< Néhémie 5 >

1 Et il y eut un grand cri du peuple et de leurs femmes, contre les Juifs leurs frères.
Kisha wale wanaume na wake zao wakalia kwa nguvu dhidi ya Wayahudi wenzao.
2 Et les uns disaient: Nous sommes en grand nombre avec nos fils et nos filles, vendons-en; puis nous achèterons du blé, et nous mangerons, et nous vivrons.
Kwa maana kulikuwa na baadhi ya watu ambao walisema, “Sisi na wana wetu na binti zetu tupo wengi. Basi hebu tupate nafaka tuweze kula na tukae tuishi.”
3 Et d'autres disaient: Engageons nos champs, nos vignes, nos maisons; puis, nous achèterons du blé, et nous mangerons.
Pia kulikuwa na baadhi ya watu ambao walisema, “Tunaweka rehani mashamba yetu, mizabibu yetu, na nyumba zetu ili tupate nafaka wakati wa njaa.”
4 D'autres encore disaient: Nous avons emprunté de l'argent pour les impôts du roi, sur nos champs, et nos vignes, et nos maisons.
Wengine pia walisema, “Tumekopesha pesa kulipa kodi ya mfalme kwenye mashamba yetu na mashamba yetu ya mizabibu.
5 Et maintenant, notre chair est comme la chair de nos frères; nos fils sont comme leurs fils, et nous traitons nos fils et nos filles comme des esclaves; et il y a de nos filles qui sont servantes, et nous n'avons pas le pouvoir de les racheter; car les nobles possèdent nos champs et nos vignes.
Hata hivyo sasa miili yetu na damu ni sawa na ndugu zetu, na watoto wetu ni sawa na watoto wao. Tunalazimishwa kuuza wana wetu na binti zetu kuwa watumwa. Baadhi ya binti zetu tayari wamekuwa watumwa. Lakini hatuna nguvu za kusaidia kwa sababu watu wengine sasa wana mashamba yetu na mizabibu yetu.”
6 Et j'eus une grande affliction, quand j'ouïs leur clameur et ces discours;
Nilikasirika sana niliposikia kilio chao na maneno haya.
7 Et je tins conseil en mon cœur, et je combattis les nobles et les princes, et je leur dis: Un homme peut-il demander à son frère ce que vous demandez? Et je convoquai contre eux une grande assemblée.
Kisha nikafikiri juu ya hili, na kuleta mashtaka dhidi ya wakuu na viongozi. Nikawaambia, “Ninyi mnatafuta riba, kila mmoja kutoka kwa ndugu yake mwenyewe.” Nikakutanisha kusanyiko kubwa juu yao
8 Et je leur dis: Nous avons, de nos dons volontaires, racheté nos frères les Juifs qui avaient été vendus aux gentils, et vous vendez vos frères; mais vous seront-ils livrés? Et ils gardèrent le silence, et ils ne trouvèrent pas un mot à dire.
na kuwaambia, “Sisi, kwa kadiri tulivyoweza, tumewakomboa toka utumwani ndugu zetu wa Kiyahudi ambao walikuwa wameuzwa kwa mataifa, lakini hata mnawauza ndugu na dada zenu ili wauzwe tena kwetu!” Walikuwa kimya na hawakupata neno la kusema.
9 Et je dis: Elle n'est pas bonne l'action que vous faites; ce n'est pas ainsi que vous vous soustrairez, par la crainte de Dieu, aux outrages des nations, vos ennemies.
Pia nikasema, 'Mnachokifanya sio kizuri. Je, hampaswi kutembea katika hofu ya Mungu wetu ili kuzuia malalamiko ya mataifa ambayo ni adui zetu?
10 Or, mes frères, mes parents et moi-même, nous leurs avons prêté de l'argent et du blé; eh bien! renonçons à rien exiger d'eux.
Mimi na ndugu zangu na watumishi wangu tunawapa fedha na nafaka. Lakini lazima tuache kutoza riba juu ya mikopo hii.
11 Rendez-leur dès aujourd'hui leurs champs, leurs vignes, leurs oliviers et leurs maisons; et apportez-leur du blé, du vin et de l'huile pour prix de l'argent.
