< Luc 12 >

1 Cependant une grande multitude s’étant assemblée autour de lui, de sorte qu’ils marchaient les uns sur les autres, il commença à dire à ses disciples: Gardez-vous du levain des pharisiens, qui est l’hypocrisie.
Wakati huo, umati mkubwa wa watu maelfu, walipokuwa wamekusanyika hata wakawa wanakanyagana, Yesu akaanza kuzungumza kwanza na wanafunzi wake, akawaambia: “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo, yaani, unafiki wao.
2 Car rien de caché qui ne se révèle, ni de secret qui ne se sache.
Hakuna jambo lolote lililositirika ambalo halitafunuliwa, au lililofichwa ambalo halitajulikana.
3 Ainsi ce que vous avez dit dans les ténèbres se dira à la lumière; et ce que vous avez dit à l’oreille, dans les chambres à coucher, sera publié sur les toits.
Kwa hiyo, lolote mlilosema gizani litasikiwa nuruni. Na kile mlichonongʼona masikioni mkiwa kwenye vyumba vya ndani, kitatangazwa juu ya paa.
4 Or je vous dis à vous, qui êtes mes amis: Ne craignez point ceux qui tuent le corps, et après cela ne peuvent plus rien faire.
“Nawaambieni rafiki zangu, msiwaogope wale wauao mwili, lakini baada ya hilo hawawezi kufanya lolote zaidi.
5 Mais je vous montrerai qui vous devez craindre: Craignez celui qui, après avoir ôté la vie, a le pouvoir d’envoyer dans la géhenne: oui, je vous le dis, craignez celui-là. (Geenna g1067)
Lakini nitawaambia nani wa kumwogopa: Mwogopeni yule ambaye baada ya kuua mwili, ana mamlaka ya kuwatupa motoni. Naam, nawaambia, mwogopeni huyo! (Geenna g1067)
6 Cinq passereaux ne se vendent-ils pas deux as, et cependant pas un d’eux n’est en oubli devant Dieu?
Mnajua kwamba shomoro watano huuzwa kwa senti mbili? Lakini Mungu hamsahau hata mmoja wao.
7 Les cheveux mêmes de votre tête sont tous comptés. Ne craignez donc point, vous valez plus que beaucoup de passereaux.
Naam, hata nywele za vichwa vyenu zote zimehesabiwa. Hivyo msiogope, kwa maana ninyi ni wa thamani kubwa kuliko shomoro wengi.
8 Or je vous le dis: Quiconque m’aura confessé devant les hommes, le Fils de l’homme aussi le confessera devant les anges de Dieu.
“Ninawaambia kwamba yeyote atakayenikiri mbele ya watu, Mwana wa Adamu naye atamkiri mbele za malaika wa Mungu.
9 Mais qui m’aura renié devant les hommes, sera renié devant les anges de Dieu.
Lakini yeye atakayenikana mimi mbele ya watu, Mwana wa Adamu naye atamkana mbele ya malaika wa Mungu.
10 Quiconque parle contre le Fils de l’homme, il lui sera remis; mais pour celui qui aura blasphémé contre l’Esprit-Saint, il ne lui sera pas remis.
Naye kila atakayenena neno baya dhidi ya Mwana wa Adamu atasamehewa, lakini yeyote atakayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
11 Lorsqu’on vous conduira dans les synagogues, devant les magistrats et les puissances, ne vous inquiétez point de quelle manière ou de ce que vous répondrez, ou bien de ce que vous direz.
“Watakapowapeleka katika masinagogi, na mbele ya watawala na wenye mamlaka, msiwe na wasiwasi kuhusu namna mtakavyojitetea au mtakavyosema.
12 Car l’Esprit-Saint vous enseignera à l’heure même ce qu’il vous faudra dire.
Kwa maana Roho Mtakatifu atawafundisha wakati huo huo mnachopaswa kusema.”
13 Alors quelqu’un de la foule lui dit: Maître, dites à mon frère de partager avec moi notre héritage.
Mtu mmoja katika umati wa watu akamwambia Yesu, “Mwalimu, mwambie ndugu yangu tugawane naye urithi wetu.”
14 Mais Jésus lui répondit: Homme, qui m’a établi juge sur vous, ou pour faire vos partages?
Lakini Yesu akamwambia, “Rafiki, ni nani aliyeniweka mimi kuwa hakimu wenu au msuluhishi juu yenu?”
15 Puis il leur dit: Voyez, et gardez-vous de toute avarice; car dans l’abondance même la vie de chacun ne dépend point des choses qu’il possède.
