< Psalm 115 >
1 Nicht uns, nicht uns, nein, Deinem Namen gib die Ehre, Herr, und Deiner Huld und Deiner Treue!
Sio kwetu, Yahwe, sio kwetu, bali kwa jina lako ulete heshima, kwa ajili ya uaminifu wa agano lako na uaminifu wako.
2 Was sollten schon die Heiden sagen: "Wo ist ihr Gott?"
Kwa nini mataifa yalazimike kusema, “Yuko wapi Mungu wako?”
3 Im Himmel ist er, unser Gott, der alles, was er will, vollbringt. -
Mungu wetu aliye mbinguni; hufanya chochote apendacho.
4 Doch ihre Götzen sind von Gold und Silber, ein Werk von Menschenhänden.
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
5 Sie haben einen Mund und reden nicht; Sie haben Augen, doch sie sehen nicht.
Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
6 Nicht hören sie mit ihren Ohren; nicht riechen sie mit ihrer Nase.
zina masikio, lakini hazisikii; zina pua lakini hazinusi.
7 Nicht tasten sie mit ihren Händen; nicht gehen sie mit ihren Füßen; sie bringen keinen Laut aus ihrer Kehle.
Sanamu hizo zina mikono, lakini hazishiki; zina miguu, lakini haziwezi kutembea; wala haziongei kutoka viywani mwao.
8 Wie sie, so werden ihre Schöpfer und alle, die auf sie vertrauen. -
Wale wanao zitengeneza wanafanana nazo, vile vile yeyote anaye amini katika hizo.
9 Hat aber Israel fest auf den Herrn gebaut, dann ist er ihm ein Schutz und Schild.
Israeli, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
10 Baut Aarons Haus fest auf den Herrn, dann ist er ihnen Schutz und Schild.
Nyumba ya Haruni, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
11 Und bauen, die den Herren fürchten, auf den Herrn, dann ist er ihnen Schutz und Schild.
Ninyi mnao mheshumu Yahwe, mwamini yeye; yeye ni msaada wenu na ngao yenu.
12 So segne unsern Fortbestand der Herr! Er segne das Haus Israel! Er segne Aarons Haus!
Yahwe hutukumbuka sisi na atatubariki; ataibariki familia ya Israeli; atabariki familia ya Haruni.
13 Er segne, die den Herren fürchten, die Kleinen mit den Großen!
Atawabariki wale wanao muheshimu yeye, wote vijana na wazee.
14 Der Herr vermehre euch, euch selbst und eure Kinder!
Yahwe na awaongeze ninyi zaidi na zaidi, ninyi pamoja na watoto wenu.
15 So seid gesegnet von dem Herrn, dem Schöpfer Himmels und der Erde! -
Yahwe na awabariki, aliyeziumba mbingu na nchi.
16 Der Himmel ist ein Himmel für den Herrn; die Erde nur gibt er den Menschenkindern.
Mbingu ni za Yahwe; lakini nchi amewapa wanadamu.
17 Die Toten loben nicht den Herrn, nicht die ins stille Reich Gesunkenen.
Wafu hawamsifu Yahwe, wala wote washukao chini kwenye ukimya;
18 Dagegen wollen wir den Herrn lobpreisen von nun an bis in Ewigkeit. Alleluja!
bali tutamtukuza Yahwe sasa na hata milele. Msifuni Yahwe.