< Jérémie 42 >

1 Alors tous les Capitaines des gens de guerre, et Johanan fils de Karéah, et Jézania fils de Hosahia, et tout le peuple, depuis le plus petit jusqu’au plus grand, s'approchèrent,
Ndipo maafisa wote wa jeshi, pamoja na Yohanani mwana wa Karea, na Yezania mwana wa Hoshaya, na watu wote kuanzia aliye mdogo kabisa hadi aliye mkuu sana wakamjia
2 Et dirent à Jérémie le Prophète: que notre supplication soit reçue de toi, et fais requête à l'Eternel ton Dieu pour nous, [savoir] pour tout ce reste-ci; car de beaucoup [de monde que nous étions] nous sommes restés peu, comme tes yeux nous voient;
Yeremia nabii na kumwambia, “Tafadhali sikia maombi yetu na umwombe Bwana Mungu wako kwa ajili ya watu hawa wote waliosalia. Kwa kuwa kama unavyoona sasa, ingawa wakati fulani tulikuwa wengi, sasa tumesalia wachache tu.
3 Et que l'Eternel ton Dieu nous déclare le chemin par lequel nous aurons à marcher, et ce que nous avons à faire.
Omba ili Bwana Mungu wako atuambie twende wapi na tufanye nini.”
4 Et Jérémie le Prophète leur répondit: J'ai entendu [votre demande]; voici, je m'en vais faire requête à l'Eternel votre Dieu selon vos paroles; et il arrivera que je vous déclarerai tout ce que l'Eternel vous répondra, et je ne vous en cacherai pas un mot.
Nabii Yeremia akajibu, “Nimewasikia. Kwa hakika nitamwomba Bwana Mungu wenu kama mlivyoomba. Nitawaambia kila kitu asemacho Bwana, wala sitawaficha chochote.”
5 Et ils dirent à Jérémie: l'Eternel soit pour témoin véritable et fidèle entre nous, si nous ne faisons selon toutes les paroles, pour lesquelles l'Eternel ton Dieu t'aura envoyé vers nous.
Kisha wakamwambia Yeremia, “Bwana na awe shahidi wa kweli na mwaminifu kati yetu kama hatutafanya sawasawa na kila kitu Bwana Mungu wako atakachokutuma utuambie.
6 Soit bien, soit mal, nous obéirons à la voix de l'Eternel notre Dieu, vers lequel nous t'envoyons; afin qu'il nous arrive du bien quand nous aurons obéi à la voix de l'Eternel notre Dieu.
Likiwa jema au likiwa baya, tutamtii Bwana Mungu wetu, ambaye tunakutuma kwake, ili mambo yote yawe mema kwetu, kwa maana tutamtii Bwana Mungu wetu.”
7 Et il arriva au bout de dix jours que la parole de l'Eternel fut [adressée] à Jérémie.
Baada ya siku kumi, neno la Bwana likamjia Yeremia.
8 Et il appela Johanan fils de Karéah, et tous les Capitaines des gens de guerre qui étaient avec lui, et tout le peuple, depuis le plus petit jusqu'au plus grand;
Kwa hiyo akawaita pamoja Yohanani mwana wa Karea, na maafisa wote wa jeshi waliokuwa pamoja naye na watu wote kuanzia mdogo kabisa hadi aliye mkuu sana.
9 Et leur dit: Ainsi a dit l'Eternel, le Dieu d'Israël, vers lequel vous m'avez envoyé pour présenter votre supplication devant lui.
Akawaambia, “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye mlinituma kuwasilisha maombi yenu:
10 Si vous continuez à demeurer dans ce pays, je vous rétablirai, et je ne vous détruirai point; je vous [y] planterai, et je ne vous arracherai point, car je me suis repenti du mal que je vous ai fait.
‘Kama mkikaa katika nchi hii, nitawajenga wala sitawabomoa, nitawapanda wala sitawangʼoa, kwani ninahuzunishwa na maafa niliyowapiga nayo.
11 N'ayez point peur du Roi de Babylone, duquel vous avez peur; n'en ayez point peur, dit l'Eternel, car je suis avec vous pour vous sauver, et pour vous délivrer de sa main.
Msimwogope mfalme wa Babeli, ambaye sasa mnamwogopa. Msimwogope, asema Bwana, kwa kuwa niko pamoja nanyi, nami nitawaokoa na kuwaponya kutoka mikononi mwake.
