< Job 18 >

1 Alors Bildad, de Shuach, prit la parole et dit:
Ndipo Bildadi Mshuhi alijibu na kusema, “
2 Quand finirez-vous ces discours? Ayez du bon sens, et ensuite parlons.
Je, lini utaacha kusema kwako? Fikiri, na baadaye tutazungumza.
3 Pourquoi sommes-nous regardés comme des bêtes, et sommes-nous stupides à vos yeux?
Kwa nini sisi tumehesabiwa kama wanyama mwitu; kwa nini tumekuwa wapumbavu machoni pako?
4 O toi qui te déchires toi-même dans ta fureur, la terre sera-t-elle abandonnée à cause de toi, et le rocher sera-t-il transporté hors de sa place?
Wewe ambaye wajirarua mwenyewe katika hasira yako, nchi haipaswi kuachwa kwa ajili yako au miamba inapaswa kuondolewa kutoka mahali pake?
5 Oui, la lumière du méchant s'éteindra, et la flamme de son feu ne brillera pas.
Ni dhahiri, nuru ya watu waovu itawekwa nje; cheche ya moto wake haitanga'ra.
6 La lumière s'obscurcira dans sa tente, et la lampe s'éteindra au-dessus de lui.
Nuru itakuwa giza katika hema yake; taa yake juu yake yeye itawekwa nje.
7 Ses pas si puissants seront restreints, et son propre conseil le renversera.
Hatua za nguvu zake yeye zitafanywa kuwa fupi; mipango yake yeye mwenyewe itamwangusha yeye chini.
8 Car il sera pris dans les filets par ses pieds, et il marchera sur le piège.
Kwa maana yeye atatupwa katika mtego kwa miguu yake mwenyewe; yeye atatembea katika mahangaiko.
9 Le lacet le tiendra par le talon, et le filet le saisira:
Tanzi litamchukua yeye kwa kisigino; mtego utabaki kushikilia juu yake.
10 Une corde est cachée pour lui sous terre, et une trappe sur son sentier.
Tanzi limefichwa kwa ajili yake chini ya ardhi; na mtego kwa ajili yake katika njia.
11 De tous côtés des terreurs l'assiégeront, et feront courir ses pieds çà et là.
Watishao watamfanya yeye aogope juu ya sehemu zote; wao watamkimbiza yeye kwenye visigino vyake.
12 Sa vigueur sera affamée; la calamité se tiendra prête à ses côtés.
Utajiri wake utageuka kuwa njaa, na majanga yatakuwa tayari upande wake.
13 Il dévorera les membres de son corps, il dévorera ses membres, le premier-né de la mort!
Sehemu za mwili wake zitakuwa zimemezwa; Hakika, mzaliwa wa kwanza wa kifo atazila sehemu zake yeye.
14 On l'arrachera de sa tente, objet de sa confiance; on l'amènera au roi des épouvantements.
Yeye ameraruliwa kutoka kwenye usalama wa hema yake na hakuweza kutembea kwenda kwa mfalme mwenye utisho.
15 On habitera dans sa tente, qui ne sera plus à lui; le soufre sera répandu sur sa demeure.
Watu ambao siyo wa kwake wataishi kwenye hema yake baada ya kuona ule moto mesambaa ndani ya nyumba yake yeye.
16 En bas ses racines sécheront, et en haut ses branches seront coupées.
Mizizi yake itanyauka chini yake; juu tawi lake yeye litakatwa.
17 Sa mémoire disparaîtra de la terre, et on ne prononcera plus son nom sur les places.
Kumbukumbu lake yeye litapotea kutoka katika nchi; yeye hatakuwa na jina katika mtaa.
18 On le chassera de la lumière dans les ténèbres, et on le bannira du monde.
Yeye atafukuzwa kutoka katika nuru mpaka kwenye giza na kuwa amefukuzwa nje na ulimwengu huu.
19 Il n'aura ni lignée, ni descendance au milieu de son peuple, ni survivant dans ses habitations.
Hatakuwa na mtoto wa kiume wala mjukuu miongonni mwa watu wake, wala kizazi chochote kitakachobakia mahali alipokuwa amekaa.
20 Ceux d'Occident seront stupéfaits du jour de sa ruine, et ceux d'Orient en seront saisis d'horreur.
Wale wanaoishi upande wa magharibi watakuwa wametiwa hofu kwa kile kitakachotokea kwake siku moja; wale wanaoishi upande wa mashariki watakuwa wameogopeshwa kwa hicho.
21 Tel est le sort de l'injuste. Telle est la destinée de celui qui ne connaît pas Dieu.
Hakika hizo ni nyumba za watu wasio haki, ni sehemu ya wale wasiomjua Mungu.”

< Job 18 >