< Jérémie 26 >

1 Au commencement du règne de Jéhojakim, fils de Josias, Roi de Juda, cette parole fut [adressée] à Jérémie par l'Eternel, en disant:
Mwanzoni mwa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, neno hili lilikuja kutoka kwa Bwana:
2 Ainsi a dit l'Eternel: tiens-toi debout au parvis de la maison de l'Eternel, et prononce à toutes les villes de Juda qui viennent pour se prosterner dans la maison de l'Eternel, toutes les paroles que je t'ai commandé de leur prononcer; n'en retranche pas une parole.
“Hili ndilo Bwana asemalo: Simama katika ua wa nyumba ya Bwana na useme na watu wote wa miji ya Yuda wanaokuja kuabudu katika nyumba ya Bwana. Waambie kila kitu nitakachokuamuru, usipunguze neno.
3 Peut-être qu'ils écouteront, et qu'ils se détourneront chacun de son mauvais train; et je me repentirai du mal que je pense de leur faire à cause de la malice de leurs actions.
Huenda watasikiliza, na kila mmoja akageuka kutoka njia yake mbaya. Kisha nitawahurumia na kuacha kuwaletea maafa niliyokuwa ninapanga kwa sababu ya maovu waliyofanya.
4 Tu leur diras donc: ainsi a dit l'Eternel: si vous ne m'écoutez point pour marcher dans ma Loi, laquelle je vous ai proposée,
Waambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ikiwa hamtanisikiliza na kuifuata sheria yangu ambayo nimeiweka mbele yenu,
5 Pour obéir aux paroles des Prophètes mes serviteurs que je vous envoie, me levant dès le matin, et [les] envoyant, lesquels vous n'avez point écoutés:
nanyi ikiwa hamtayasikiliza maneno ya watumishi wangu manabii, ambao nimewatuma kwenu tena na tena (ijapokuwa hamkuwasikiliza),
6 Je mettrai cette maison en même état que Silo, et je livrerai cette ville en malédiction à toutes les nations de la terre.
ndipo nitaifanya nyumba hii kama Shilo na mji huu kuwa kitu cha kulaaniwa na mataifa yote ya dunia.’”
7 Or les Sacrificateurs et les Prophètes, et tout le peuple entendirent Jérémie prononçant ces paroles dans la maison de l'Eternel.
Makuhani, manabii na watu wote wakamsikia Yeremia akiyasema maneno haya ndani ya nyumba ya Bwana.
8 Et il arriva qu'aussitôt que Jérémie eut achevé de prononcer tout ce que l'Eternel lui avait commandé de prononcer à tout le peuple, les Sacrificateurs et les Prophètes et tout le peuple le saisirent, en disant: tu mourras de mort.
Lakini mara tu Yeremia alipomaliza kuwaambia watu kila kitu Bwana alichomwamuru kukisema, basi makuhani, manabii na watu wote walimkamata wakisema, “Ni lazima ufe!
9 Pourquoi as-tu prophétisé au Nom de l'Eternel, disant: cette maison sera comme Silo, et cette ville sera déserte, tellement que personne n'y habitera? Et tout le peuple s'assembla vers Jérémie dans la maison de l'Eternel.
Kwa nini unatoa unabii katika jina la Bwana kwamba nyumba hii itakuwa kama Shilo na mji huu utakuwa ukiwa na kuachwa tupu?” Nao watu wote wakamkusanyikia na kumzunguka Yeremia ndani ya nyumba ya Bwana.
10 Et les principaux de Juda ayant ouï toutes ces choses montèrent de la maison du Roi à la maison de l'Eternel, et s'assirent à l'entrée de la porte neuve de la maison de l'Eternel.
Maafisa wa Yuda waliposikia kuhusu mambo haya, wakapanda kutoka jumba la kifalme, wakaenda katika nyumba ya Bwana na kushika nafasi zao kwenye ingilio la Lango Jipya la nyumba ya Bwana.
11 Et les Sacrificateurs et les Prophètes parlèrent aux principaux, et à tout le peuple, en disant: cet homme mérite d'être condamné à la mort, car il a prophétisé contre cette ville, comme vous l'avez entendu de vos oreilles.
Kisha makuhani na manabii wakawaambia maafisa pamoja na watu wote, “Mtu huyu anastahili ahukumiwe kifo kwa sababu ametoa unabii mbaya dhidi ya mji huu. Mmesikia kwa masikio yenu wenyewe!”
12 Et Jérémie parla à tous les principaux, et à tout le peuple, en disant: l'Eternel m'a envoyé pour prophétiser contre cette maison, et contre cette ville, [selon] toutes les paroles que vous avez ouïes.
Kisha Yeremia akawaambia maafisa wote na watu wote: “Bwana amenituma kutoa unabii dhidi ya nyumba hii na mji huu mambo yote mliyoyasikia.
13 Maintenant donc, corrigez votre conduite et vos actions; et écoutez la voix de l'Eternel votre Dieu, et l'Eternel se repentira du mal qu'il a prononcé contre vous.
Sasa tengenezeni njia zenu na matendo yenu, na kumtii Bwana Mungu wenu. Ndipo Bwana atawahurumia na kuacha kuleta maafa aliyokuwa ameyatamka dhidi yenu.
