< Jérémie 46 >

1 Parole du Seigneur qui fut adressée à Jérémie, le prophète, contre les nations;
Hili ni neno la Bwana lililomjia nabii Yeremia kuhusu mataifa:
2 À l’Egypte, contre l’armée de Pharaon Néchao, roi d’Egypte, qui était auprès du fleuve d’Euphrate à Charcamis, que Nabuchodonosor, roi de Babylone, battit dans ]a quatrième année de Joakim, fils de Josias, roi de Juda.
Kuhusu Misri: Huu ni ujumbe dhidi ya jeshi la Farao Neko mfalme wa Misri, lililoshindwa huko Karkemishi kwenye Mto Frati na Nebukadneza mfalme wa Babeli, katika mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda:
3 Préparez le grand bouclier et le petit bouclier, et avancez-vous pour la guerre.
“Wekeni tayari ngao zenu, kubwa na ndogo, mtoke kwa ajili ya vita!
4 Attelez les chevaux, montez, cavaliers, mettez des casques, polissez vos lances, revêtez-vous de vos cuirasses.
Fungieni farasi lijamu, pandeni farasi! Shikeni nafasi zenu mkiwa mmevaa chapeo! Isugueni mikuki yenu, vaeni dirii vifuani!
5 Quoi donc? Je les ai vus eux-mêmes effrayés et tournant le dos; leurs braves taillés en pièces; ils ont fui en se précipitant, et n’ont pas regardé derrière eux; la terreur vient de toutes parts, dit le Seigneur.
Je, ninaona nini? Wametiwa hofu, wanarudi nyuma, askari wao wameshindwa. Wanakimbia kwa haraka pasipo kutazama nyuma, tena kuna hofu kuu kila upande,” asema Bwana.
6 Que l’homme agile ne fuie pas, que le brave ne croie pas se sauver; vers l’aquilon, près de l’Euphrate, ils ont été vaincus et renversés.
Walio wepesi na wenye mbio hawawezi kukimbia, wala wenye nguvu hawawezi kutoroka. Kaskazini, kando ya Mto Frati, wanajikwaa na kuanguka.
7 Qui est celui qui monte comme un fleuve, et dont les eaux profondes s’enflent comme celles des grandes rivières?
“Ni nani huyu ajiinuaye kama Mto Naili, kama mito yenye maji yanayofanya mawimbi?
8 L’Egypte monte comme un fleuve, et ses flots s’agiteront comme des fleuves, et elle dira: En montant je couvrirai la terre, je perdrai la cité et ses habitants.
Misri hujiinua kama Mto Naili, kama mito yenye maji yanayofanya mawimbi. Husema, ‘Nitainuka na kufunika dunia, nitaiangamiza miji na watu wake.’
9 Montez sur vos chevaux, et sautez sur vos chars; qu’ils s’avancent, les braves d’Ethiopie, et les Lybiens tenant des boucliers, et les Lydiens saisissant et lançant des flèches.
Songeni mbele, enyi farasi! Endesheni kwa ukali, enyi magari ya farasi, Endeleeni mbele, enyi mashujaa: watu wa Kushi na Putu wachukuao ngao, watu wa Ludi wavutao upinde.
10 Mais c’est le jour du Seigneur, Dieu des armées, jour de vengeance, pour tirer vengeance de ses ennemis; le glaive dévorera, et il se rassasiera, et il s’enivrera de leur sang; car la victime du Seigneur Dieu des armées est dans la terre de l’aquilon, près du fleuve de l’Euphrate.
Lakini ile siku ni ya Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, siku ya kulipiza kisasi, kisasi juu ya adui zake. Upanga utakula hata utakapotosheka, hadi utakapozima kiu yake kwa damu. Kwa maana Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatoa dhabihu kwenye nchi ya kaskazini, kando ya Mto Frati.
11 Monte à Galaad, et prends de la résine, vierge fille de l’Egypte; vainement tu multiplies les remèdes; il n’y aura pas de guérison pour toi.
“Panda hadi Gileadi ukapate zeri, ee Bikira Binti wa Misri. Lakini umetumia dawa nyingi bila mafanikio; huwezi kupona.
12 Les nations ont entendu ton ignominie, et ton hurlement a rempli la terre, parce que le fort a heurté contre le fort et que tous deux sont tombés ensemble.
Mataifa yatasikia juu ya aibu yako, kilio chako kitaijaza dunia. Shujaa mmoja atajikwaa juu ya mwingine, nao wataanguka chini pamoja.”
13 Parole que le Seigneur à dite à Jérémie, le prophète, sur ce que Nabuchodonosor, roi de Babylone, devait venir et frapper la terre d’Egypte.
Huu ndio ujumbe Bwana aliomwambia nabii Yeremia kuhusu kuja kwa Nebukadneza mfalme wa Babeli ili kuishambulia Misri:
14 Annoncez à l’Egypte, et faites entendre à Magdalum votre voix, et qu’elle retentisse à Memphis et à Taphnis; dites: Sois debout, prépare-toi; parce que le glaive dévorera ce qui est autour de toi.
“Tangaza hili katika Misri, nawe ulihubiri katika Migdoli, hubiri pia katika Memfisi na Tahpanhesi: ‘Shikeni nafasi zenu na mwe tayari, kwa kuwa upanga unawala wale wanaokuzunguka.’