Warudishieni leo leo mashamba yao, mizabibu yao, mashamba yao ya mizeituni, na nyumba zao na asilimia ya fedha, nafaka, divai mpya, na mafuta mliyowatoza.”
12 Et ils dirent: Nous rendrons tout; nous ne leur demanderons rien, et nous ferons ce que tu dis. Et j'appelai les prêtres, et je les adjurai de faire selon cette parole.
Wakasema, “Tutarudisha kile tulichochukua kutoka kwao, wala hatutahitaji kitu kutoka kwao. Tutafanya kama unavyosema.” Ndipo nikawaita makuhani, na kuwaapisha kuwafanya kama walivyoahidi.
13 Et je secouai mon manteau, et je dis: Que Dieu ainsi secoue hors de sa maison et de son jardin tout homme qui n'accomplira pas cette parole; que cet homme soit ainsi secoué et vide. Et toute l'Église dit: Amen. Et ils louèrent le Seigneur, et le peuple fit comme il avait été dit.
Nikakung'uta vazi langu, nikasema, “Basi Mungu aondoe nyumba na mali ya kila mtu asiyetimiza ahadi yake. Kwa hiyo akung'utwe na kuwa hana kitu. Kusanyiko lote likasema “Amina,” na wakamsifu Bwana. Na watu wakafanya kama walivyoahidi.
14 Depuis le jour où le roi m'avait commandé d'être leur chef en la terre de Juda: de la vingtième à la trente-deuxième année du règne d'Arthasastha, pendant douze ans, ni moi ni mes frères nous ne mangeâmes de vivres extorqués d'eux.
Kwa hiyo tangu wakati niliowekwa kuwa mkuu wao katika nchi ya Yuda, tangu mwaka wa ishirini mpaka mwaka wa thelathini na pili wa mfalme Artashasta, miaka kumi na miwili, mimi na ndugu zangu hatukula chakula kilichotolewa kwa gavana.
15 Et toutes les extorsions dont mes devanciers les grevaient avant moi, leur avaient enlevé jusqu'à leur dernier argent; ils leur prenaient pour le pain et le vin quarante sicles par jour; et leurs agents avaient toute autorité sur le peuple; et moi je ne fis pas ainsi, en face de la crainte de Dieu.
Lakini wakuu wa zamani waliokuwa kabla yangu waliwaweka watu mizigo mizito, na wakachukua kwao shekeli arobaini za fedha kwa ajili ya chakula na divai yao ya kila siku. Hata watumishi wao waliwadhulumu watu. Lakini sikufanya hivyo kwa sababu ya hofu ya Mungu.
16 Et, pendant la réédification des murailles, je ne leur extorquai rien, je n'achetai point de champ, non plus qu'aucun de ceux que j'avais rassemblés pour cette œuvre.
Niliendelea kufanya kazi kwenye ukuta, na hatukununua ardhi. Na watumishi wangu wote walikusanyika huko kwa ajili ya kazi hiyo.
17 Et les Juifs, au nombre de cent cinquante, et ceux des gentils qui venaient d'alentour auprès de nous, mangeaient à ma table.
Katika meza yangu walikuwa Wayahudi na maafisa, watu 150, isipokuwa wale waliokuja kwetu kutoka kwa mataifa waliokuwa wakituzunguka.
18 Et tous les jours on m'amenait un bœuf, six brebis de choix et un chevreau. Et, tous les dix jours, il me venait pour nous tous une ample provision de vin; et, avec tout cela, je ne pris jamais de vivres par extorsion, parce que la servitude avait été pesante pour le peuple.
Kila kitu kilichoandaliwa kila siku kilikuwa ng'ombe moja, kondoo sita waliochaguliwa, na ndege, na kila siku kumi aina zote za divai nyingi. Na hata kwa haya yote sikuhitaji mahitaji ya chakula cha gavana, kwa sababu madai yalikuwa mazito sana juu ya watu.
19 Souvenez-vous de moi, mon Dieu, pour mon bien, à cause de tout ce que j'ai fait en faveur de ce peuple.
Nikumbuke, Ee Mungu wangu, kwa wema, kwa sababu ya yote niliyoyafanya kwa watu hawa.

< Néhémie 5 >