Ndipo Yesu akawaambia, “Jihadharini! Jilindeni na aina zote za choyo. Kwa maana maisha ya mtu hayatokani na wingi wa mali alizo nazo.”
16 Il leur dit ensuite cette parabole: il y avait un homme riche dont le champ rapportait beaucoup de fruits;
Kisha akawaambia mfano huu: “Shamba la mtu mmoja tajiri lilizaa sana.
17 Or il pensait en lui-même, disant: Que ferai-je, car je n’ai point où serrer mes fruits?
Akawaza moyoni mwake, ‘Nifanye nini? Sina mahali pa kuhifadhi mavuno yangu.’
18 Et il dit: Voici ce que je ferai: je détruirai mes greniers, et j’en ferai de plus grands, et j’y rassemblerai tous mes produits et tous mes biens.
“Ndipo huyo tajiri akasema, ‘Nitafanya hivi: Nitabomoa ghala zangu za nafaka na kujenga nyingine kubwa zaidi na huko nitayahifadhi mavuno yangu yote na vitu vyangu.
19 Et je dirai à mon âme: Mon âme, tu as beaucoup de biens en réserve pour plusieurs années; repose-toi, mange, bois, fais grande chère.
Nami nitaiambia nafsi yangu, “Nafsi, unavyo vitu vingi vizuri ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi. Pumzika; kula, unywe, ufurahi.”’
20 Mais Dieu lui dit: Insensé, cette nuit même on te redemandera ton âme; et ce que tu as amassé, à qui sera-t-il?
“Lakini Mungu akamwambia, ‘Mpumbavu wewe! Usiku huu uhai wako unatakiwa. Sasa hivyo vitu ulivyojiwekea akiba vitakuwa vya nani?’
21 Ainsi est celui qui thésaurise pour lui, et qui n’est point riche devant Dieu.
“Hivyo ndivyo ilivyo kwa wale wanaojiwekea mali lakini hawajitajirishi kwa Mungu.”
22 Et il dit à ses disciples: C’est pourquoi je vous dis: Ne vous inquiétez point pour votre vie, de ce que vous mangerez; ni pour votre corps, de quoi vous le vêtirez.
Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Kwa hiyo nawaambia, msisumbukie maisha yenu kwamba mtakula nini; au msumbukie miili yenu kwamba mtavaa nini.
23 La vie est plus que la nourriture, et le corps plus que le vêtement.
Maisha ni zaidi ya chakula, na mwili ni zaidi ya mavazi.
24 Considérez les corbeaux, ils ne sèment ni ne moissonnent, ils n’ont ni cellier ni grenier, et Dieu les nourrit. Combien ne valez-vous pas plus qu’eux?
Fikirini ndege! Wao hawapandi wala hawavuni, hawana ghala wala popote pa kuhifadhi nafaka; lakini Mungu huwalisha. Ninyi ni wa thamani zaidi kuliko ndege!
25 Qui de vous, en s’inquiétant ainsi, peut ajouter à sa taille une seule coudée?
Ni nani miongoni mwenu ambaye kwa kujitaabisha kwake anaweza kujiongezea hata saa moja zaidi katika maisha yake?
26 Si donc vous ne pouvez même pas les moindres choses, pourquoi vous inquiéter des autres?
Kama hamwezi kufanya jambo dogo kama hilo, kwa nini basi kuyasumbukia hayo mengine?
27 Considérez les lis comme ils croissent; ils ne travaillent ni ne filent: et cependant je vous le dis, Salomon lui-même, dans toute sa gloire, n’était pas vêtu comme l’un d’eux.
“Angalieni maua jinsi yameavyo: Hayafanyi kazi wala hayafumi. Lakini nawaambia, hata Solomoni katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo ya hayo maua.
28 Or si l’herbe qui est aujourd’hui dans les champs, et qui demain sera jetée au four, Dieu la revêt ainsi, combien plus le fera-t-il pour vous, hommes de peu de foi?
Basi ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya shambani, ambayo leo yapo, na kesho yanatupwa motoni, si atawavika ninyi vizuri zaidi, enyi wa imani haba!
29 Ne demandez donc point ce que vous aurez à manger ou à boire, et ne vous élevez pas si haut;
Wala msisumbuke mioyoni mwenu mtakula nini au mtakunywa nini. Msiwe na wasiwasi juu ya haya.
