< מִשְׁלֵי 27 >
אל תתהלל ביום מחר כי לא תדע מה ילד יום׃ | 1 |
Usijisifu kwa ajili ya kesho, kwa kuwa hujui ni nini kitakachozaliwa kwa siku moja.
יהללך זר ולא פיך נכרי ואל שפתיך׃ | 2 |
Mwache mwingine akusifu, wala si kinywa chako mwenyewe; mtu mwingine afanye hivyo na si midomo yako mwenyewe.
כבד אבן ונטל החול וכעס אויל כבד משניהם׃ | 3 |
Jiwe ni zito na mchanga ni mzigo, lakini kukasirishwa na mpumbavu ni kuzito kuliko vyote viwili.
אכזריות חמה ושטף אף ומי יעמד לפני קנאה׃ | 4 |
Hasira ni ukatili na ghadhabu kali ni gharika, lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu?
טובה תוכחת מגלה מאהבה מסתרת׃ | 5 |
Afadhali karipio la wazi kuliko upendo uliofichika.
נאמנים פצעי אוהב ונעתרות נשיקות שונא׃ | 6 |
Majeraha kutoka kwa rafiki yaonyesha uaminifu, bali kubusu kwa adui ni kwingi sana.
נפש שבעה תבוס נפת ונפש רעבה כל מר מתוק׃ | 7 |
Yeye aliyeshiba huchukia kabisa asali, bali kwa mwenye njaa hata kile kilicho kichungu kwake ni kitamu.
כצפור נודדת מן קנה כן איש נודד ממקומו׃ | 8 |
Kama ndege atangatangavyo mbali na kiota chake, ndivyo alivyo mtu atangatangaye mbali na nyumbani mwake.
שמן וקטרת ישמח לב ומתק רעהו מעצת נפש׃ | 9 |
Manukato na uvumba huleta furaha moyoni, nao uzuri wa rafiki huchipuka kutoka kwenye ushauri wake wa uaminifu.
רעך ורעה אביך אל תעזב ובית אחיך אל תבוא ביום אידך טוב שכן קרוב מאח רחוק׃ | 10 |
Usimwache rafiki yako wala rafiki wa baba yako, tena usiende nyumbani mwa ndugu yako wakati umepatwa na maafa. Bora jirani wa karibu kuliko ndugu aliye mbali.
חכם בני ושמח לבי ואשיבה חרפי דבר׃ | 11 |
Mwanangu, uwe na hekima, nawe ulete furaha moyoni mwangu, ndipo nitakapoweza kumjibu yeyote anitendaye kwa dharau.
ערום ראה רעה נסתר פתאים עברו נענשו׃ | 12 |
Mtu mwenye busara huona hatari na kujificha, bali mjinga huendelea mbele nayo ikamtesa.
קח בגדו כי ערב זר ובעד נכריה חבלהו׃ | 13 |
Chukua vazi la yule awekaye dhamana kwa ajili ya mgeni; lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
מברך רעהו בקול גדול בבקר השכים קללה תחשב לו׃ | 14 |
Kama mtu akimbariki jirani yake kwa sauti kuu asubuhi na mapema, itahesabiwa kama ni laana.
דלף טורד ביום סגריר ואשת מדונים נשתוה׃ | 15 |
Mke mgomvi ni kama matone yasiyokoma ya siku ya mvua.
צפניה צפן רוח ושמן ימינו יקרא׃ | 16 |
Kumzuia yeye ni kama kuuzuia upepo au kukamata mafuta kwa kiganja cha mkono.
ברזל בברזל יחד ואיש יחד פני רעהו׃ | 17 |
Kama vile chuma kinoavyo chuma, ndivyo mtu amnoavyo mwenzake.
נצר תאנה יאכל פריה ושמר אדניו יכבד׃ | 18 |
Yeye autunzaye mtini atakula tunda lake, naye amtunzaye bwana wake ataheshimiwa.
כמים הפנים לפנים כן לב האדם לאדם׃ | 19 |
Kama uso uonekanavyo kwenye maji, ndivyo hivyo moyo wa mtu humwonyesha alivyo.
שאול ואבדה לא תשבענה ועיני האדם לא תשבענה׃ (Sheol ) | 20 |
Kuzimu na Uharibifu havishibi kadhalika macho ya mwanadamu. (Sheol )
מצרף לכסף וכור לזהב ואיש לפי מהללו׃ | 21 |
Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru kwa ajili ya dhahabu, bali mtu hupimwa kwa sifa azipokeazo.
אם תכתוש את האויל במכתש בתוך הריפות בעלי לא תסור מעליו אולתו׃ | 22 |
Hata ukimtwanga mpumbavu kwenye kinu, ukimtwanga kama nafaka kwa mchi, hutauondoa upumbavu wake.
ידע תדע פני צאנך שית לבך לעדרים׃ | 23 |
Hakikisha kuwa unajua hali ya makundi yako ya kondoo na mbuzi, angalia kwa bidii ngʼombe zako.
כי לא לעולם חסן ואם נזר לדור דור׃ | 24 |
Kwa kuwa utajiri haudumu milele, nayo taji haidumu vizazi vyote.
גלה חציר ונראה דשא ונאספו עשבות הרים׃ | 25 |
Wakati majani makavu yameondolewa na mapya yamechipua, nayo majani toka milimani yamekusanywa,
כבשים ללבושך ומחיר שדה עתודים׃ | 26 |
wana-kondoo watakupatia mavazi na mbuzi thamani ya shamba.
ודי חלב עזים ללחמך ללחם ביתך וחיים לנערותיך׃ | 27 |
Utakuwa na maziwa mengi ya mbuzi kukulisha wewe na jamaa yako, na kuwalisha watumishi wako wa kike.