< Sophonie 2 >

1 Recueillez-vous, recueillez-vous, nation sans pudeur!
Kusanyikeni pamoja ninyi wenyewe mkutano wa hadhara na kusanyikeni, taifa lisilokuwa na aibu -
2 Avant que le décret enfante, et que le jour passe comme la balle; avant que l'ardeur de la colère de l'Éternel vienne sur vous, avant que le jour de la colère de l'Éternel vienne sur vous!
kabla amri kuchukua madhara na siku hiyo kupita kama makapi, kabla hasira kali ya ghadhabu ya Yahwe kuja juu yenu, kabla siku ya ghadhabu ya Bwana kuja juu yenu.
3 Cherchez l'Éternel, vous tous les humbles du pays, qui faites ce qu'il ordonne! Recherchez la justice, recherchez la débonnaireté! Peut-être serez-vous mis à couvert, au jour de la colère de l'Éternel.
Mtafuteni Yahwe, ninyi watu wote wanyenyekevu duniani mnaozitii amri zake! Tafuteni haki yake. Tafuteni unyenyekevu, na labda mtalindwa katika siku ya ghadhabu ya Yahwe.
4 Car Gaza sera abandonnée, et Askélon sera en désolation; on chassera Asdod en plein midi, et Ékron sera renversée.
hivyo Gaza utatelekezwa, na Ashkeloni utageuka kuwa uharibifu. Watauondoshea mbali Ashdodi wakati wa mchana, na wataung'oa Ekroni!
5 Malheur aux habitants de la région maritime, à la nation des Kéréthiens! La parole de l'Éternel est contre vous, Canaan, terre des Philistins! Je te détruirai, jusqu'à n'avoir plus d'habitants.
Ole kwa wanaokaa kando ya bahari, taifa la Wakerethi! Yahwe amesema dhidi yenu, Kanaani, nchi ya Wafilisiti. Nitawaangamiza hakuna mkazi atakayebakia.
6 Et la région maritime ne sera plus que des pâturages, des loges de bergers et des parcs de brebis.
Hiyo nchi ya kando ya bahari itakuwa malisho kwa wachungaji na kwa mazizi ya kondoo.
7 Et ce sera une région pour les restes de la maison de Juda, et ils y paîtront; le soir ils reposeront dans les maisons d'Askélon, car l'Éternel leur Dieu les visitera, et ramènera leurs captifs.
Nchi ya kando ya bahari itakuwa mali ya mabaki ya watu wa nyumba ya Yuda, watakaochungia makundi yao huko. Watu wao watalala jioni katika nyumba ya Ashikeloni, kwa kuwa Yahwe Mungu wao atawatunza na kurejesha wafungwa wao.
8 J'ai entendu les insultes de Moab et les outrages des enfants d'Ammon, qui ont insulté mon peuple, et se sont insolemment élevés contre ses frontières.
Nilizisikia dhihaka za Moabu na wakiwatukana watu wa Amoni wakati walipowadhihaki watu wangu na kujitukuza mipakani mwao.
9 C'est pourquoi, je suis vivant! dit l'Éternel des armées, le Dieu d'Israël, Moab sera comme Sodome, et les enfants d'Ammon comme Gomorrhe, un domaine couvert d'orties, une mine de sel, une désolation à jamais; le reste de mon peuple les pillera, et le résidu de ma nation les possédera.
Kwa hiyo, kama ninavyoishi - hili ni tamko la Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, - Moabu itakuja kuwa kama Sodoma, na watu wa Amoni kama Gomora; mahali pa viwavi na shimo la chumvi, jangwa la daima. Lakini watu wangu waliosalia watawateka mateka, na watu wa taifa langu waliobaki watachukua umiliki wao.'
10 C'est là ce qu'ils auront pour leur orgueil, parce qu'ils ont insulté et bravé le peuple de l'Éternel des armées.
Hili litatokea kwa Moabu na Amoni kwa sababu ya kiburi chao, tangu walipowadhihaki na kuwatukana watu wa Yahwe wa majeshi.
11 L'Éternel sera terrible contre eux; car il anéantira tous les dieux de la terre, et chacun se prosternera devant lui dans son pays, et même toutes les îles des nations.
Ndipo watamwogopa Yahwe, kwa kuwa ataidhihaki miungu yote ya dunia. Kila mmoja atamwabudu yeye, kila mmoja kutoka mahali pake, kutoka kila upande wa pwani.
12 Vous aussi, Cushites, vous serez frappés par mon épée.
Ninyi Wakushi pia mtakufa kwa upanga wangu,
13 Il étendra sa main vers le nord, et il détruira l'Assyrie; il fera de Ninive une désolation, un lieu aride comme le désert.
na mkono wa Mungu utaishambulia kaskazini na kuiangamiza Ashuru, Kwa hiyo Ninawi utatelekezwa kwa kuteketezwa, kuwa pakavu kama jangwa.
14 Les troupeaux se coucheront au milieu d'elle, des bêtes de toute espèce, en foule; le pélican et le hérisson logeront parmi ses chapiteaux; leur cri retentira aux fenêtres; la dévastation sera sur le seuil, et les lambris de cèdre seront arrachés.
Ndipo makundi ya wanyama yatalala pale, kila mnyama wa mataifa, wote kirukanjia na nungunungu watapumzika juu ya safu zao. Sauti itasikika kutoka madirishani; kifusi kitakuwa milangoni; nakshi za mwerezi wao mihimili itakuwa imeifunua.
15 C'est là cette ville joyeuse qui vivait dans la sécurité, qui disait en son cœur: Moi, et nulle autre que moi! Comment est-elle devenue un désert, un gîte pour les bêtes? Quiconque passera près d'elle, sifflera et agitera la main
huu ni mji wa kushangiliwa ambao umekaa pasipo hofu, ambaye husema moyoni mwake, “Mimi niko, na hakuna mwingine wa kufanana na Mimi”. Kwa namna ulivyokuwa wa kutisha, mahali pa kulala wanyama ndani yake. Kila mmoja ambaye hupitia kwake huuhisia na kutingisha ngumi kwake.

< Sophonie 2 >