< Matthieu 14 >

1 En ce temps-là Hérode, le tétrarque, apprit la renommée de Jésus;
Wakati huo, Mfalme Herode, mtawala wa Galilaya, alisikia habari za Yesu,
2 Et il dit à ses serviteurs: C’est Jean-Baptiste, c’est lui-même qui est ressuscité des morts, et voilà pourquoi des miracles s’opèrent par lui:
akawaambia watumishi wake, “Huyu ni Yohana Mbatizaji; amefufuka kutoka kwa wafu! Hii ndiyo sababu nguvu za kutenda miujiza zinafanya kazi ndani yake.”
3 Car Hérode s’était saisi de Jean, l’avait chargé de fers et jeté en prison, à cause d’Hérodiade, femme de Philippe son frère.
Herode alikuwa amemkamata Yohana, akamfunga na kumweka gerezani kwa sababu ya Herodia, mke wa Filipo, ndugu yake,
4 Car Jean lui disait: Il ne t’est pas permis de l’avoir.
kwa kuwa Yohana alikuwa amemwambia Herode: “Si halali kwako kuwa na huyo mwanamke.”
5 Et voulant le faire mourir, il craignit le peuple qui le tenait pour prophète.
Herode alitaka sana kumuua Yohana, lakini akaogopa watu, kwa maana walimtambua kuwa ni nabii.
6 Or, au jour de la naissance d’Hérode, la fille d’Hérodiade dansa au milieu de sa cour, et plut à Hérode.
Katika siku ya kuadhimisha sikukuu ya kuzaliwa kwa Herode, binti wa Herodia alicheza mbele ya watu waliohudhuria, akamfurahisha sana Herode,
7 D’où il lui promit, avec serment, de lui donner tout ce qu’elle lui demanderait.
kiasi kwamba aliahidi kwa kiapo kumpa huyo binti chochote angeomba.
8 Mais elle, instruite à l’avance par sa mère: Donnez-moi, dit-elle, ici dans un bassin, la tête de Jean-Baptiste.
Huyo binti, akiwa amechochewa na mama yake, akasema, “Nipe kichwa cha Yohana Mbatizaji kwenye sinia.”
9 Et le roi fut contristé; cependant à cause du serment et de ceux qui étaient à table avec lui, il commanda qu’on la lui donnât.
Mfalme akasikitika, lakini kwa sababu ya viapo alivyoapa mbele ya wageni, akaamuru kwamba apatiwe ombi lake.
10 Et il envoya décapiter Jean dans la prison.
Hivyo akaagiza Yohana Mbatizaji akatwe kichwa mle gerezani.
11 Et sa tête fut apportée dans un bassin, et donnée à la jeune fille, qui la porta à sa mère.
Kichwa chake kikaletwa kwenye sinia, akapewa yule binti, naye akampelekea mama yake.
12 Or ses disciples étant venus prirent son corps et l’ensevelirent; puis ils vinrent l’annoncer à Jésus.
Wanafunzi wa Yohana wakaja na kuuchukua mwili wake kwenda kuuzika. Kisha wakaenda wakamwambia Yesu.
13 Ce que Jésus ayant entendu, il partit de là dans une barque, pour se retirer à l’écart en un lieu désert; mais le peuple l’ayant su, le suivit à pied, des villes.
Yesu aliposikia yaliyokuwa yametukia, aliondoka kwa chombo akaenda mahali pasipo na watu ili awe peke yake. Lakini watu walipopata habari, wakamfuata kwa miguu kupitia nchi kavu kutoka miji.
14 Et, comme il sortait de la barque, il vit une grande foule; il eut pitié d’eux, et il guérit leurs malades.
Yesu alipofika kando ya bahari, aliona makutano makubwa ya watu, akawahurumia na akawaponya wagonjwa wao.
15 Or le soir étant venu, ses disciples s’approchèrent de lui, disant: Ce lieu est désert, et déjà l’heure est avancée; renvoyez le peuple, pour qu’ils aillent dans les villages acheter de quoi manger.
Ilipofika jioni, wanafunzi wake walienda kwake, wakamwambia, “Mahali hapa ni nyikani, na muda sasa umekwisha. Waage makutano ili waende zao vijijini wakajinunulie chakula.”
16 Mais Jésus leur dit: Il n’est pas nécessaire qu’ils y aillent; donnez-leur vous-mêmes à manger.
Yesu akawaambia, “Hakuna sababu ya wao kuondoka. Ninyi wapeni chakula.”
17 Ils lui répondirent: Nous n’avons ici que cinq pains et deux poissons.
Wakamjibu, “Tuna mikate mitano na samaki wawili tu.”
18 Jésus leur dit: Apportez-les moi ici.
Akawaambia, “Nileteeni hivyo vitu hapa.”
