa daima.
20 Sia questa da parte del Signore la ricompensa per chi mi accusa, per chi dice male contro la mia vita.
Haya na yawe malipo ya Bwana kwa washtaki wangu, kwa wale wanaoninenea mabaya.
21 Ma tu, Signore Dio, agisci con me secondo il tuo nome: salvami, perché buona è la tua grazia.
Lakini wewe, Ee Bwana Mwenyezi, unitendee wema kwa ajili ya jina lako, uniokoe kwa wema wa pendo lako.
22 Io sono povero e infelice e il mio cuore è ferito nell'intimo.
Maana mimi ni maskini na mhitaji, moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
23 Scompaio come l'ombra che declina, sono sbattuto come una locusta.
Ninafifia kama kivuli cha jioni, nimerushwa-rushwa kama nzige.
24 Le mie ginocchia vacillano per il digiuno, il mio corpo è scarno e deperisce.
Magoti yangu yamelegea kwa kufunga, mwili wangu umedhoofika na kukonda.
25 Sono diventato loro oggetto di scherno, quando mi vedono scuotono il capo.
Nimekuwa kitu cha kudharauliwa kwa washtaki wangu, wanionapo, hutikisa vichwa vyao.
26 Aiutami, Signore mio Dio, salvami per il tuo amore.
Ee Bwana, Mungu wangu nisaidie, niokoe sawasawa na upendo wako.
27 Sappiano che qui c'è la tua mano: tu, Signore, tu hai fatto questo.
Watu na wafahamu kuwa ni mkono wako, kwamba wewe, Ee Bwana, umetenda hili.
28 Maledicano essi, ma tu benedicimi; insorgano quelli e arrossiscano, ma il tuo servo sia nella gioia.
Wanaweza kulaani, lakini wewe utabariki, watakaposhambulia wataaibishwa, lakini mtumishi wako atashangilia.
29 Sia coperto di infamia chi mi accusa e sia avvolto di vergogna come d'un mantello.
Washtaki wangu watavikwa fedheha, na kufunikwa na aibu kama joho.
30 Alta risuoni sulle mie labbra la lode del Signore, lo esalterò in una grande assemblea;
Kwa kinywa changu nitamtukuza sana Bwana, katika umati mkubwa nitamsifu.
31 poiché si è messo alla destra del povero per salvare dai giudici la sua vita.
Kwa maana husimama mkono wa kuume wa mhitaji, kuokoa maisha yake kutoka kwa wale wanaomhukumu.

< Salmi 109 >