< Marc 1 >

1 Commencement de l’Evangile de Jésus-Christ, fils de Dieu.
Mwanzo wa Injili ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
2 Comme il est écrit dans le prophète Isaïe: Voilà que j’envoie mon ange devant votre face, lequel préparera votre voie devant vous.
Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Tazama, nitamtuma mjumbe wangu mbele yako, atakayetengeneza njia mbele yako”:
3 Voix de quelqu’un qui crie dans le désert: Préparez la voie du Seigneur, faites droits ses sentiers.
“sauti ya mtu aliaye nyikani. ‘Itengenezeni njia ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.’”
4 Jean a été dans le désert, baptisant et prêchant le baptême de pénitence pour la rémission des péchés.
Yohana alikuja, akibatiza huko nyikani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi.
5 Et tout le pays de Judée, et tous les habitants de Jérusalem allaient à lui; et ils étaient baptisés par lui dans le fleuve du Jourdain, confessant leurs péchés.
Watu kutoka Uyahudi wote na sehemu zote za Yerusalemu walikuwa wakimwendea. Nao wakaziungama dhambi zao, akawabatiza katika Mto Yordani.
6 Or Jean était vêtu de poils de chameau, et d’une ceinture de cuir autour de ses reins; et il se nourrissait de sauterelles et de miel sauvage; et il prêchait, disant:
Yohana alivaa mavazi yaliyotengenezwa kwa singa za ngamia na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwitu.
7 Il vient après moi un plus puissant que moi; et je ne suis pas digne, me prosternant, de délier les cordons de sa chaussure.
Naye alihubiri akisema, “Baada yangu atakuja yeye aliye na uwezo kuniliko mimi, ambaye sistahili hata kuinama na kulegeza kamba za viatu vyake.
8 Moi je vous ai baptisés dans l’eau; mais lui vous baptisera dans l’Esprit-Saint.
Mimi nawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”
9 Or il arriva qu’en ces jours-là Jésus vint de Nazareth, ville de Galilée, et qu’il fut baptisé par Jean dans le Jourdain.
Wakati huo Yesu akaja kutoka Nazareti ya Galilaya, naye akabatizwa na Yohana katika Mto Yordani.
10 Et soudain, sortant de l’eau, il vit les deux ouverts, et l’Esprit descendant en forme de colombe, et se reposant sur lui.
Yesu alipokuwa akitoka ndani ya maji, aliona mbingu zikifunguka na Roho akishuka juu yake kama hua.
11 Et une voix vint des cieux: Vous êtes mon fils bien-aimé; c’est en vous que j’ai mis mes complaisances.
Nayo sauti kutoka mbinguni ikasema, “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”
12 Et aussitôt l’Esprit le poussa dans le désert.
Wakati huo huo, Roho akamwongoza Yesu kwenda nyikani,
13 Et il passa dans le désert quarante jours et quarante nuits; et il fut tenté par Satan; et il était parmi les bêtes, et les anges le servaient.
naye akawa huko nyikani kwa muda wa siku arobaini, akijaribiwa na Shetani. Alikaa na wanyama wa mwituni, nao malaika wakamhudumia.
14 Mais après que Jean eut été livré, Jésus vint en Galilée, prêchant l’Evangile du royaume de Dieu,
Baada ya Yohana kukamatwa na kutiwa gerezani, Yesu aliingia Galilaya akaanza kuhubiri habari njema ya Mungu,
15 Et disant: Parce que le temps est accompli, et que le royaume de Dieu est proche, faites pénitence et croyez à l’Evangile.
akisema, “Wakati umewadia, Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema.”
16 Or passant le long de la mer de Galilée, il vit Simon et André son frère, qui jetaient leurs filets dans la mer, car ils étaient pêcheurs;
Yesu alipokuwa akitembea kando ya Bahari ya Galilaya, aliwaona Simoni na Andrea nduguye wakizitupa nyavu zao baharini, kwa kuwa wao walikuwa wavuvi.
17 Et Jésus leur dit: Suivez-moi, et je vous ferai devenir pêcheurs d’hommes.
Yesu akawaambia, “Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu.”
18 Et aussitôt, laissant leurs filets, ils le suivirent.
Mara wakaacha nyavu zao, wakamfuata.
19 De là s’étant un peu avancé, il vit Jacques fils de Zébédée, et Jean son frère, qui raccommodaient leurs filets dans leur barque:
Alipokwenda mbele kidogo, akamwona Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana nduguye, wakiwa kwenye mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
20 Et au moment même, il les appela. Or laissant leur père Zébédée dans la barque avec les ouvriers, ils le suivirent.
Papo hapo akawaita, nao wakamwacha Zebedayo baba yao kwenye mashua pamoja na watumishi wa kuajiriwa, nao wakamfuata Yesu.
21 Ils vinrent ensuite à Capharnaüm; et d’abord entrant le jour du sabbat dans la synagogue, il les instruisait.
Wakaenda mpaka Kapernaumu. Ilipofika siku ya Sabato, mara Yesu akaingia sinagogi, akaanza kufundisha.
22 Et ils s’étonnaient de sa doctrine; car il les enseignait comme ayant autorité, et non comme les scribes.
Watu wakashangaa sana kwa mafundisho yake, kwa maana aliwafundisha kama yeye aliye na mamlaka, wala si kama walimu wa sheria.
23 Or il y avait dans leur synagogue un homme possédé d’un esprit impur, et il s’écria,
Wakati huo huo katika sinagogi lao palikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu,
24 Disant: Qu’importe à nous et à vous, Jésus de Nazareth? Êtes-vous venu pour nous perdre? Je sais que vous êtes le saint de Dieu.
naye akapiga kelele akisema, “Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakujua wewe ni nani. Wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu!”