30 Car ce sont ces choses que les nations du monde recherchent; mais votre Père sait que vous en avez besoin.
Watu wa mataifa ya duniani husumbuka sana kuhusu vitu hivi vyote, lakini Baba yenu anafahamu kuwa mnahitaji haya yote.
31 Ainsi cherchez premièrement le royaume de Dieu et sa justice; et toutes ces choses vous seront données par surcroît.
Bali utafuteni Ufalme wa Mungu, na haya yote atawapa pia.
32 Ne craignez point, petit troupeau, parce qu’il a plu à votre Père de vous donner son royaume.
“Msiogope enyi kundi dogo, kwa maana Baba yenu ameona vyema kuwapa ninyi Ufalme.
33 Vendez ce que vous avez et donnez l’aumône. Faites-vous des bourses que le temps n’use point, un trésor qui ne vous fasse pas défaut dans les cieux, où le voleur n’approche point, et où les vers ne rongent point.
Uzeni mali zenu mkawape maskini. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, mkajiwekee hazina mbinguni isiyokwisha, mahali ambapo mwizi hakaribii wala nondo haharibu.
34 Car où est votre trésor, là sera aussi votre cœur.
Kwa sababu mahali hazina yako ilipo, hapo ndipo moyo wako utakapokuwa pia.
35 Ceignez vos reins, et ayez en vos mains les lampes allumées;
“Kuweni tayari mkiwa mmevikwa kwa ajili ya huduma na taa zenu zikiwa zinawaka,
36 Semblables à des hommes qui attendent que leur maître revienne des noces; afin que lorsqu’il viendra et frappera à la porte, ils lui ouvrent aussitôt.
kama watumishi wanaomngojea bwana wao arudi kutoka kwenye karamu ya arusi, ili ajapo na kubisha mlango waweze kumfungulia mara.
37 Heureux ces serviteurs, que le maître, quand il viendra, trouvera veillant! En vérité, je vous le dis, il se ceindra, et les fera mettre à table, et passant de l’un à l’autre, il les servira.
Heri wale watumishi ambao bwana wao atakapokuja atawakuta wakiwa wanakesha. Amin, nawaambia, atajifunga mkanda wake na kuwaketisha ili wale, naye atakuja na kuwahudumia.
38 Et s’il vient à la seconde veille, et s’il vient à la troisième veille, et qu’il les trouve ainsi, heureux sont ces serviteurs.
Itakuwa heri kwa watumwa hao ikiwa bwana wao atakapokuja atawakuta wamekesha hata kama atakuja mnamo usiku wa manane, au karibu na mapambazuko.
39 Car sachez bien que si le père de famille savait à quelle heure le voleur doit venir, il veillerait et ne laisserait point percer sa maison.
Lakini fahamuni jambo hili: Kama mwenye nyumba angalijua saa mwizi atakuja, asingaliiacha nyumba yake kuvunjwa.
40 Et vous aussi, tenez-vous prêts; parce qu’à l’heure que vous ne pensez pas, le Fils de l’homme viendra.
Ninyi nanyi hamna budi kuwa tayari, kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja saa msiyotazamia.”
41 Or Pierre lui dit: Seigneur, est-ce pour nous que vous dites cette parabole, ou pour tout le monde?
Ndipo Petro akamuuliza, “Bwana, mfano huu unatuambia sisi peke yetu au watu wote?”
42 Et le Seigneur dit: Qui, pensez-vous, est le dispensateur fidèle et prudent que le maître a établi sur tous ses serviteurs pour leur distribuer, dans le temps, leur mesure de froment?
Yesu akamjibu, “Ni yupi basi wakili mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamfanya msimamizi juu ya watumishi wake wote, ili awape watumishi wengine chakula chao wakati unaofaa?
43 Heureux ce serviteur que le maître, lorsqu’il viendra, trouvera agissant ainsi!
Heri mtumishi yule ambaye bwana wake atakaporudi atamkuta akifanya hivyo.
44 Je vous dis, en vérité, qu’il l’établira sur tous les biens qu’il possède.
Amin nawaambia, atamweka mtumishi huyo kuwa msimamizi wa mali yake yote.
45 Que si ce serviteur dit en son cœur: Mon maître tarde à venir; et qu’il commence à battre les serviteurs et les servantes, à manger, à boire et à s’enivrer;
Lakini kama yule mtumishi atasema moyoni mwake, ‘Bwana wangu anakawia kurudi,’ kisha akaanza kuwapiga wale watumishi wa kiume na wa kike, na kula na kunywa na kulewa.
