< Salmi 108 >

1 Canto. Salmo. Di Davide. Saldo è il mio cuore, Dio, saldo è il mio cuore: voglio cantare inni, anima mia.
Wimbo. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
2 Svegliatevi, arpa e cetra, voglio svegliare l'aurora.
Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
3 Ti loderò tra i popoli, Signore, a te canterò inni tra le genti,
Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
4 perché la tua bontà è grande fino ai cieli e la tua verità fino alle nubi.
Kwa maana upendo wako ni mkuu, ni juu kuliko mbingu; uaminifu wako unazifikia anga.
5 Innàlzati, Dio, sopra i cieli, su tutta la terra la tua gloria.
Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
6 Perché siano liberati i tuoi amici,
Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume, ili wale uwapendao wapate kuokolewa.
7 Dio ha parlato nel suo santuario: «Esulterò, voglio dividere Sichem e misurare la valle di Succot;
Mungu amenena kutoka patakatifu pake: “Nitaigawa Shekemu kwa ushindi na kulipima Bonde la Sukothi.
8 mio è Gàlaad, mio Manasse, Efraim è l'elmo del mio capo, Giuda il mio scettro.
Gileadi ni yangu, Manase ni yangu, Efraimu ni kofia yangu ya chuma, nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.
9 Moab è il catino per lavarmi, sull'Idumea getterò i miei sandali, sulla Filistea canterò vittoria».
Moabu ni sinia langu la kunawia, juu ya Edomu natupa kiatu changu; nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”
10 Chi mi guiderà alla città fortificata, chi mi condurrà fino all'Idumea?
Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome? Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?
11 Non forse tu, Dio, che ci hai respinti e più non esci, Dio, con i nostri eserciti?
Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi, na hutoki tena na majeshi yetu?
12 Contro il nemico portaci soccorso, poiché vana è la salvezza dell'uomo.
Tuletee msaada dhidi ya adui, kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.
13 Con Dio noi faremo cose grandi ed egli annienterà chi ci opprime.
Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi, naye atawaponda adui zetu.

< Salmi 108 >