< Luc 6 >

1 Or, il arriva qu’un jour de sabbat, second-premier, comme Jésus passait par les blés, ses disciples arrachaient les épis et en mangeaient, en les froissant dans leurs mains.
Ikawa siku moja ya Sabato Yesu alikuwa akipita katika mashamba ya nafaka, nao wanafunzi wake wakaanza kuvunja masuke ya nafaka, wakayafikicha kwa mikono yao na kula punje zake.
2 Quelques-uns des pharisiens leur disaient: Pourquoi faites-vous ce qui n’est point permis les jours du sabbat?
Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, “Mbona mnafanya mambo yasiyo halali kufanywa siku ya Sabato?”
3 Jésus leur répondant, dit: N’avez-vous point lu ce que fit David lorsqu’il eut faim, lui et ceux qui étaient avec lui;
Yesu akawajibu, “Je, ninyi hamjasoma kamwe alivyofanya Daudi wakati yeye na wenzake walikuwa na njaa?
4 Comment il entra dans la maison de Dieu, et prit les pains de proposition, en mangea, et en donna à ceux qui étaient avec lui, quoiqu’il ne soit pas permis d’en manger, si ce n’est aux prêtres?
Aliingia ndani ya nyumba ya Mungu, akaichukua na kuila ile mikate iliyowekwa wakfu, ambayo ni halali kuliwa na makuhani peke yao. Naye pia akawapa wenzake.”
5 Et il ajouta: Le Fils de l’homme est maître même du sabbat.
Yesu akawaambia, “Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato.”
6 Il arriva, un autre jour de sabbat, qu’il entra dans la synagogue, et qu’il y enseignait. Or il y avait là un homme dont la main droite était desséchée.
Ikawa siku nyingine ya Sabato, Yesu aliingia ndani ya sinagogi na akawa anafundisha. Huko palikuwa na mtu ambaye mkono wake wa kuume ulikuwa umepooza.
7 Et les scribes et les pharisiens observaient s’il le guérirait le jour du sabbat, afin de trouver de quoi l’accuser.
Mafarisayo na walimu wa sheria walikuwa wakitafuta sababu ya kumshtaki Yesu. Kwa hivyo wakawa wanamwangalia sana ili waone kama ataponya katika siku ya Sabato.
8 Mais il connaissait leurs pensées; il dit à l’homme qui avait la main desséchée: Lève-toi et tiens-toi là debout au milieu. Et, se levant, il se tint debout.
Lakini Yesu alijua mawazo yao, hivyo akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Inuka usimame mbele ya watu wote.” Hivyo yule mtu akainuka, akasimama mbele yao wote.
9 Alors Jésus leur dit: Je vous le demande, est-il permis, les jours du sabbat, de faire du bien ou du mal, de sauver une âme ou de la perdre?
Ndipo Yesu akawaambia wale walimu wa sheria na Mafarisayo, “Nawauliza ninyi, ni lipi lililo halali siku ya Sabato? Ni kutenda mema au kutenda mabaya? Ni kuokoa maisha au kuyaangamiza?”
10 Et après les avoir regardés tous, il dit à l’homme: Etends ta main. Il retendit, et sa main redevint saine.
Akawatazama watu wote waliokuwepo, kisha akamwambia yule aliyepooza mkono, “Nyoosha mkono wako!” Akaunyoosha na mkono wake ukaponywa kabisa.
11 Mais eux, remplis de dépit, se consultaient sur ce qu’ils feraient à Jésus.
Wale wakuu wakakasirika sana, wakashauriana wao kwa wao ni nini watakachomtendea Yesu.
12 Il arriva qu’en ces jours-là il se retira sur la montagne pour prier, et y passa toute la nuit à prier Dieu.
Ikawa katika siku hizo Yesu alikwenda mlimani kuomba, akakesha usiku kucha akimwomba Mungu.
13 Et quand le jour fut venu, il appela ses disciples, et il en choisit douze d’entre eux (qu’il nomma aussi apôtres):
Kulipopambazuka, akawaita wanafunzi wake, naye akachagua kumi na wawili, ambao pia aliwaita mitume:
14 Simon, auquel il donna le surnom de Pierre, et André son frère; Jacques et Jean; Philippe et Barthélemi;
Simoni aliyemwita Petro, Andrea nduguye, Yakobo, Yohana, Filipo, Bartholomayo,
15 Matthieu et Thomas; Jacques, fils d’Alphée, et Simon, appelé le Zélé;
Mathayo, Tomaso, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni aliyeitwa Zelote,
16 Judas, frère de Jacques, et Judas Iscariote, qui fut le traître.
Yuda mwana wa Yakobo, na Yuda Iskariote ambaye alikuwa msaliti.
17 Et, descendant avec eux, il s’arrêta dans une plaine, de même que la troupe de ses disciples, et une grande multitude de peuple de toute la Judée, de Jérusalem, de la contrée maritime, de Tyr et de Sidon,
Akashuka pamoja nao, akasimama mahali penye uwanja tambarare. Hapo palikuwa na idadi kubwa ya wanafunzi wake na umati mkubwa wa watu kutoka sehemu zote za Uyahudi, kutoka Yerusalemu, na kutoka pwani ya Tiro na Sidoni.
