< Luc 20 >

1 Et il arriva, l’un de ces jours, comme il enseignait le peuple dans le temple et évangélisait, que les principaux sacrificateurs et les scribes survinrent avec les anciens.
Siku moja, Yesu alipokuwa akiwafundisha watu Hekaluni na kuwahubiria juu ya Habari Njema, makuhani wakuu na walimu wa Sheria pamoja na wazee walifika,
2 Et ils lui parlèrent, disant: Dis-nous par quelle autorité tu fais ces choses, ou qui est celui qui t’a donné cette autorité?
wakasema, “Tuambie! Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani?”
3 Et répondant, il leur dit: Je vous demanderai, moi aussi, une chose, et dites-moi:
Yesu akawaambia, “Na mimi nitawaulizeni swali:
4 Le baptême de Jean était-il du ciel, ou des hommes?
mamlaka ya Yohane ya kubatiza yalitoka kwa Mungu au kwa watu?”
5 Et ils raisonnèrent entre eux, disant: Si nous disons: Du ciel, il dira: Pourquoi ne l’avez-vous pas cru?
Lakini wao wakajadiliana hivi: “Tukisema yalitoka mbinguni, yeye atatuuliza: Mbona hamkumsadiki?
6 Et si nous disons: Des hommes, tout le peuple nous lapidera, car il est persuadé que Jean était un prophète.
Na tukisema yalitoka kwa binadamu, watu wote hapa watatupiga mawe, maana wote wanaamini kwamba Yohane alikuwa nabii.”
7 Et ils répondirent qu’ils ne savaient pas d’où [il était].
Basi, wakamwambia, “Hatujui mamlaka hayo yalitoka wapi.”
8 Et Jésus leur dit: Moi non plus, je ne vous dis pas par quelle autorité je fais ces choses.
Yesu akawaambia, “Hata mimi sitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani.”
9 Et il se mit à dire au peuple cette parabole: Un homme planta une vigne, et la loua à des cultivateurs, et s’en alla hors du pays pour longtemps.
Yesu akaendelea kuwaambia watu mfano huu: “Mtu mmoja alilima shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima; kisha akasafiri hadi nchi ya mbali, akakaa huko kwa muda mrefu.
10 Et en la saison, il envoya un esclave aux cultivateurs, afin qu’ils lui donnent du fruit de la vigne; mais les cultivateurs, l’ayant battu, le renvoyèrent à vide.
Wakati wa mavuno, mtu huyo alimtuma mtumishi wake kwa wale wakulima, akachukue sehemu ya matunda ya shamba la mizabibu. Lakini wale wakulima wakampiga mtumishi huyo wakamrudisha mikono mitupu.
11 Et il envoya encore un autre esclave; mais l’ayant battu lui aussi, et l’ayant traité ignominieusement, ils le renvoyèrent à vide.
Yule bwana akamtuma tena mtumishi mwingine; lakini wao wakampiga huyo vilevile na kumtendea vibaya, wakamrudisha mikono mitupu.
12 Et il en envoya encore un troisième; mais ils blessèrent aussi celui-ci, et le jetèrent dehors.
Akamtuma tena wa tatu; huyu naye, baada ya kumwumiza, wakamfukuza.
13 Et le maître de la vigne dit: Que ferai-je? J’enverrai mon fils bien-aimé; peut-être que, quand ils verront celui-ci, ils le respecteront.
Yule mwenye shamba akafikiri: Nitafanya nini? Nitamtuma mwanangu mpenzi; labda watamjali yeye.
14 Mais quand les cultivateurs le virent, ils raisonnèrent entre eux, disant: Celui-ci est l’héritier, tuons-le, afin que l’héritage soit à nous.
Wale wakulima walipomwona tu, wakasemezana: Huyu ndiye mrithi. Basi, tumwue ili urithi wake uwe wetu.
15 Et l’ayant jeté hors de la vigne, ils le tuèrent. Que leur fera donc le maître de la vigne?
Basi, wakamtoa nje ya lile shamba la mizabibu, wakamwua.” Yesu akauliza, “Yule mwenye shamba atawafanya nini hao wakulima?
16 Il viendra et fera périr ces cultivateurs, et donnera la vigne à d’autres. Et l’ayant entendu, ils dirent: Qu’ainsi n’advienne!
