< Psaumes 88 >

1 Éternel, Dieu de ma délivrance, je crie jour et nuit devant toi.
Yahwe, Mungu wa wokovu wangu, ninalia mchana na usiku mbele zako.
2 Que ma prière parvienne en ta présence; incline ton oreille à mon cri.
Sikiliza maombi yangu; utazame kulia kwangu.
3 Car mon âme est rassasiée de maux, et ma vie touche au séjour des morts. (Sheol h7585)
Maana nimejawa taabu, na uhai wangu umefika kuzimuni. (Sheol h7585)
4 Je suis compté parmi ceux qui descendent dans la fosse; je suis comme un homme sans vigueur,
Watu hunichukulia kama wale waendao chini shimoni; mimi ni mtu asiye na nguvu.
5 Gisant parmi les morts, tel que les blessés à mort, qui sont couchés dans le tombeau, dont tu ne te souviens plus, et qui sont séparés de ta main.
Nimetelekezwa miongoni mwa wafu; niko kama mfu alalaye katika kaburi, wao ambao wewe huwajari tena kwa sababu wametengwa mbali na nguvu zako.
6 Tu m'as mis dans la fosse la plus basse, dans les lieux ténébreux, dans les abîmes.
Wewe umeniweka katika sehemu ya chini kabisa ya shimo, sehemu yenye giza na kilindini.
7 Ta colère pèse sur moi, et tu m'accables de tous tes flots. (Sélah)
Gadhabu yako yanielemea, na mawimbi yako yote yanatua juu yangu. (Selah)
8 Tu as éloigné de moi ceux que je connais; tu m'as rendu pour eux un objet d'horreur; je suis enfermé et je ne puis sortir.
Kwa sababu yako, wale wanijuao wote hunikwepa. Umenifanya wakutisha machoni pao. Nimefungwa na siwezi kutoroka.
9 Mon œil se consume par l'affliction; je t'invoque, ô Éternel, tous les jours; j'étends mes mains vers toi.
Macho yangu yamefifia kutokana na shida; kila siku nakuita wewe, Yahwe; ninakunyoshea wewe mikono yangu.
10 Feras-tu quelque merveille pour les morts? Ou les trépassés se lèveront-ils pour te louer? (Sélah)
Je! utafanya miujiza kwa ajili ya wafu? Wale waliokufa watafufuka na kukusifu wewe? (Selah)
11 Annoncera-t-on ta bonté dans le tombeau, et ta fidélité dans l'abîme?
Uaminifu wa agano lako utatangazwa kaburini? au uaminifu wako mahali pa wafu?
12 Connaîtra-t-on tes merveilles dans les ténèbres, et ta justice dans la terre d'oubli?
Matendo yako ya ajabu yatajulikana gizani? au haki yako katika mahali pa usahaulifu?
13 Et moi, Éternel, je crie à toi; ma prière te prévient dès le matin.
Lakini ninakulilia wewe, Yahwe; wakati wa asubuhi maombi yangu huja kwako.
14 Éternel, pourquoi rejettes-tu mon âme, et me caches-tu ta face?
Yahwe, kwa nini unanikataa? Kwa nini unauficha uso wako mbali nami?
15 Je suis affligé et comme expirant dès ma jeunesse; je suis chargé de tes terreurs, je suis éperdu.
Nimekuwa nikiteswa kila siku na hatihati ya kifo tangu ujana wangu. Nimeteseka dhidi ya hofu yako kuu; ninakata tamaa.
16 Tes fureurs ont passé sur moi; tes épouvantes me tuent.
Matendo yako ya hasira yamepita juu yangu, na matendo yako ya kutisha yameniangamiza.
17 Elles m'environnent comme des eaux chaque jour; elles m'enveloppent toutes à la fois.
Siku zote yananizingira mimi kama maji; yote yamenizunguka mimi.
18 Tu as éloigné de moi amis et compagnons; ceux que je connais, ce sont les ténèbres.
Wewe umemuondoa kwangu kila rafiki na anijuaye. Na sasa anijuaye pekee ni giza.

< Psaumes 88 >