< Ephesians 4 >

1 Therfor Y boundun for the Lord biseche you, that ye walke worthili in the clepyng,
Basi, mimi niliye mfungwa wa Bwana, nawasihi mwenende kama inavyostahili wito wenu mlioitiwa.
2 in which ye ben clepid, with al mekenesse and myldenesse, with pacience supportinge ech other in charite,
Kwa unyenyekevu wote na upole, mkiwa wavumilivu, mkichukuliana kwa upendo.
3 bisi to kepe vnyte of spirit in the boond of pees.
Jitahidini kudumisha umoja wa Roho katika kifungo cha amani.
4 O bodi and o spirit, as ye ben clepid in oon hope of youre cleping;
Kuna mwili mmoja na Roho mmoja, kama vile mlivyoitwa katika tumaini moja.
5 o Lord,
Tena kuna Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja,
6 o feith, o baptym, o God and fadir of alle, which is aboue alle men, and bi alle thingis, and in vs alle.
Mungu mmoja ambaye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote, katika yote na ndani ya yote.
7 But to ech of vs grace is youun bi the mesure of the yyuyng of Crist;
Lakini kila mmoja wetu amepewa neema kwa kadiri ya kipimo cha kipawa cha Kristo.
8 for which thing he seith, He stiynge an hiy, ledde caitifte caitif, he yaf yiftis to men.
Kwa hiyo husema: “Alipopaa juu zaidi, aliteka mateka, akawapa wanadamu vipawa.”
9 But what is it, that he stiede vp, no but that also he cam doun first in to the lowere partis of the erthe?
(Asemapo “alipaa juu,” maana yake nini isipokuwa ni kusema pia kwamba Kristo alishuka pande za chini sana za dunia?
10 He it is that cam doun, and that stiede on alle heuenes, that he schulde fille alle thingis.
Yeye aliyeshuka ndiye alipaa juu zaidi kupita mbingu zote, ili apate kuujaza ulimwengu wote.)
11 And he yaf summe apostlis, summe prophetis, othere euangelistis, othere scheepherdis and techeris,
Ndiye aliweka wengine kuwa mitume, wengine kuwa manabii, wengine kuwa wainjilisti, wengine kuwa wachungaji na walimu,
12 to the ful endyng of seyntis, in to the werk of mynystrie, in to edificacioun of Cristis bodi,
kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu kwa ajili ya kazi za huduma, ili kwamba mwili wa Kristo upate kujengwa
13 til we rennen alle, in to vnyte of feith and of knowyng of Goddis sone, in to a parfit man, aftir the mesure of age of the plente of Crist;
mpaka sote tutakapoufikia umoja katika imani na katika kumjua sana Mwana wa Mungu na kuwa watu wazima kwa kufikia kimo cha ukamilifu wa Kristo.
14 that we be not now litle children, mouynge as wawis, and be not borun aboute with ech wynd of teching, in the weiwardnesse of men, in sutil wit, to the disseyuyng of errour.
Ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwatupwa huku na huku na kuchukuliwa na kila upepo wa mafundisho kwa hila za watu, kwa ujanja, kwa kufuata njia zao za udanganyifu.
15 But do we treuthe in charite, and wexe in him by alle thingis, that is Crist oure heed;
Badala yake, tukiambiana kweli kwa upendo, katika mambo yote tukue, hata tumfikie yeye aliye kichwa, yaani, Kristo.
16 of whom alle the bodi set togidere, and boundun togidere bi ech ioynture of vnder seruyng, bi worching in to the mesure of ech membre, makith encreesyng of the bodi, in to edificacioun of it silf in charite.
Kutoka kwake, mwili wote ukiwa umeungamanishwa na kushikamanishwa pamoja kwa msaada wa kila kiungo, hukua na kujijenga wenyewe katika upendo, wakati kila kiungo kinafanya kazi yake.