14 Pour moi, me voici entre vos mains, faites de moi comme il vous semblera bon et juste.
Lakini kwa habari yangu mimi, niko mikononi mwenu, nifanyieni lolote mnaloona kuwa ni jema na la haki.
15 Mais sachez comme une chose certaine, que si vous me faites mourir, vous mettrez du sang innocent sur vous, et sur cette ville, et sur ses habitants; car en vérité l'Eternel m'a envoyé vers vous, afin de prononcer toutes ces paroles, vous l'entendant.
Hata hivyo, jueni kwa hakika, ikiwa mtaniua, mtakuwa mmejipatia dhambi kwa damu isiyo na hatia juu yenu wenyewe, na juu ya mji huu na wote wanaoishi ndani yake, kwa maana ni kweli Bwana amenituma kwenu ili niseme maneno haya yote masikioni mwenu.”
16 Alors les principaux et tout le peuple dirent aux Sacrificateurs et aux Prophètes: cet homme ne mérite pas d'être condamné à la mort; car il nous a parlé au Nom de l'Eternel notre Dieu.
Kisha maafisa na watu wote wakawaambia makuhani na manabii, “Mtu huyu asihukumiwe kifo! Amesema nasi katika jina la Bwana, Mungu wetu.”
17 Et quelques-uns des Anciens du pays se levèrent, et parlèrent à toute l'assemblée du peuple, en disant:
Baadhi ya wazee wa nchi wakasogea mbele, wakaliambia kusanyiko lote la watu,
18 Michée Morastite a prophétisé aux jours d'Ezéchias Roi de Juda, et a parlé à tout le peuple de Juda, en disant: ainsi a dit l'Eternel des armées, Sion sera labourée [comme] un champ, et Jérusalem sera réduite en monceaux de pierres, et la montagne du Temple en de hauts lieux d'une forêt.
“Mika Mmoreshethi alitoa unabii katika siku za Hezekia mfalme wa Yuda. Akawaambia watu wote wa Yuda, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “‘Sayuni italimwa kama shamba, Yerusalemu itakuwa lundo la kokoto, na kilima cha Hekalu kitakuwa kichuguu kilichofunikwa na vichaka.’
19 Ezéchias le Roi de Juda, et tous ceux de Juda le firent-ils mourir? Ne craignit-il pas l'Eternel, et ne supplia-t-il pas l'Eternel? et l'Eternel se repentit du mal qu'il avait prononcé contre eux; nous faisons donc un grand mal contre nos âmes.
Je, Hezekia mfalme wa Yuda au mtu mwingine yeyote katika Yuda alimhukumu Mika kufa? Je, Hezekia hakumcha Bwana na kuhitaji msaada wake? Je, Bwana hakuwahurumia na akaacha kuleta maafa aliyokuwa ametamka dhidi yao? Tunakaribia sana kujiletea maangamizo ya kutisha sisi wenyewe!”
20 Mais aussi, [dirent les autres], il y eut un homme qui prophétisa au Nom de l'Eternel, [savoir] Urie, fils de Sémahia, de Kiriath-jéharim, lequel ayant prophétisé contre cette même ville, et contre ce même pays, en la même manière que Jérémie;
(Wakati huu, Uria mwana wa Shemaya kutoka mji wa Kiriath-Yearimu alikuwa mtu mwingine aliyetoa unabii kwa jina la Bwana. Alitoa unabii juu ya mambo yaliyofanana na haya dhidi ya mji huu na nchi hii kama alivyofanya Yeremia.
21 Et le Roi Jéhojakim, avec tous ses officiers, et les principaux ayant entendu ses paroles, le Roi chercha à le faire mourir; mais Urie l'ayant appris, et ayant craint, s'enfuit, et se retira en Egypte.
Mfalme Yehoyakimu na wakuu wake wote na maafisa waliposikia maneno yake, mfalme alitafuta kumuua. Lakini Uria alipata habari, na kwa kuogopa akakimbilia Misri.
22 Et le Roi Jéhojakim envoya des hommes en Egypte, [savoir] Elnathan, fils de Hacbor, et quelques gens avec lui, qui allèrent en Egypte,
Hata hivyo, Mfalme Yehoyakimu alimtuma Elnathani mwana wa Akbori huko Misri, pamoja na watu wengine ili kwenda kumkamata Uria.
23 Et qui firent revenir Urie d'Egypte, et l'amenèrent au Roi Jéhojakim, qui le frappa avec l'épée, et jeta son corps mort aux sépulcres du peuple.
Wakamrudisha Uria kutoka Misri na kumpeleka kwa Mfalme Yehoyakimu, ambaye alimuua kwa upanga, na mwili wake kutupwa kwenye eneo la makaburi ya watu wasio na cheo.)
24 Toutefois la main d'Ahikam fils de Saphan fut pour Jérémie, afin qu'on ne le livrât point entre les mains du peuple, pour le faire mourir.
Zaidi ya hayo, Ahikamu mwana wa Shafani akamuunga mkono Yeremia, kwa hiyo hakutiwa tena mikononi mwa watu ili auawe.

< Jérémie 26 >