Atakuja kuwaangamiza wakulima hao, na atawapa wakulima wengine hilo shamba la mizabibu.” Watu waliposikia maneno hayo, walisema: “Hasha! Yasitukie hata kidogo!”
17 Et lui, les regardant, dit: Qu’est-ce donc que ceci qui est écrit: « La pierre que ceux qui bâtissaient ont rejetée, celle-là est devenue la maîtresse pierre du coin »?
Lakini Yesu akawatazama, akawaambia, “Maandiko haya Matakatifu yana maana gani basi? Jiwe walilokataa waashi, sasa limekuwa jiwe kuu la msingi!
18 Quiconque tombera sur cette pierre, sera brisé; mais celui sur qui elle tombera, elle le broiera.
Mtu yeyote akianguka juu ya jiwe hilo, atavunjika vipandevipande; na likimwangukia mtu yeyote, litamsaga kabisa.”
19 Et les principaux sacrificateurs et les scribes cherchèrent, en cette heure même, à mettre les mains sur lui; et ils craignaient le peuple, car ils connurent qu’il avait dit cette parabole contre eux.
Walimu wa Sheria na makuhani wakuu walifahamu kwamba mfano huo ulikuwa unawahusu, na hivyo walitaka kumkamata palepale, ila tu waliogopa watu.
20 Et l’observant, ils envoyèrent des agents secrets, qui feignaient d’être justes, pour le surprendre en [quelque] parole, de manière à le livrer au magistrat et au pouvoir du gouverneur.
Basi, wakawa wanatafuta wakati wa kufaa. Wakawahonga watu fulani wajisingizie kuwa wema, wakawatuma wamnase Yesu kwa maswali, na hivyo waweze kumtia nguvuni na kumpeleka kwa wakuu wa serikali.
21 Et ils l’interrogèrent, disant: Maître, nous savons que tu dis et que tu enseignes justement, et que tu n’as point égard à l’apparence des personnes, mais que tu enseignes la voie de Dieu avec vérité.
Hao wapelelezi wakamwambia, “Mwalimu, tunajua kwamba unasema na kufundisha mambo ya kweli; tunajua kwamba wewe huna ubaguzi; wewe wafundisha ukweli juu ya njia ya Mungu.
22 Nous est-il permis de payer le tribut à César, ou non?
Basi, twambie kama ni halali, au la, kulipa kodi kwa Kaisari!”
23 Et s’apercevant de leur perfidie, il leur dit: Pourquoi me tentez-vous?
Yesu alitambua mtego wao, akawaambia,
24 Montrez-moi un denier; de qui a-t-il l’image et l’inscription? Et répondant, ils dirent: De César.
“Nionyesheni sarafu. Je, sura na chapa ni vya nani?”
25 Et il leur dit: Rendez donc les choses de César à César, et les choses de Dieu à Dieu.
Nao wakamjibu, “Ni vya Kaisari.” Yesu akawaambia, “Basi, mpeni Kaisari vilivyo vyake Kaisari, na Mungu vilivyo vyake Mungu.”
26 Et ils ne pouvaient le surprendre dans ses paroles devant le peuple; et étonnés de sa réponse, ils se turent.
Hawakufaulu kumnasa kwa neno lolote pale mbele ya watu na hivyo wakakaa kimya wakilistaajabia jibu lake.
27 Et quelques-uns des sadducéens, qui nient qu’il y ait une résurrection, s’approchèrent, et l’interrogèrent,
Kisha Masadukayo, ambao husema kwamba wafu hawafufuki, wakamjia Yesu, wakasema:
28 disant: Maître, Moïse nous a écrit, que si le frère de quelqu’un meurt, ayant une femme, et qu’il meure sans enfants, son frère prenne la femme et suscite de la postérité à son frère.
“Mwalimu, Mose alituandikia kwamba kama ndugu ya mtu fulani akifa na kumwacha mjane wake bila watoto, ni lazima ndugu yake amchukue huyo mama mjane, amzalie watoto ndugu yake marehemu.
29 Il y avait donc sept frères; et le premier, ayant pris une femme, mourut sans enfants;
Sasa, wakati mmoja kulikuwa na ndugu saba. Yule wa kwanza alioa na baadaye akafa bila kuacha mtoto.
