< Psalms 71 >

1 Lord, Y hopide in thee, be Y not schent with outen ende;
Ee Bwana, nimekukimbilia wewe, usiache nikaaibika kamwe.
2 in thi riytwisnesse delyuere thou me, and rauysche me out. Bowe doun thin eere to me; and make me saaf.
Kwa haki yako uniponye na kuniokoa, unitegee sikio lako uniokoe.
3 Be thou to me in to God a defendere; and in to a strengthid place, that thou make me saaf. For thou art my stidefastnesse; and my refuit.
Uwe kwangu mwamba wa kimbilio, mahali nitakapokimbilia kila wakati; toa amri ya kuniokoa, kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.
4 My God, delyuere thou me fro the hoond of the synner; and fro the hoond of a man doynge ayens the lawe, and of the wickid man.
Ee Mungu wangu uniokoe kutoka kwenye mkono wa mwovu, kutoka kwenye makucha ya watu wabaya na wakatili.
5 For thou, Lord, art my pacience; Lord, thou art myn hope fro my yongthe.
Kwa kuwa umekuwa tumaini langu, Ee Bwana Mwenyezi, tegemeo langu tangu ujana wangu.
6 In thee Y am confermyd fro the wombe; thou art my defendere fro the wombe of my modir.
Tangu kuzaliwa nimekutegemea wewe, ulinitoa tumboni mwa mama yangu. Nitakusifu wewe daima.
7 My syngyng is euere in thee; Y am maad as a greet wonder to many men; and thou art a strong helpere.
Nimekuwa kama kioja kwa wengi, lakini wewe ni kimbilio langu imara.
8 My mouth be fillid with heriyng; that Y synge thi glorie, al dai thi greetnesse.
Kinywa changu kimejazwa sifa zako, nikitangaza utukufu wako mchana kutwa.
9 Caste thou not awei me in the tyme of eldnesse; whanne my vertu failith, forsake thou not me.
Usinitupe wakati wa uzee, wala usiniache nguvu zangu zinapopungua.
10 For myn enemyes seiden of me; and thei that kepten my lijf maden counsel togidere.
Kwa maana adui zangu wananisengenya, wale wanaonivizia kuniua wafanya hila.
11 Seiynge, God hath forsake hym; pursue ye, and take hym; for noon is that schal delyuere.
Wanasema, “Mungu amemwacha, mkimbilieni mkamkamate, kwani hakuna wa kumwokoa.”
12 God, be thou not maad afer fro me; my God, biholde thou in to myn help.
Ee Mungu, usiwe mbali nami, njoo haraka kunisaidia, Ee Mungu wangu.
13 Men that bacbiten my soule, be schent, and faile thei; and be thei hilid with schenschip and schame, that seken yuels to me.
Washtaki wangu na waangamie kwa aibu, wale wanaotaka kunidhuru na wafunikwe kwa dharau na fedheha.
14 But Y schal hope euere; and Y schal adde euere ouer al thi preising.
Lakini mimi, nitatumaini siku zote, nitakusifu zaidi na zaidi.
15 Mi mouth schal telle thi riytfulnesse; al dai thin helthe. For Y knewe not lettrure, Y schal entre in to the poweres of the Lord;
Kinywa changu kitasimulia haki yako, wokovu wako mchana kutwa, ingawa sifahamu kipimo chake.
16 Lord, Y schal bithenke on thi riytfulnesse aloone.
Ee Bwana Mwenyezi, nitakuja na kutangaza matendo yako makuu, nitatangaza haki yako, yako peke yako.
17 God, thou hast tauyt me fro my yongthe, and `til to now; Y schal telle out thi merueilis.
Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu, hadi leo ninatangaza matendo yako ya ajabu.
18 And til in to `the eldnesse and the laste age; God, forsake thou not me. Til Y telle thin arm; to eche generacioun, that schal come. Til Y telle thi myyt,
Ee Mungu, usiniache, hata niwapo mzee wa mvi, mpaka nitangaze uwezo wako kwa kizazi kijacho, nguvu zako kwa wote watakaokuja baadaye.
19 and thi riytfulnesse, God, til in to the hiyeste grete dedis which thou hast do; God, who is lijk thee?
Ee Mungu, haki yako imefika juu katika mbingu, wewe ambaye umefanya mambo makuu. Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?
20 Hou grete tribulaciouns many and yuele hast thou schewid to me; and thou conuertid hast quykenyd me, and hast eft brouyt me ayen fro the depthis of erthe.
Ingawa umenifanya nipate taabu, nyingi na chungu, utanihuisha tena, kutoka vilindi vya dunia utaniinua tena.
21 Thou hast multiplied thi greet doyng; and thou conuertid hast coumfortid me.
Utaongeza heshima yangu na kunifariji tena.
22 For whi and Y schal knowleche to thee, thou God, thi treuthe in the instrumentis of salm; Y schal synge in an harpe to thee, that art the hooli of Israel.
Ee Mungu wangu, nitakusifu kwa kinubi kwa ajili ya uaminifu wako; Ee Uliye Mtakatifu wa Israeli, nitakuimbia sifa kwa zeze.
23 Mi lippis schulen make fulli ioye, whanne Y schal synge to thee; and my soule, which thou ayen bouytist.
Midomo yangu itapaza sauti kwa furaha ninapokuimbia sifa, mimi, ambaye umenikomboa.
24 But and my tunge schal thenke al dai on thi riytfulnesse; whanne thei schulen be schent and aschamed, that seken yuelis to me.
Ulimi wangu utasimulia matendo yako ya haki mchana kutwa, kwa maana wale waliotaka kunidhuru, wameaibishwa na kufadhaishwa.

< Psalms 71 >