< Sophonie 1 >

1 La parole de l'Éternel, qui fut adressée à Sophonie, fils de Cushi, fils de Guédalia, fils d'Amaria, fils d'Ézéchias, aux jours de Josias, fils d'Amon, roi de Juda.
Hili ni neno la Yahwe ambalo lilikuja kwa Sefania mwana wa Kushi mwana wa Gedalia mwana wa Amaria mwana Hezekia, katika siku za Yosia mwana wa Amoni, mfalme wa Yuda. “
2 Je ferai périr entièrement toutes choses sur la face de la terre, dit l'Éternel.
Nitaangamiza kabisa kila kitu kutoka usoni mwa dunia - hili ni tamko la Bwana mwenyewe.
3 Je ferai périr les hommes et les bêtes; je ferai périr les oiseaux du ciel et les poissons de la mer; j'enlèverai les scandales avec les méchants, et je retrancherai les hommes de la face de la terre, dit l'Éternel.
Nitamwangamiza mtu na mnyama; Nitawaangamiza ndege wa mbinguni na samaki wa baharini, uharibifu pamoja na waovu. Hivyo nitamfutilia mbali mtu kutoka uso wa dunia - hili ni tamko la Bwana mwenyewe.
4 J'étendrai ma main sur Juda et sur tous les habitants de Jérusalem; et je retrancherai de ce lieu le reste de Baal, et le nom de ses prêtres avec les sacrificateurs,
Nitafika kwa mkono wangu juu ya Yuda na wote wenyeji wa Yerusalemu. Nitafutilia mbali kila mabaki ya Baali kutoka sehemu hii na majina ya watu waabuduo sanamu miongoni mwa makuhani,
5 Et ceux qui se prosternent sur les toits devant l'armée des cieux, et ceux qui se prosternent en jurant par l'Éternel, et qui jurent aussi par leur roi,
watu ambao juu ya nyumba huabudu miili ya mbinguni, na watu ambao huabudu na kuapa kwa Yahwe bali ambao pia huapa kwa mfalme wao.
6 Et ceux qui se détournent de l'Éternel, et ceux qui ne cherchent pas l'Éternel et ne s'enquièrent pas de lui.
Nitawafutilia mbali pia wale ambao wamegeuka nyuma kutoka kumfuata Yahwe, wale ambao pia humtafuta Yahwe pasipo kuuliza ulinzi wake.
7 Tais-toi devant le Seigneur, l'Éternel! Car le jour de l'Éternel est proche; l'Éternel a préparé un sacrifice, il a sanctifié ses conviés.
Uwe kimya mbele ya Bwana Yahwe! Kwa kuwa siku ya Yahwe ni karibu, Yahwe ameandaa dhabihu na amewatenga wageni wake.
8 Et au jour du sacrifice de l'Éternel, je châtierai les princes, et les fils du roi, et tous ceux qui revêtent des vêtements étrangers.
“Itakuja katika siku ya dhabihu ya Bwana, hivyo nitawapiga wakuu na wana wa mfalme, na kila mmoja aliyevikwa mavazi ya kigeni.
9 Et je châtierai, en ce jour-là, tous ceux qui sautent par-dessus le seuil, ceux qui remplissent la maison de leur Seigneur de violence et de fraude.
Katika siku hiyo nitawapiga wote wale ambao huruka juu ya kizingiti, wale ambao hujaza nyumba ya bwana wao kwa vurugu na udanganyifu.
10 En ce jour-là, dit l'Éternel, on entendra des cris à la porte des Poissons, des hurlements dans la seconde partie de la ville, et un grand désastre sur les collines.
Itakuwa katika siku ile - hili ni tangazo la Yahwe - kwamba kilio cha huzuni kitakuja kutoka kwenye mlango wa samaki, ikipiga yowe kutoka Wilaya ya Pili, na sauti ya kishindo kikuu kutoka vilimani.
11 Lamentez-vous, habitants de Macthesh! Car tous ceux qui trafiquent sont détruits, tous ces gens chargés d'argent sont exterminés!
Pigeni yowe, wenyeji wa Soko la Wilaya, kwa wote wafanyabiashara watakuwa wameharibiwa, wote wale ambao hupima fedha watakuwa wamefutiliwa mbali.
12 Et il arrivera, en ce temps-là, que je fouillerai Jérusalem avec des lampes, et que je châtierai ces hommes qui se figent sur leurs lies, et qui disent dans leur cœur: L'Éternel ne fera ni bien ni mal.
Itakuwa katika siku ile nitaitafuta Yerusalemu kwa taa na kuwapiga wanaume ambao watakuwa wamekaa kwenye mvinyo wao na kusema mioyoni mwao, 'Yahwe hatafanya chochote, ama kizuri au kiovu.'.
13 Leurs biens seront au pillage, et leurs maisons en désolation; ils auront bâti des maisons, mais ils n'y habiteront point; ils auront planté des vignes, mais ils n'en boiront pas le vin.
Mali zao zitakuja kuporwa, na nyumba zao zitakuwa zimetelekezwa kwa maangamizi! Watajenga nyumba lakini hawataishi humo, na kupanda mizabibu lakini hawatakunywa mvinyo wake.
14 Le grand jour de l'Éternel est proche; il est proche, et vient en toute hâte. La voix du jour de l'Éternel retentit; là l'homme vaillant lui-même pousse des cris amers.
Siku kubwa ya Yahwe ni karibu, karibu na inaharakisha upesi! Sauti ya siku ya Yahwe itakuwa ya kilio cha uchungu wa kishujaa!
15 C'est un jour de colère que ce jour-là; un jour de détresse et d'angoisse, un jour de ruine et de désolation, un jour de ténèbres et d'obscurité, un jour de nuées et de brouillards,
Siku hiyo itakuwa siku ya ghadabu, siku ya huzuni na uchungu, siku ya dhoruba na maangamizi, siku ya giza na utusitusi, siku ya mawingu na giza nene.
16 Un jour de trompettes et d'alarmes contre les villes fortes et contre les hautes tours.
Itakuwa siku ya parapanda na kengele dhidi ya ngome mijini na buruji ndefu.
17 Je mettrai les hommes dans la détresse, et ils marcheront comme des aveugles, parce qu'ils ont péché contre l'Éternel. Leur sang sera répandu comme de la poussière, et leur chair comme de l'ordure.
Hivyo nitaleta dhiki juu ya wanadamu, kwa hiyo watatembea karibu kama wanaume vipofu tangu walipofanya dhambi dhidi ya Yahwe. Damu yao itamwagwa kama vumbi, na sehemu zao za ndani kama kinyesi.
18 Ni leur argent, ni leur or ne pourront les délivrer au jour de la colère de l'Éternel; et par le feu de sa jalousie tout le pays sera consumé; car c'est d'une entière destruction, c'est d'une ruine soudaine qu'il frappera tous les habitants de la terre.
Wala fedha zao wala dhahabu zao hazitaweza kuwaokoa juu ya ghadhabu ya Yahwe. Ndani ya moto wa wivu wake dunia yote itateketezwa, hivyo ataleta ukamilifu, miwisho wa kutisha kwa wote wakaao duniani.”

< Sophonie 1 >