< Psalms 45 >

1 To the ouercomere for the lilies, the most loued song of lernyng of the sones of Chore. Myn herte hath teld out a good word; Y seie my workis `to the kyng. Mi tunge is `a penne of a writere; writynge swiftli.
Moyo wangu unafurika kwa neno zuri; nitasoma kwa sauti maneno niliyo yaandika kuhusu mfalme; ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi mwenye ustadi.
2 Crist, thou art fairer in schap than the sones of men; grace is spred abrood in thi lippis; therfor God blessid thee withouten ende.
Wewe u mzuri sana kuliko mwanadamu yeyote; neema imemiminwa midomoni mwako; Kwa hiyo tunajua ya kuwa Mungu amekubariki milele.
3 Be thou gird with thi swerd; on thi hipe most myytili.
Weka upanga wako upande wako, wewe uliye mwenye nguvu, katika utukufu wako na enzi yako.
4 Biholde thou in thi schaplynesse and thi fairnesse; come thou forth with prosperite, and regne thou. For treuthe, and myldenesse, and riytfulnesse; and thi riyt hond schal lede forth thee wondurfuli.
Katika enzi yako enenda katika ushindi kwa sababu ya uaminifu, upole, na haki; mkono wako wa kuume utakufundisha mambo ya kutisha.
5 Thi scharpe arowis schulen falle in to the hertis of the enemyes of the kyng; puplis schulen be vndur thee.
Mishale yako ni mkali; watu huanguka chini yako; mishale yako imo ndani ya mioyo ya adui za mfalme.
6 God, thi seete is in to the world of world; the yerde of thi rewme is a yerde of riyt reulyng, `ethir of equite.
Kiti chako cha enzi, Mungu ni cha milele na milele; na fimbo ya haki ni fimbo ya utawala wako.
7 Thou louedist riytfulnesse, and hatidist wickidnesse; therfor thou, God, thi God, anoyntide thee with the oile of gladnesse, more than thi felowis.
Umeipenda haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekupaka mafuta ya furaha kuliko wenzako.
8 Mirre, and gumme, and cassia, of thi clothis, of the `housis yuer;
Mavazi yako yote hunukia manemane, udi, na mdalasini; kukoka katika majumba ya pembe vyombo vya muziki wa nyuzi vimekufurahisha.
9 of whiche the douytris of kyngis delitiden thee. A queen stood nyy on thi riyt side in clothing ouergildid; cumpassid with dyuersitee.
Binti za wafalme ni kati ya wake zako waheshimiwa; na mkono wako wa kuume amesimama malikia aliye vaa mavazi ya dhahabu ya Ofiri.
10 Douyter, here thou, and se, and bowe doun thin eere; and foryete thi puple, and the hows of thi fadir.
Sikiliza, mwanangu, tafakari na utege sikio lako; uwasahahu watu wako na watu wa nyumba ya baba yako.
11 And the kyng schal coueyte thi fairnesse; for he is thi Lord God, and thei schulen worschipe hym.
Hivyo mfalme atautamani uzuri wako; yeye ni Bwana wako; umstahi.
12 And the douytris of Tire in yiftis; alle the riche men of the puple schulen biseche thi cheer.
Binti wa Tiro atakuwepo akiwa na zawadi; matajiri kati wa watu watajipendekeza kwako.
13 Al the glorye of that douyter of the kyng is with ynne in goldun hemmes;
Binti mfalme katika jumba la kifahari ana utukufu wote; mavazi yake yametengenezwa kwa dhahabu.
14 sche is clothid aboute with dyuersitees. Virgyns schulen be brouyt to the kyng aftir hir; hir neiyboressis schulen be brouyt to thee.
Naye ataongozwa kwa mfalme akiwa katika mavazi ya dhahabu; mabikra, wenzake wanoumfuata, wataletwa kwako mafalme.
15 Thei schulen be brouyt in gladnesse, and ful out ioiyng; thei schulen be brouyt in to the temple of the kyng.
Wao wataongozwa kwa furaha na shangwe; wataingia mahali pa mfalme.
16 Sones ben borun to thee, for thi fadris; thou schalt ordeyne hem princes on al erthe.
Katika mahali pa baba zako watoto wako watakuwepo, ambao wewe utawafanya kuwa wakuu katika nchi yote.
17 Lord, thei schulen be myndeful of thi name; in ech generacioun, and in to generacioun. Therfor puplis schulen knouleche to thee withouten ende; and in to the world of world.
Nami nitalifanya jina lako kukumbukwa katika uzao wote; kwa hiyo watu watakushukuru milele na milele.

< Psalms 45 >