15 Pourquoi ton brave s’est-il pourri? il ne s’est pas tenu debout, parce que le Seigneur l’a renversé.
Kwa nini mashujaa wako wamesombwa na kupelekwa mbali? Hawawezi kusimama, kwa maana Bwana atawasukuma awaangushe chini.
16 Il a multiplié ceux qui tombaient, et l’homme est tombé sur son voisin, et ils diront: Lève-toi, et retournons à notre peuple et dans la terre de notre naissance, à cause de l’épée de la colombe.
Watajikwaa mara kwa mara, wataangukiana wao kwa wao. Watasema, ‘Amka, turudi kwa watu wetu na nchi yetu, mbali na upanga wa mtesi.’
17 Appelez le nom de Pharaon, roi d’Egypte: Le temps a amené du tumulte.
Huko watatangaza, ‘Farao mfalme wa Misri ni makelele tu, amekosa wasaa wake.’
18 Je vis, moi (dit le roi dont le nom est le Seigneur des armées); comme le Thabor est parmi les montagnes, et comme le Carmel est sur la mer, ainsi il viendra.
“Kwa hakika kama niishivyo,” asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana Mwenye Nguvu Zote, “mmoja atakuja ambaye ni kama Tabori miongoni mwa milima, kama Karmeli kando ya bahari.
19 Fais tes préparatifs de transmigration, fille habitante de l’Egypte, parce que Memphis deviendra un désert, qu’elle sera abandonnée et inhabitable.
Funga mizigo yako kwenda uhamishoni, wewe ukaaye Misri, kwa kuwa Memfisi utaangamizwa na kuwa magofu pasipo mkazi.
20 C’est une génisse élégante et belle que l’Egypte; celui qui l’aiguillonnera viendra de l’aquilon.
“Misri ni mtamba mzuri, lakini kipanga anakuja dhidi yake kutoka kaskazini.
21 Ses mercenaires aussi qui vivaient au milieu d’elle, comme des veaux engraissés, ont tourné le dos, et ils ont fui tous ensemble, et ils n’ont pu demeurer debout, parce qu’est venu sur eux le jour de leur carnage, le temps de leur visite.
Askari wake waliokodiwa katika safu zake wako kama ndama walionenepeshwa. Wao pia watageuka na kukimbia pamoja, hawataweza kuhimili vita, kwa maana siku ya msiba inakuja juu yao, wakati wao wa kuadhibiwa.
22 Sa voix retentira comme le bruit de l’airain, parce qu’ils marcheront rapidement avec une armée, et qu’avec des haches ils viendront à elle, comme des bûcherons.
Misri atatoa sauti kama ya nyoka anayekimbia kadiri adui anavyowasogelea na majeshi, watakuja dhidi yake wakiwa na mashoka, kama watu wakatao miti.
23 Ils ont coupé par le pied, dit le Seigneur, les arbres de sa forêt, qu’on ne peut compter: ils se sont multipliés plus que les sauterelles, et ils sont sans nombre.
Wataufyeka msitu wake,” asema Bwana, “hata kama umesongamana kiasi gani. Ni wengi kuliko nzige, hawawezi kuhesabika.
24 La fille d’Egypte a été couverte de confusion, et livrée aux mains du peuple de l’aquilon.
Binti wa Misri ataaibishwa, atatiwa mikononi mwa watu wa kaskazini.”
25 Le Seigneur des armées. Dieu d’Israël, a dit: Voici que moi je visiterai le tumulte d’Alexandrie, et Pharaon, et l’Egypte, et ses dieux, et ses rois, et Pharaon, et ceux qui se confient en lui.
Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asema: “Nakaribia kuleta adhabu juu ya Amoni mungu wa Thebesi, na juu ya Farao, Misri na miungu yake, na wafalme wake, pamoja na wale wanaomtegemea Farao.
26 Et je les livrerai à la main de ceux qui cherchent leur âme, à la main de Nabuchodonosor, roi de Babylone, et à la main de ses serviteurs; et après cela elle sera habitée comme dans les jours anciens, dit le Seigneur.
Nitawatia mikononi mwa wale wanaotafuta uhai wao, yaani Nebukadneza mfalme wa Babeli na maafisa wake. Hatimaye, hata hivyo, Misri itakaliwa kama nyakati zilizopita,” asema Bwana.
27 Et toi, ne crains pas, mon serviteur Jacob, et ne t’effraye point, Israël, parce que moi je le sauverai, en te ramenant de loin, et ta race, en la retirant de la terre de ta captivité; et Jacob retournera, et il se reposera, et il prospérera, et il n’y aura personne qui l’épouvante.
“Usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu, usifadhaike, ee Israeli. Hakika nitakuokoa kutoka nchi za mbali, uzao wako kutoka nchi ya uhamisho wao. Yakobo atakuwa tena na amani na salama, wala hakuna hata mmoja atakayewatia hofu.
28 Et toi, ne crains pas, Jacob mon serviteur, dit le Seigneur, parce que moi je suis avec toi, parce que moi je détruirai entièrement toutes les nations chez lesquelles je t’ai jeté; pour toi, je ne te détruirai pas entièrement, mais je te châtierai selon la justice et je ne t’épargnerai pas comme un innocent.
Usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu, kwa maana mimi niko pamoja nawe,” asema Bwana. “Ingawa nitayaangamiza kabisa mataifa yote ambayo miongoni mwake nimekutawanya, sitakuangamiza wewe kabisa. Nitakurudi, lakini kwa haki tu, wala sitakuacha kabisa bila kukuadhibu.”

< Jérémie 46 >