12 Même je vous ferai obtenir miséricorde, tellement qu'il aura pitié de vous, et vous fera retourner en votre pays.
Nitawaonea huruma ili naye awe na huruma nanyi na kuwarudisha katika nchi yenu.’
13 Que si vous dites: nous ne demeurerons point en ce pays, et nous n'écouterons point la voix de l'Eternel notre Dieu;
“Hata hivyo, kama mkisema, ‘Hatutakaa katika nchi hii,’ hivyo mkaacha kumtii Bwana Mungu wenu,
14 En disant: non; mais nous irons au pays d'Egypte, afin que nous ne voyions point de guerre, et que nous n'entendions point le son de la trompette, et que nous n'ayons point disette de pain; et nous demeurerons là.
nanyi kama mkisema, ‘Hapana, tutakwenda kuishi Misri, mahali ambapo hatutaona vita au kusikia sauti ya tarumbeta au kuwa na njaa ya chakula,’
15 A cause de cela écoutez maintenant la parole de l'Eternel, [vous] les restes de Juda. Ainsi a dit l'Eternel des armées, le Dieu d'Israël: si vous vous préparez pour aller en Egypte, et que vous y entriez pour y séjourner;
basi sikieni neno la Bwana, enyi mabaki ya Yuda. Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Ikiwa mmekusudia kwenda Misri na kufanya makazi huko,
16 Il arrivera que l'épée dont vous avez peur vous attrapera là au pays d'Egypte; et la famine que vous craignez si fort vous suivra en Egypte, tellement que vous y mourrez.
basi ule upanga mnaouogopa utawapata huko, na njaa mnayoihofia itawafuata huko Misri, nanyi mtafia huko.
17 Et il arrivera que tous les hommes qui auront fait les démarches nécessaires pour entrer en Egypte afin d'y séjourner, mourront par l'épée, par la famine, et par la mortalité; nul d'eux ne restera, ni échappera de devant le mal que je m'en vais faire venir sur eux.
Naam, wote waliokusudia kwenda kuishi Misri watakufa kwa upanga, njaa na tauni; hakuna hata mmoja wao atakayenusurika au kuokoka maafa nitakayoyaleta juu yao.’
18 Car ainsi a dit l'Eternel des armées, le Dieu d'Israël: comme ma colère et ma fureur a fondu sur les habitants de Jérusalem, ainsi ma fureur fondra sur vous, quand vous serez entrés en Egypte; et vous serez en exécration, et en étonnement, et en malédiction, et en opprobre; et vous ne verrez plus ce lieu-ci.
Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Kama vile hasira yangu na ghadhabu yangu ilivyomwagwa juu ya wale walioishi Yerusalemu, ndivyo ghadhabu yangu itakavyomwagwa juu yenu mtakapokwenda Misri. Mtakuwa kitu cha kulaania na cha kutisha, cha kulaumia na cha kushutumia, nanyi kamwe hamtaona mahali hapa tena.’
19 Vous, les restes de Juda, l'Eternel a parlé contre vous: n'entrez point en Egypte, vous sentirez certainement que je vous en ai sommés aujourd'hui.
“Enyi mabaki ya Yuda, Bwana amewaambia, ‘Msiende Misri.’ Hakikisheni jambo hili: Ninawaonya leo
20 Car vous avez usé de fraude contre vous-mêmes quand vous m'avez envoyé vers l'Eternel votre Dieu, en me disant: fais requête pour nous envers l'Eternel notre Dieu, et nous déclare tout ce que l'Eternel notre Dieu te dira, et nous [le] ferons.
kwamba mmefanya kosa kubwa mioyoni mwenu mliponituma kwa Bwana Mungu wenu na kusema, ‘Mwombe Bwana Mungu wetu kwa ajili yetu, nawe utuambie kila kitu atakachosema, nasi tutafanya.’
21 Et je vous [l']ai déclaré aujourd'hui; mais vous n'avez point écouté la voix de l'Eternel votre Dieu, ni rien de tout ce pour quoi il m'a envoyé vers vous.
Nimewaambieni leo, lakini bado ninyi hamtaki kumtii Bwana Mungu wenu katika yote aliyonituma niwaambie.
22 Maintenant donc sachez certainement que vous mourrez par l'épée, par la famine, et par la mortalité, au lieu auquel vous avez désiré d'entrer, pour y séjourner.
Basi sasa, hakikisheni jambo hili: Mtakufa kwa upanga, njaa na tauni mahali ambapo mnataka kwenda kuishi.”

< Jérémie 42 >