< תהילים 76 >
למנצח בנגינת מזמור לאסף שיר ב נודע ביהודה אלהים בישראל גדול שמו | 1 |
Mungu amefanya mwenyewe kujulikana katika Yuda; jina lake ni kuu katika Israeli.
ויהי בשלם סוכו ומעונתו בציון | 2 |
Hema yake iko salemu; makao yake yako yako Sayuni.
שמה שבר רשפי-קשת מגן וחרב ומלחמה סלה | 3 |
Huko ndiko alivunja mishale ya upinde, ngao, upanga, na silaha zingine za vita. (Selah)
נאור אתה אדיר-- מהררי-טרף | 4 |
Wewe unang'aa sana na huufunua utukufu wako, ushukapo kutoka milimani, ambako uliwauwa mateka.
אשתוללו אבירי לב-- נמו שנתם ולא-מצאו כל-אנשי-חיל ידיהם | 5 |
Wenye moyo shujaa walitekwa nyara; walilala mauti. Mashujaa wote walikuwa wanyonge.
מגערתך אלהי יעקב נרדם ורכב וסוס | 6 |
Kwa kukemea kwako, ewe Mungu wa Yakobo, wote gari na farasi walilala mauti.
אתה נורא אתה--ומי-יעמד לפניך מאז אפך | 7 |
Wewe, ndiyo wewe, ni wa kuogopwa; ni nani awezaye kusimama mbele yako wakati ukiwa na hasira?
משמים השמעת דין ארץ יראה ושקטה | 8 |
Kutoka mbinguni wewe uliifanya hukumu yako isikike; nchi iliogopa na ikaa kimya
בקום-למשפט אלהים-- להושיע כל-ענוי-ארץ סלה | 9 |
wakati wewe, Mungu, ulipoinuka kutekeleza hukumu na kuwaokoa wote wa nchi walio onewa. (Selah)
כי-חמת אדם תודך שארית חמת תחגר | 10 |
Hakika hukumu ya hasira yako dhidi ya binadamu itakuletea wewe sifa; wewe hujifunga mwenyewe hasira yako iliyo baki.
נדרו ושלמו ליהוה אלהיכם כל-סביביו--יבילו שי למורא | 11 |
Wekeni nadhiri kwa Yahwe Mungu wenu na kuzihifadhi. Nao wote wamzungukao yeye mleteeni zawadi yeye ambaye ni wa kuogopwa.
יבצר רוח נגידים נורא למלכי-ארץ | 12 |
Yeye huzikata roho za wakuu; huogopwa na wafalme wa nchi.