< Psalms 49 >
1 To victorie, a salm to the sones of Chore. Alle ye folkis, here these thingis; alle ye that dwellen in the world, perseyue with eeris.
Sikieni hili, ninyi watu wote; tegeni masikio, ninyi wenyeji wa dunia,
2 Alle the sones of erthe and the sones of men; togidere the riche man and the pore in to oon.
wote walio chini na walio juu, tajiri na masikini wote pamoja.
3 Mi mouth schal speke wisdom; and the thenkyng of myn herte schal speke prudence.
Mdomo wangu utazungumza hekima na tafakari ya moyo wangu itakuwa ya uelewa.
4 I schal bouwe doun myn eere in to a parable; Y schal opene my resoun set forth in a sautree.
Nitaelekeza sikio langu kwenye mfano; nitaanza mfano wangu kwa kinubi.
5 Whi schal Y drede in the yuel dai? the wickidnesse of myn heele schal cumpasse me.
Kwa nini nilazimike kuziogopa siku za uovu, wakati uovu umenizunguka kwenye visigino vyangu?
6 Whiche tristen in her owne vertu; and han glorie in the multitude of her richessis.
Kwa nini niwaogope wale wanao amini katika mali zao na kujivuna kuhusu utajiri wao?
7 A brother ayenbieth not, schal a man ayenbie? and he schal not yyue to God his plesyng.
Ni hakika kuwa hakuna yeyote atakaye muokoa ndugu yake au kumpa Mungu pesa kwa ajili yake,
8 And he schal not yyue the prijs of raunsum of his soule; and he schal trauele with outen ende,
Kwa maana ukombozi wa uhai wa mtu ni gharama kubwa, na hakuna awezaye kulipa kile tunacho daiwa.
9 and he schal lyue yit in to the ende.
Hakuna yeyote atakaye ishi milele ili mwili wake usioze.
10 He schal not se perischyng, whanne he schal se wise men diynge; the vnwise man and fool schulen perische togidere. And thei schulen leeue her richessis to aliens;
Maana yeye ataona uozo. Watu wenye hekima hufa; wajinga pia huangamia na kuacha mali zao kwa wengine.
11 and the sepulcris of hem ben the housis of hem with outen ende. The tabernaclis of hem ben in generacioun and generacioun; thei clepiden her names in her londis.
Mawazo yao ya ndani ni kuwa familia zao zitaishi milele, na mahali waishipo, kwa vizazi vyote; wanaita ardhi zao kwa majina yao wenyewe.
12 A man, whanne he was in honour, vndurstood not; he is comparisound to vnwise beestis, and he is maad lijk to tho.
Lakini mtu, kuwa na mali, haimaanishi atabaki hai; kama wanyama walioangamia.
13 This weie of hem is sclaundir to hem; and aftirward thei schulen plese togidere in her mouth.
Hii ni hatma ya wafanyao ujinga baada ya kufa, .................
14 As scheep thei ben set in helle; deth schal gnawe hem. And iust men schulen be lordis of hem in the morewtid; and the helpe of hem schal wexe eld in helle, for the glorie of hem. (Sheol )
Kama kondoo wamechaguliwa kwa ajili ya kuzimu na kifo kitakuwa mchungaji wao. Nao watatawaliwa na wenye haki ifikapo asubuhi, na miili yao italiwa kuzimuni, wakiwa hawana afasi ya kuishi kwa ajili yao. (Sheol )
15 Netheles God schal ayenbie my soule from the power of helle; whanne he schal take me. (Sheol )
Bali Mungu ataufufua uhai wangu kutoka katika nguvu ya kuzimu; naye atanipokea. (Selah) (Sheol )
16 Drede thou not, whanne a man is maad riche; and the glorie of his hows is multiplied.
Msifadhaike mtu awapo tajiri, utukufu wa nyumba yake uongezekapo.
17 For whanne he schal die, he schal not take alle thingis; and his glorie schal not go doun with him.
Maana atakapo kufa hataondoka na chochote; utukufu wake hautamfuata yeye.
18 For his soule schal be blessid in his lijf; he schal knouleche to thee, whanne thou hast do wel to hym.
Yeye huifurahisha nafsi yake awapo hai na watu hukusifu wewe uishipo maisha yako mwenyewe-
19 He schal entre til in to the generaciouns of hise fadris; and til in to with outen ende he schal not se liyt.
naye atakwenda kwenye ukoo wa baba zake naye kamwe hataiona nuru tena.
20 A man, whanne he was in honour, vndurstood not; he is comparisound to vnwise beestis, and is maad lijk to tho.
Yule ambaye ana mali lakini hana ufahamu ni kama wanyama, ambao wataangamia.