19 Et après avoir ordonné à la multitude de s’asseoir sur l’herbe, il prit les cinq pains et les deux poissons, et levant les yeux au ciel, il les bénit; puis rompant les pains, il les donna à ses disciples, et ses disciples au peuple.
Yesu akaagiza makutano wakae chini kwenye nyasi. Akaichukua ile mikate mitano na wale samaki wawili, akainua macho yake akatazama mbinguni, akavibariki na kuimega ile mikate. Kisha akawapa wanafunzi, nao wanafunzi wakawagawia makutano.
20 Ils en mangèrent tous et furent rassasiés; et les disciples emportèrent les restes, douze paniers pleins de morceaux.
Wote wakala, wakashiba. Nao wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu kumi na viwili.
21 Or, le nombre de ceux qui mangèrent fut de cinq mille hommes, outre les femmes et les petits enfants.
Idadi ya watu waliokula walikuwa wanaume wapatao 5,000, bila kuhesabu wanawake na watoto.
22 Aussitôt Jésus ordonna à ses disciples de monter dans la barque et de le précéder de l’autre côté de la mer, tandis qu’il renverrait le peuple.
Mara Yesu akawaambia wanafunzi wake waingie kwenye mashua watangulie kwenda ngʼambo ya bahari, wakati yeye alikuwa akiwaaga wale makutano.
23 Et, le peuple renvoyé, il monta seul sur la montagne pour prier. Or, le soir étant venu, il se trouvait là seul.
Baada ya kuwaaga, akaenda zake mlimani peke yake kuomba. Jioni ilipofika, Yesu alikuwa huko peke yake.
24 Cependant, la barque était agitée par les flots au milieu de la mer; car le vent était contraire.
Wakati huo ile mashua ilikuwa mbali kutoka nchi kavu ikisukwasukwa na mawimbi, kwa sababu upepo ulikuwa wa mbisho.
25 Mais à la quatrième veille de la nuit, il vint à eux marchant sur la mer.
Wakati wa zamu ya nne ya usiku, Yesu akawaendea wanafunzi wake akiwa anatembea juu ya maji.
26 Or, le voyant marcher sur la mer, ils se troublèrent et dirent; C’est un fantôme; et ils poussèrent des cris de frayeur.
Wanafunzi wake walipomwona akitembea juu ya maji, waliingiwa na hofu kuu, wakasema, “Ni mzimu.” Wakapiga yowe kwa kuogopa.
27 Mais Jésus aussitôt leur parla, disant: Ayez confiance, c’est moi, ne craignez point.
Lakini mara Yesu akasema nao, akawaambia, “Jipeni moyo! Ni mimi. Msiogope.”
28 Pierre, répondant, dit: Seigneur, si c’est vous, ordonnez-moi de venir à vous sur les eaux.
Petro akamjibu, “Bwana, ikiwa ni wewe, niambie nije kwako nikitembea juu ya maji.”
29 Et Jésus dit: Viens. Et Pierre descendant de la barque, marchait sur les eaux pour venir à Jésus.
Yesu akamwambia, “Njoo.” Basi Petro akatoka kwenye chombo, akatembea juu ya maji kumwelekea Yesu.
30 Mais, voyant la violence du vent, il eut peur; et comme il commençait à enfoncer, il cria, disant: Seigneur, sauvez-moi!
Lakini alipoona upepo mkali aliingiwa na hofu, naye akaanza kuzama, huku akipiga kelele, “Bwana, niokoe!”
31 Et à l’instant même Jésus étendant la main, le saisit, et lui dit: Homme de peu de foi, pourquoi as-tu douté?
Mara Yesu akaunyoosha mkono wake na kumshika, akamwambia, “Wewe mwenye imani haba, kwa nini uliona shaka?”
32 Or, lorsqu’ils furent montés dans la barque, le vent cessa.
Nao walipoingia ndani ya mashua, upepo ukakoma.
33 Alors ceux qui étaient dans la barque, vinrent et l’adorèrent, disant: Vraiment, vous êtes le fils de Dieu.
Ndipo wote waliokuwa ndani ya ile mashua wakamwabudu Yesu, wakisema, “Hakika, wewe ndiwe Mwana wa Mungu.”
34 Lorsqu’ils eurent traversé la mer, ils vinrent dans la terre de Génésar.
Walipokwisha kuvuka, wakafika nchi ya Genesareti.
35 Et quand les hommes de ce lieu l’eurent reconnu, ils envoyèrent dans toute cette contrée, et lui présentèrent tous les malades;
Watu wa eneo lile walipomtambua Yesu, walipeleka habari sehemu zote za jirani. Watu wakamletea wagonjwa wao wote,
36 Et ils lui demandaient de toucher seulement la frange de ses vêtements; et tous ceux qui la touchèrent furent guéris.
wakamsihi awaruhusu wagonjwa waguse tu pindo la vazi lake, nao wote waliomgusa, wakaponywa.

< Matthieu 14 >