46 Le maître de ce serviteur viendra le jour où il ne s’y attend pas, et à l’heure qu’il ne sait pas, et il le divisera, et il lui donnera ainsi sa part avec les infidèles.
Basi bwana wa mtumishi huyo atakuja siku asiyodhani na saa asiyoijua. Atamkata vipande vipande na kumweka katika sehemu moja pamoja na wale wasioamini.
47 Mais ce serviteur, qui a connu la volonté de son maître, et ne s’est pas tenu prêt, et de cette manière n’a pas agi selon sa volonté, recevra un grand nombre de coups;
“Yule mtumishi anayefahamu vyema mapenzi ya bwana wake na asijiandae wala kufanya kama apendavyo bwana wake, atapigwa kwa mapigo mengi.
48 Celui qui ne l’a pas connue, et qui a fait des choses dignes de châtiment, recevra peu de coups. Car à celui à qui on a donné beaucoup, on demandera beaucoup; et de celui à qui on a confié beaucoup, on exigera davantage.
Lakini yeyote ambaye hakujua naye akafanya yale yastahiliyo kupigwa, atapigwa kidogo. Yeyote aliyepewa vitu vingi, atadaiwa vingi; na yeyote aliyekabidhiwa vingi, kwake vitatakiwa vingi.
49 Je suis venu jeter un feu sur la terre; et que veux-je, sinon qu’il s’allume?
“Nimekuja kuleta moto duniani; laiti kama ungekuwa tayari umewashwa!
50 Je dois être baptisé d’un baptême; or combien je me sens pressé jusqu’à ce qu’il s’accomplisse?
Lakini ninao ubatizo ambao lazima nibatizwe, nayo dhiki yangu ni kuu mpaka ubatizo huo ukamilike!
51 Pensez-vous que je sois venu apporter la paix sur la terre? Non, je vous le dis; mais la division.
Mnadhani nimekuja kuleta amani duniani? La, nawaambia sivyo, nimekuja kuleta mafarakano.
52 Car, désormais, dans une seule maison, cinq seront divisés, trois contre deux, et deux contre trois;
Kuanzia sasa, kutakuwa na watu watano katika nyumba moja, watatu dhidi ya wawili, na wawili dhidi ya watatu.
53 Seront divisés: le père contre le fils, et le fils contre le père; la mère contre la fille, et la fille contre la mère; la belle-mère contre sa belle-fille, et la belle-fille contre sa belle-mère.
Watafarakana baba dhidi ya mwanawe na mwana dhidi ya babaye, mama dhidi ya bintiye na binti dhidi ya mamaye, naye mama mkwe dhidi ya mkwewe na mkwe dhidi ya mama mkwe wake.”
54 Il disait aussi au peuple: Lorsque vous voyez un nuage se former au couchant, aussitôt vous dites: La pluie vient, et il arrive ainsi.
Pia Yesu akauambia ule umati wa watu, “Mwonapo wingu likitokea magharibi, mara mwasema, ‘Mvua itanyesha,’ nayo hunyesha.
55 Et quand vous voyez souffler le vent du midi, vous dites: Il fera chaud, et cela arrive.
Nanyi mwonapo upepo wa kusini ukivuma, ninyi husema, ‘Kutakuwa na joto,’ na huwa hivyo.
56 Hypocrites, vous savez juger d’après l’aspect du ciel et de la terre; mais ce temps-ci, comment ne le reconnaissez-vous point?
Enyi wanafiki! Mnajua jinsi ya kutambua kuonekana kwa dunia na anga. Inakuwaje basi kwamba mnashindwa kutambua wakati huu wa sasa?
57 Comment ne discernez-vous pas de vous-mêmes ce qui est juste?
“Kwa nini hamwamui wenyewe lililo haki?
58 Lorsque tu vas avec ton adversaire devant un magistrat, tâche de te dégager de lui en chemin, de peur qu’il ne te traîne devant le juge et que le juge ne te livre à l’exécuteur, et que l’exécuteur ne te jette en prison.
Uwapo njiani na mshtaki wako kwenda kwa hakimu, jitahidi kupatana naye mkiwa njiani. La sivyo, atakupeleka kwa hakimu, naye hakimu atakukabidhi kwa afisa, naye afisa atakutupa gerezani.
59 Je te le dis, tu n’en sortiras point que tu n’aies payé jusqu’à la dernière obole.
Nakuambia, hautatoka humo hadi uwe umelipa senti ya mwisho.”

< Luc 12 >