< Psalms 36 >

1 `To victorie, to Dauid, `the seruaunt of the Lord. The vniust man seide, that he trespasse in hym silf; the drede of God is not bifor hise iyen.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana. Kuna neno moyoni mwangu kuhusu hali ya dhambi ya mwovu. Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.
2 For he dide gilefuli in the siyt of God; that his wickidnesse be foundun to hatrede.
Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake.
3 The wordis of his mouth ben wickidnesse and gile, he nolde vndirstonde to do wel.
Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu, ameacha kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
4 He thouyte wickidnesse in his bed, he stood nyy al weie not good; forsothe he hatide not malice.
Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya, hujitia katika njia ya dhambi na hakatai lililo baya.
5 Lord, thi merci is in heuene; and thi treuthe is `til to cloudis.
Upendo wako, Ee Bwana, unafika hadi mbinguni, uaminifu wako hadi kwenye anga.
6 Thi riytfulnesse is as the hillis of God; thi domes ben myche depthe of watris. Lord, thou schalt saue men and beestis;
Haki yako ni kama milima mikubwa, hukumu zako ni kama kilindi kikuu. Ee Bwana, wewe huwahifadhi mwanadamu na mnyama.
7 as thou, God, hast multiplied thi merci. But the sones of men; schulen hope in the hilyng of thi wyngis.
Upendo wako usiokoma ni wa thamani mno! Watu wakuu na wadogo hujificha uvulini wa mbawa zako.
8 Thei schulen be fillid gretli of the plentee of thin hows; and thou schalt yyue drynke to hem with the steef streem of thi likyng.
Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako, nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.
9 For the wel of life is at thee; and in thi liyt we schulen se liyt.
Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima, katika nuru yako twaona nuru.
10 Lord, sette forth thi mercy to hem, that knowen thee; and thi ryytfulnesse to hem that ben of riytful herte.
Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe, haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.
11 The foot of pryde come not to me; and the hond of the synnere moue me not.
Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu, wala mkono wa mwovu usinifukuze.
12 There thei felden doun, that worchen wickidnesse; thei ben cast out, and myyten not stonde.
Angalia jinsi watenda mabaya walivyoanguka: wametupwa chini, hawawezi kuinuka!

< Psalms 36 >