< Isaïe 46 >

1 Bel s’est affaissé, Nebo se courbe; leurs idoles ont été [mises] sur les animaux et sur le bétail: celles que vous portiez sont chargées, – un fardeau pour la [bête] lassée!
Beli anasujudu hadi nchi, Nebo anainama; sanamu zao zabebwa na wanyama wa mizigo. Vinyago hivi mnavyobeba kila mahali ni mzigo wa kulemea, mzigo kwa waliochoka.
2 Ils se sont courbés, ils se sont affaissés ensemble; ils n’ont pas pu sauver leur fardeau: eux-mêmes sont allés en captivité.
Vinyago pamoja na wale wanaovibeba wanainama chini; hiyo miungu haiwezi kuwaokoa watu, wote wanakwenda utumwani pamoja.
3 Écoutez-moi, maison de Jacob, et vous, tout le résidu de la maison d’Israël, vous qui avez été chargés dès le ventre, [et] qui avez été portés dès la matrice:
“Nisikilizeni mimi, ee nyumba ya Yakobo, ninyi nyote mliobaki wa nyumba ya Israeli, ninyi ambao nimewategemeza tangu mlipotungwa mimba, nami nimewabeba tangu kuzaliwa kwenu.
4 Jusqu’à votre vieillesse je suis le Même, et jusqu’aux cheveux blancs, je vous porterai. Moi, je l’ai fait; moi, je porterai, et moi, je chargerai sur moi, et je délivrerai.
Hata mpaka wakati wa uzee wenu na mvi, Mimi ndiye, Mimi ndiye nitakayewasaidia ninyi. Nimewahuluku, nami nitawabeba, nitawasaidia ninyi na kuwaokoa.
5 À qui me comparerez-vous et m’égalerez-vous ou m’assimilerez-vous, pour que nous soyons semblables?
“Mtanilinganisha na nani, au mtanihesabu kuwa sawa na nani? Ni nani mtakayenifananisha naye ili tuweze kulinganishwa?
6 – Ils prodiguent l’or de la bourse, et pèsent l’argent à la balance; ils louent un orfèvre pour qu’il en fasse un dieu: ils se prosternent, oui, ils l’adorent;
Wengine humwaga dhahabu kutoka kwenye mifuko yao, na kupima fedha kwenye mizani; huajiri mfua dhahabu kutengeneza mungu, kisha huisujudia na kuiabudu.
7 ils le chargent sur l’épaule, ils le portent, et le posent à sa place; et il se tient debout, il ne quitte pas sa place; on crie bien à lui, mais il ne répond pas, il ne les sauve pas de leur détresse.
Huiinua mabegani na kuichukua; huiweka mahali pake, papo hapo ndipo isimamapo. Wala haiwezi kusogea kutoka mahali pale. Ingawa mtu huililia, haimjibu; haiwezi kumwokoa kwenye taabu zake.
8 Souvenez-vous de cela, et montrez-vous hommes; rappelez-le à votre esprit, transgresseurs.
“Kumbukeni hili, litieni akilini, liwekeni moyoni, enyi waasi.
9 Souvenez-vous des premières choses de jadis. Car moi, je suis Dieu, et il n’y en a pas d’autre; [je suis] Dieu, et il n’y en a point comme moi,
Kumbukeni mambo yaliyopita, yale ya zamani za kale; mimi ndimi Mungu, wala hakuna mwingine; mimi ndimi Mungu, wala hakuna mwingine aliye kama mimi.
10 déclarant dès le commencement ce qui sera à la fin, et d’ancienneté ce qui n’a pas été fait, disant: Mon conseil s’accomplira, et je ferai tout mon bon plaisir,
Ni mimi nitangazaye mwisho tangu mwanzo, naam, tangu zamani za kale, mambo ambayo hayajatendeka. Ninasema: Kusudi langu ndilo litakalosimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote.
11 appelant du levant un oiseau de proie, d’un pays lointain l’homme de mon conseil. Oui, je l’ai dit, et je ferai que cela arrivera; je me le suis proposé, et je l’effectuerai.
Kutoka mashariki ninaita ndege awindaye; kutoka nchi ya mbali, mtu atakayetimiza kusudi langu. Lile ambalo nimelisema, ndilo nitakalolitimiza; lile nililolipanga, ndilo nitakalolitenda.
12 Écoutez-moi, vous au cœur dur, qui êtes éloignés de la justice!
Nisikilizeni, ninyi wenye mioyo migumu, ninyi mlio mbali na haki.
13 J’ai fait approcher ma justice; elle ne sera pas éloignée, et mon salut ne tardera pas; et je mets en Sion le salut, [et] sur Israël ma gloire.
Ninaleta haki yangu karibu, haiko mbali; wala wokovu wangu hautachelewa. Nitawapa Sayuni wokovu, Israeli utukufu wangu.

< Isaïe 46 >