17 Therfor Y seie and witnesse this thing in the Lord, that ye walke not now, as hethene men walken, in the vanyte of her wit;
Hivyo nawaambia hivi, nami nasisitiza katika Bwana kwamba, msiishi tena kama watu wa Mataifa waishivyo, katika ubatili wa mawazo yao.
18 that han vndurstondyng derkned with derknessis, and ben alienyd fro the lijf of God, bi ignoraunce that is in hem, for the blyndenesse of her herte.
Watu hao akili zao zimetiwa giza na wametengwa mbali na uzima wa Mungu kwa sababu ya ujinga wao kutokana na ugumu wa mioyo yao.
19 Which dispeirynge bitoken hem silf to vnchastite, in to the worchyng of al vnclennesse in coueitise.
Wakiisha kufa ganzi, wamejitia katika mambo ya ufisadi na kupendelea kila aina ya uchafu, wakiendelea kutamani zaidi.
20 But ye han not so lerud Crist, if netheles ye herden hym,
Lakini ninyi, hivyo sivyo mlivyojifunza Kristo.
21 and ben tauyt in hym, as is treuthe in Jhesu.
Kama hivyo ndivyo ilivyo, ninyi mmemsikia, tena mmefundishwa naye, vile kweli ilivyo katika Yesu.
22 Do ye awey bi the elde lyuyng the elde man, that is corrupt bi the desiris of errour;
Mlifundishwa kuuvua mwenendo wenu wa zamani, utu wenu wa kale, ulioharibiwa na tamaa zake za udanganyifu,
23 and be ye renewlid in the spirit of youre soule;
ili mfanywe upya roho na nia zenu,
24 and clothe ye the newe man, which is maad aftir God in riytwisnesse and hoolynesse of treuthe.
mkajivike utu mpya, ulioumbwa sawasawa na mfano wa Mungu katika haki yote na utakatifu.
25 For which thing `ye putte awei leesyng, and speke ye treuthe ech man with his neiybore, for we ben membris ech to othere.
Kwa hiyo kila mmoja wenu avue uongo na kuambiana kweli mtu na jirani yake, kwa maana sisi sote tu viungo vya mwili mmoja.
26 Be ye wrooth, and nyle ye do synne; the sunne falle not doun on youre wraththe.
Mkikasirika, msitende dhambi, wala jua lisichwe mkiwa bado mmekasirika,
27 Nyle ye yyue stide to the deuel.
wala msimpe ibilisi nafasi.
28 He that stal, now stele he not; but more trauele he in worchinge with hise hondis that that is good, that he haue whereof he schal yyue to nedi.
Yeye ambaye amekuwa akiiba, asiibe tena, lakini lazima ajishughulishe, afanye kitu kifaacho kwa mikono yake mwenyewe, ili awe na kitu cha kuwagawia wahitaji.
29 Ech yuel word go not of youre mouth; but if ony is good to the edificacioun of feith, that it yyue grace to men that heren.
Maneno mabaya yasitoke vinywani mwenu, bali yale yafaayo kwa ajili ya kuwajenga wengine kulingana na mahitaji yao, ili yawafae wale wasikiao.
30 And nyle ye make the Hooli Goost of God sori, in which ye ben markid in the dai of redempcioun.
Wala msimhuzunishe Roho Mtakatifu wa Mungu, ambaye kwake mlitiwa muhuri kwa ajili ya siku ya ukombozi.
31 Al bitternesse, and wraththe, and indignacioun, and cry, and blasfemye be takun awey fro you, with al malice;
Ondoeni kabisa uchungu, ghadhabu, hasira, makelele na masingizio pamoja na kila aina ya uovu.
32 and be ye togidere benygne, merciful, foryyuynge togidere, as also God foryaf to you in Crist.
Kuweni wafadhili na wenye kuhurumiana ninyi kwa ninyi, mkisameheana, kama vile naye Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.

< Ephesians 4 >