< תהילים 77 >

למנצח על-ידיתון (ידותון) לאסף מזמור ב קולי אל-אלהים ואצעקה קולי אל-אלהים והאזין אלי 1
Nitampazia Mungu sauti yangu, nitamuita Mungu kwa sauti yangu, na Mungu wangu atanisikia.
ביום צרתי אדני דרשתי ידי לילה נגרה--ולא תפוג מאנה הנחם נפשי 2
Katika siku ya taabu nilimtafuta Bwana; usiku niliinua mikono yangu, nayo haikuchoka. Moyo wangu ulikataa kufarijiwa.
אזכרה אלהים ואהמיה אשיחה ותתעטף רוחי סלה 3
Ningali nikiugua nilielekeza mawazo yangu kwa Mungu. Nilimfikiria Mungu nilipokuwa dhaifu. (Selah)
אחזת שמרות עיני נפעמתי ולא אדבר 4
Uliyafanya macho yangu yasisinzie; nilisumbuka sana kuongea.
חשבתי ימים מקדם-- שנות עולמים 5
Nilifikiri kuhusu siku za kale, kuhusu mambo yaliyopita muda mrefu.
אזכרה נגינתי בלילה עם-לבבי אשיחה ויחפש רוחי 6
Wakati wa usiku niliukumbuka wimbo niliouimba mara moja. Nilifikiria kwa makini na kujaribu kuelewa kile kilichokuwa kimetokea.
הלעולמים יזנח אדני ולא-יסיף לרצות עוד 7
Je, Mungu atanikataa milele? Je, hatanionesha tena huruma?
האפס לנצח חסדו גמר אמר לדר ודר 8
Je, uaminifu wa agano lake ulikuwa umetoweka milele? Je, ahadi yake imeshindwa milele?
השכח חנות אל אם-קפץ באף רחמיו סלה 9
Je, Mungu amesahau kuwa mwenye neema? Je, hasira yake imeifunga huruma yake? (Selah)
ואמר חלותי היא-- שנות ימין עליון 10
Nilisema, “Hii ni huzuni yangu: mabadiliko ya mkono wa kuume wa Aliye Juu dhidi yetu.”
אזכיר (אזכור) מעללי-יה כי-אזכרה מקדם פלאך 11
Lakini nitayakumbuka matendo yako, Yahwe; nitafikiri kuhusu matendo yako makuu yaliyopita.
והגיתי בכל-פעלך ובעלילותיך אשיחה 12
Nitayatafakari matendo yako yote nami nitayaishi.
אלהים בקדש דרכך מי-אל גדול כאלהים 13
Njia yako, Mungu, ni takatifu; ni mungu gani wa kulinganishwa na Mungu wetu aliye mkuu?
אתה האל עשה פלא הודעת בעמים עזך 14
Wewe ni Mungu utendaye maajabu; wewe umeonesha nguvu zako kati ya mataifa.
גאלת בזרוע עמך בני-יעקב ויוסף סלה 15
Uliwapa watu wako ushindi kwa uweza wako mkuu - ukoo wa Yakobo na Yusufu. (Selah)
ראוך מים אלהים--ראוך מים יחילו אף ירגזו תהמות 16
Maji yalikuona wewe, Mungu; maji yalikuona wewe, nayo yakaogopa; vina vya maji vilitetemeka.
זרמו מים עבות--קול נתנו שחקים אף-חצציך יתהלכו 17
Mawingu yalitiririsha maji chini; anga zito lilitoa sauti; mishale yako ilipita kati.
קול רעמך בגלגל--האירו ברקים תבל רגזה ותרעש הארץ 18
Sauti yako kama ya radi ilisikika katika upepo; radi iliwasha dunia; nchi iliogopa na kutetemeka.
בים דרכך--ושביליך (ושבילך) במים רבים ועקבותיך לא נדעו 19
Njia yako ilipita baharini na mapito yako katika maji mengi, lakini alama za miguu yako hazikuonekana.
נחית כצאן עמך-- ביד-משה ואהרן 20
Uliwaongoza watu wako kama kundi kwa mkono wa Musa na Haruni.

< תהילים 77 >