25 Et Jésus le menaça disant: Tais-toi et sors de cet homme.
Lakini Yesu akamkemea, akamwambia, “Nyamaza kimya! Nawe umtoke!”
26 Alors l’esprit impur le déchirant, et criant d’une voix forte, sortit de lui.
Yule pepo mchafu akamtikisatikisa huyo mtu kwa nguvu, kisha akamtoka akipiga kelele kwa sauti kubwa.
27 Et ils furent tous saisis d’étonnement, de sorte qu’ils s’interrogeaient entre eux, disant: Qu’est ceci? quelle est cette doctrine nouvelle? Car il commande avec empire, même aux esprits impurs, et ils lui obéissent.
Watu wote wakashangaa, hata wakaulizana wao kwa wao, “Haya ni mambo gani? Ni mafundisho mapya, tena yenye mamlaka! Anaamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!”
28 Et sa renommée se répandit promptement dans tout le pays de Galilée.
Sifa zake zikaanza kuenea haraka katika eneo lote la karibu na Galilaya.
29 Et aussitôt, sortant de la synagogue, ils vinrent dans la maison de Simon et d’André, avec Jacques et Jean.
Mara walipotoka katika sinagogi, walikwenda pamoja na Yakobo na Yohana hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea.
30 Or la belle-mère de Simon était au lit, ayant la fièvre: et incontinent ils lui parlèrent d’elle.
Mama mkwe wa Simoni alikuwa kitandani, ana homa, nao wakamweleza Yesu habari zake.
31 Alors s’approchant, il la fit lever en prenant sa main; et sur-le-champ la fièvre la quitta, et elle les servait.
Hivyo Yesu akamwendea, akamshika mkono na kumwinua. Kisha homa ikamwacha, naye akaanza kuwahudumia.
32 Cependant, le soir venu, lorsque le soleil fut couché, ils lui amenèrent tous les malades, et les démoniaques.
Jioni ile baada ya jua kutua, watu wakamletea Yesu wagonjwa wote na waliopagawa na pepo wachafu.
33 Et toute la ville était assemblée à la porte.
Mji wote ukakusanyika mbele ya nyumba hiyo.
34 Et il guérit beaucoup de malades affligés de diverses infirmités, et il chassait beaucoup de démons; mais il ne leur permettait pas de dire qu’ils le connaissaient.
Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa ya aina mbalimbali. Akawatoa pepo wachafu wengi, lakini hakuwaacha hao pepo wachafu waseme, kwa sababu walimjua yeye ni nani.
35 Le lendemain, s’étant levé de grand matin, il sortit et s’en alla en un lieu désert, où il priait.
Alfajiri na mapema sana kulipokuwa bado kuna giza, Yesu akaamka, akaondoka, akaenda mahali pa faragha ili kuomba.
36 Simon et ceux qui étaient avec lui le suivirent.
Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta,
37 Quand ils l’eurent trouvé, ils lui dirent: Tout le monde vous cherche.
nao walipomwona, wakamwambia, “Kila mtu anakutafuta!”
38 Il leur répondit: Allons dans les villages et les villes voisines, afin que je prêche là aussi; car c’est pour cela que je suis venu.
Yesu akawajibu, “Twendeni mahali pengine kwenye vijiji jirani, ili niweze kuhubiri huko pia, kwa sababu hicho ndicho nilichokuja kukifanya.”
39 Il prêchait donc dans leurs synagogues et dans toute la Galilée; et il chassait les démons.
Kwa hiyo akazunguka Galilaya kote, akihubiri katika masinagogi yao na kutoa pepo wachafu.
40 Or un lépreux vint à lui, le suppliant et se jetant à genoux, il lui dit: Si vous voulez, vous pouvez me guérir.
Mtu mmoja mwenye ukoma alimjia Yesu, akamwomba akipiga magoti, akamwambia, “Ukitaka, waweza kunitakasa.”
41 Jésus, ému de compassion, étendit sa main, et le touchant, lui dit: Je le veux, sois guéri.
Yesu, akiwa amejawa na huruma, akanyoosha mkono wake akamgusa, akamwambia, “Nataka. Takasika!”
42 Lorsqu’il eut parlé, la lèpre disparut soudain de cet homme, et il fut guéri.
Mara ukoma ukamtoka, naye akatakasika.
43 Mais Jésus le renvoya aussitôt, le menaça,
Baada ya Yesu kumwonya vikali, akamruhusu aende zake
44 Et lui dit: Garde-toi de rien dire à personne; mais va et montre-toi au prince des prêtres, et offre pour ta guérison ce que Moïse a ordonné, en témoignage pour eux.
akimwambia, “Hakikisha humwambii mtu yeyote habari hizi, bali nenda ukajionyeshe kwa kuhani, na ukatoe sadaka alizoagiza Mose kwa utakaso wako, ili kuwa ushuhuda kwao.”
45 Mais celui-ci étant parti, se mit à raconter et à publier partout ce qui s’était passé; de sorte que Jésus ne pouvait plus paraître publiquement dans la ville, mais qu’il se tenait dehors dans des lieux déserts; et l’on venait à lui de tous côtés.
Lakini yule mtu akaenda akaanza kutangaza habari za kuponywa kwake waziwazi. Kwa hiyo, Yesu hakuweza tena kuingia katika miji waziwazi lakini alikaa sehemu zisizo na watu. Hata hivyo watu wakamfuata huko kutoka kila upande.

< Marc 1 >