< Psalms 114 >

1 When Israel went out of Egypt, the house of Jacob from a people of foreign language,
Wakati Israeli walipotoka Misri, nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
2 Judah became his sanctuary, Israel his dominion.
Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu, Israeli akawa milki yake.
3 The sea saw it, and fled. The Jordan was driven back.
Bahari ilitazama ikakimbia, Yordani ulirudi nyuma,
4 The mountains skipped like rams, the little hills like lambs.
milima ilirukaruka kama kondoo dume, vilima kama wana-kondoo.
5 What was it, you sea, that you fled? You Jordan, that you turned back?
Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia, nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
6 You mountains, that you skipped like rams? You little hills, like lambs?
enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume, enyi vilima, kama wana-kondoo?
7 Tremble, you earth, at the presence of the Lord, at the presence of the God of Jacob,
Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana, mbele za Mungu wa Yakobo,
8 who turned the rock into a pool of water, the flint into a spring of waters.
aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji, mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.

< Psalms 114 >