30 et le second [prit la femme, et celui-ci aussi mourut sans enfants];
Yule ndugu wa pili akamwoa yule mjane, naye pia, akafa;
31 et le troisième la prit, et de même aussi les sept: ils ne laissèrent pas d’enfants et moururent;
na ndugu wa tatu vilevile. Mambo yakawa yaleyale kwa wote saba—wote walikufa bila kuacha watoto.
32 et après eux tous la femme aussi mourut.
Mwishowe akafa pia yule mwanamke.
33 Dans la résurrection donc, duquel d’entre eux sera-t-elle la femme, car les sept l’ont eue pour femme?
Je, siku wafu watakapofufuliwa, mwanamke huyo atakuwa mke wa nani? Alikuwa ameolewa na wote saba.”
34 Et Jésus leur dit: Les fils de ce siècle se marient et sont donnés en mariage; (aiōn g165)
Yesu akawaambia, “Watu wa nyakati hizi huoa na kuolewa; (aiōn g165)
35 mais ceux qui seront estimés dignes d’avoir part à ce siècle-là et à la résurrection d’entre les morts, ne se marient ni ne sont donnés en mariage, (aiōn g165)
lakini wale ambao Mungu atawawezesha kushiriki ule wakati wa ufufuo, hawataoa wala kuolewa. (aiōn g165)
36 car aussi ils ne peuvent plus mourir; car ils sont semblables aux anges, et ils sont fils de Dieu, étant fils de la résurrection.
Ama hakika, hawawezi kufa tena, kwa sababu watakuwa kama malaika, na ni watoto wa Mungu kwa vile wamefufuliwa katika wafu.
37 Or que les morts ressuscitent, Moïse même l’a montré, au [titre]: “Du buisson”, quand il appelle le Seigneur: le Dieu d’Abraham, et le Dieu d’Isaac, et le Dieu de Jacob.
Lakini, kwamba kuna kufufuka kutoka wafu, hata Mose alithibitisha jambo hilo katika Maandiko Matakatifu. Katika sehemu ya Maandiko Matakatifu juu ya kile kichaka kilichokuwa kinawaka moto, anamtaja Bwana kama Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo.
38 Or il n’est pas le Dieu des morts, mais des vivants; car pour lui tous vivent.
Basi, yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa wale walio hai; maana wale aliowaita kwake, wanaishi naye.”
39 Et quelques-uns des scribes, répondant, dirent: Maître, tu as bien dit.
Baadhi ya wale walimu wa Sheria wakasema, “Mwalimu, umejibu vema kabisa.”
40 Et ils n’osèrent plus l’interroger sur rien.
Walisema hivyo kwa sababu hawakuthubutu kumwuliza tena maswali mengine.
41 Et il leur dit: Comment dit-on que le Christ est fils de David?
Yesu akawauliza, “Yasemekanaje kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?
42 Et David lui-même dit, dans le livre des Psaumes: « Le Seigneur a dit à mon seigneur: Assieds-toi à ma droite,
Maana Daudi mwenyewe anasema katika Zaburi: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti upande wangu wa kulia
43 jusqu’à ce que je mette tes ennemis pour marchepied de tes pieds ».
mpaka niwafanye adui zako kama kiti cha kuwekea miguu yako.
44 David donc l’appelle seigneur; et comment est-il son fils?
Ikiwa Daudi anamwita yeye, Bwana, basi atakuwaje mwanawe?”
45 Et comme tout le peuple écoutait, il dit à ses disciples:
Yesu aliwaambia wanafunzi wake mbele ya watu wote,
46 Soyez en garde contre les scribes, qui se plaisent à se promener en longues robes, et qui aiment les salutations dans les places publiques, et les premiers sièges dans les synagogues, et les premières places dans les repas;
“Jihadharini na walimu wa Sheria ambao hupenda kupitapita wamevalia kanzu. Hupenda kusalimiwa na watu kwa heshima masokoni, huketi mahali pa heshima katika masunagogi na kuchukua nafasi za heshima katika karamu.
47 qui dévorent les maisons des veuves, et pour prétexte font de longues prières; – ceux-ci recevront une sentence plus sévère.
Huwadhulumu wajane huku wakisingizia kuwa wema kwa kusali sala ndefu. Hao watapata hukumu kali zaidi!”

< Luc 20 >