18 Qui étaient venus pour l’entendre et pour être guéris de leurs maladies. Or ceux aussi qui étaient tourmentés par des esprits impurs, étaient guéris.
Walikuwa wamekuja kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao. Wale waliokuwa wakiteswa na pepo wachafu akawaponya.
19 Et toute la foule cherchait à le toucher, parce qu’une vertu sortait de lui, et les guérissait tous.
Watu wote walikuwa wanajitahidi kumgusa kwa sababu nguvu zilikuwa zikimtoka na kuwaponya wote.
20 Alors Jésus, les yeux levés sur ses disciples, dit: Bienheureux, ô pauvres! parce qu’à vous appartient le royaume de Dieu.
Akawatazama wanafunzi wake, akasema: “Mmebarikiwa ninyi mlio maskini, kwa sababu Ufalme wa Mungu ni wenu.
21 Bienheureux, vous qui maintenant avez faim, parce que vous serez rassasiés. Bienheureux, vous qui pleurez maintenant, parce que vous rirez,
Mmebarikiwa ninyi mlio na njaa sasa, kwa sababu mtashibishwa. Mmebarikiwa ninyi mnaolia sasa, kwa sababu mtacheka.
22 Vous serez heureux lorsque les hommes vous haïront, vous éloigneront, vous injurieront, et rejetteront votre nom comme mauvais, à cause du Fils de l’homme.
Mmebarikiwa ninyi, watu watakapowachukia, watakapowatenga na kuwatukana na kulikataa jina lenu kama neno ovu, kwa ajili ya Mwana wa Adamu.
23 Réjouissez-vous en ce jour-là, et tressaillez d’allégresse, parce que votre récompense est grande dans le ciel; car c’est ainsi que leurs pères faisaient aux prophètes.
“Furahini na kurukaruka kwa shangwe, kwa sababu thawabu yenu ni kubwa mbinguni, kwa kuwa hivyo ndivyo baba zao walivyowatenda manabii.
24 Cependant, malheur à vous, riches, parce que vous avez votre consolation.
“Lakini ole wenu ninyi mlio matajiri, kwa sababu mmekwisha kupokea faraja yenu.
25 Malheur à vous qui êtes rassasiés, parce que vous aurez faim. Malheur à vous qui riez maintenant, parce que vous gémirez et vous pleurerez.
Ole wenu ninyi mlioshiba sasa, maana mtaona njaa. Ole wenu ninyi mnaocheka sasa, maana mtaomboleza na kulia.
26 Malheur, quand les hommes vous loueront, car c’est ainsi que leurs pères faisaient aux faux prophètes.
Ole wenu watu watakapowasifu, kwani ndivyo baba zao walivyowasifu manabii wa uongo.
27 Mais je vous dis, à vous qui écoutez: Aimez vos ennemis, faites du bien à ceux qui vous haïssent.
“Lakini nawaambia ninyi mnaonisikia: Wapendeni adui zenu. Watendeeni mema wanaowachukia.
28 Bénissez ceux qui vous maudissent, et priez pour ceux qui vous calomnient.
Wabarikini wale wanaowalaani, waombeeni wale wanaowatendea mabaya.
29 À quiconque vous frappe sur une joue, présentez encore l’autre. Et pour celui qui vous prend votre manteau, laissez-le prendre votre tunique.
Kama mtu akikupiga shavu moja, mgeuzie na la pili pia. Mtu akikunyangʼanya koti lako, usimzuie kuchukua joho pia.
30 Donnez à quiconque vous demande; et ne redemandez point votre bien à celui qui vous le ravit.
Mpe kila akuombaye, na kama mtu akichukua mali yako usitake akurudishie.
31 Comme vous voulez que les hommes vous fassent, faites-le leur pareillement.
Watendeeni wengine kama ambavyo mngetaka wawatendee ninyi.
32 Si vous aimez ceux qui vous aiment, quel est votre mérite? puisque les pécheurs aiment aussi ceux qui les aiment.
“Kama mkiwapenda tu wale wanaowapenda, mwapata sifa gani? Hata ‘wenye dhambi’ huwapenda wale wawapendao.
33 Et si vous faites du bien à ceux qui vous en font, quel est votre mérite? puisque les pécheurs même le font.
Tena mkiwatendea mema wale tu wanaowatendea ninyi mema, mwapata sifa gani? Hata ‘wenye dhambi’ hufanya vivyo hivyo.
34 Et si vous prêtez à ceux de qui vous espérez recevoir, quel remerciement méritez-vous? car les pécheurs aussi prêtent aux pécheurs, pour en recevoir un pareil avantage.
Tena mnapowakopesha wale tu mnaotegemea wawalipe, mwapata sifa gani? Hata ‘wenye dhambi’ huwakopesha ‘wenye dhambi’ wenzao wakitarajia kulipwa mali yao yote.
35 Mais vous, aimez vos ennemis, faites du bien et prêtez, sans en rien espérer, et votre récompense sera grande, et vous serez les fils du Très-Haut; car il est bon pour les ingrats même et pour les méchants.
Lakini wapendeni adui zenu, watendeeni mema, wakopesheni bila kutegemea kurudishiwa mlichokopesha. Ndipo thawabu yenu itakapokuwa kubwa, nanyi mtakuwa wana wa Aliye Juu Sana, kwa sababu yeye ni mwema kwa watu wasio na shukrani na kwa wale waovu.
36 Soyez donc miséricordieux, comme votre Père est miséricordieux.
Kuweni na huruma, kama Baba yenu alivyo na huruma.
37 Ne jugez point, et vous ne serez point jugés; ne condamnez point, et vous ne serez point condamnés; remettez, et il vous sera remis.
“Msihukumu, nanyi hamtahukumiwa. Msilaumu, nanyi hamtalaumiwa. Sameheni, nanyi mtasamehewa.
38 Donnez, et il vous sera donné; on versera dans votre sein une bonne mesure, pressée, bien remuée, et débordante. Car on usera pour vous de la même mesure dont vous aurez usé pour les autres.
Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa. Kipimo cha kujaa na kushindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile mpimacho, ndicho mtakachopimiwa.”
39 Il leur faisait aussi cette comparaison: Un aveugle peut-il conduire un aveugle? ne tomberont-ils pas tous deux dans une fosse?
Pia akawapa mfano akasema, “Je, kipofu aweza kumwongoza kipofu? Je, wote wawili hawatatumbukia shimoni?
40 Le disciple n’est point au-dessus du maître; mais tout disciple sera parfait, s’il est comme son maître.
Mwanafunzi hawezi kumzidi mwalimu wake, ila yule aliyehitimu aweza kuwa kama mwalimu wake.
41 Pourquoi voyez-vous la paille dans l’œil de votre frère, et n’apercevez-vous point la poutre qui est dans votre œil?
“Mbona unatazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, wala huoni boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe?
42 Ou comment pouvez-vous dire à votre frère: Mon frère, laisse-moi ôter la paille de ton œil, ne voyant pas toi-même la poutre qui est dans le tien? Hypocrite, ôte premièrement la poutre de ton œil, et alors tu verras à ôter la paille de l’œil de ton frère.
Utawezaje kumwambia ndugu yako, ‘Ndugu yangu, acha nitoe kibanzi kilicho ndani ya jicho lako,’ wakati wewe mwenyewe huoni boriti iliyo ndani ya jicho lako? Ewe mnafiki, ondoa boriti ndani ya jicho lako kwanza, ndipo utaweza kuona dhahiri jinsi ya kuondoa kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako.
43 Un arbre n’est pas bon s’il produit de mauvais fruits, et un arbre n’est pas mauvais s’il produit du bon fruit.
“Hakuna mti mzuri uzaao matunda mabaya, wala hakuna mti mbaya uzaao matunda mazuri.
44 Car chaque arbre se connaît par son fruit. On ne cueille point de figues sur des épines, et on ne vendange point du raisin sur des ronces.
Kila mti hujulikana kwa matunda yake. Kwa maana watu hawachumi tini kwenye miiba, wala zabibu kwenye michongoma.
45 L’homme bon tire le bien du bon trésor de son cœur; et l’homme mauvais tire le mal du mauvais trésor. Car la bouche parle de l’abondance du cœur.
Vivyo hivyo mtu mwema hutoa mambo mema kutoka kwenye hazina ya moyo wake, naye mtu mwovu hutoa mambo maovu kutoka kwenye hazina ya moyo wake. Kwa kuwa mtu hunena kwa kinywa chake yale yaliyoujaza moyo wake.
46 Mais pourquoi m’appelez-vous Seigneur, Seigneur, et ne faites point ce que je dis?
“Kwa nini mnaniita, ‘Bwana, Bwana,’ nanyi hamfanyi ninayowaambia?
47 Quiconque vient à moi, écoute mes paroles et les met en pratique, je vous montrerai à qui il est semblable.
Nitawaonyesha jinsi alivyo mtu yule anayekuja kwangu na kusikia maneno yangu na kuyatenda.
48 Il est semblable à un homme qui, bâtissant une maison, a creusé très avant, et en a posé le fondement sur la pierre: l’inondation survenant, le fleuve s’est brisé contre cette maison, et n’a pu l’ébranler, parce qu’elle était fondée sur la pierre.
Yeye ni kama mtu aliyejenga nyumba, akachimba chini sana, na kuweka msingi kwenye mwamba. Mafuriko yalipokuja, maji ya ghafula yaliipiga ile nyumba, lakini haikutikisika, kwa sababu ilikuwa imejengwa vizuri.
49 Mais celui qui écoute et ne pratique point, est semblable à un homme qui a bâti sa maison sur la terre, sans fondement: le fleuve s’est brisé contre elle, et elle s’est écroulée aussitôt; et la ruine de cette maison a été grande.
Lakini yeye anayesikia maneno yangu wala asiyatende, ni kama mtu aliyejenga nyumba juu ya ardhi bila kuweka msingi. Mafuriko yalipoikumba nyumba ile, ikaanguka mara na kubomoka kabisa.”

< Luc 6 >