< Luke 21 >

1 Jesus looked up and saw the rich men who were putting their gifts into the treasury.
Yesu alipoinua macho yake, aliwaona matajiri wakiweka sadaka zao kwenye sanduku la hazina ya Hekalu.
2 He saw a certain poor widow putting in two mites.
Akamwona pia mjane mmoja maskini akiweka humo sarafu mbili ndogo za shaba.
3 So he said, “Truly I say to you, this poor widow put in more than all of them.
Yesu akasema, “Amin, nawaambia, huyu mjane maskini ameweka humo zaidi ya watu wengine wote.
4 All of these gave gifts out of their abundance. But this widow, out of her poverty, put in all she had to live on.”
Hawa watu wengine wote wametoa sadaka kutokana na wingi wa mali zao. Lakini huyu mjane ametoa kutokana na umaskini wake vyote alivyokuwa navyo, hata kile alichohitaji ili kuishi.”
5 As some spoke of the temple, how it was decorated with beautiful stones and offerings, he said,
Baadhi ya wanafunzi wake wakawa wanamwonyesha jinsi Hekalu lilivyopambwa kwa mawe mazuri na kwa vitu vilivyotolewa kuwa sadaka kwa Mungu. Lakini Yesu akawaambia,
6 “As for these things that you see, the days will come when not one stone will be left on another which will not be torn down.”
“Kuhusu haya mnayoyaona hapa, wakati utafika ambapo hakuna jiwe moja litakalobaki juu ya jingine, bali kila moja litabomolewa.”
7 So they asked him, saying, “Teacher, when will these things happen? What will be the sign when these things are about to happen?”
Wakamuuliza, “Mwalimu, mambo haya yatatukia lini? Ni dalili gani itaonyesha kwamba yanakaribia kutendeka?”
8 Jesus answered, “Be careful that you are not deceived. For many will come in my name, saying, 'I am he,' and, 'The time is near.' Do not go after them.
Yesu akawajibu, “Jihadharini msije mkadanganywa. Maana wengi watakuja kwa Jina langu, wakidai, ‘Mimi ndiye,’ na, ‘Wakati umekaribia.’ Msiwafuate.
9 When you hear of wars and riots, do not be terrified, for these things must happen first, but the end will not happen immediately.”
Lakini msikiapo habari za vita na machafuko, msiogope. Kwa maana hayo ni lazima yatokee kwanza, ila ule mwisho hautakuja wakati huo.”
10 Then he said to them, “Nation will rise against nation, and kingdom against kingdom.
Kisha akawaambia: “Taifa litainuka dhidi ya taifa jingine, na ufalme mmoja dhidi ya ufalme mwingine.
11 There will be great earthquakes, and in various places famines and plagues. There will be terrifying events and great signs from heaven.
Kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, na njaa kali, na magonjwa ya kuambukiza katika sehemu mbalimbali. Pia kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara kuu kutoka mbinguni.
12 But before all of these things, they will lay their hands on you and will persecute you, delivering you over to the synagogues and prisons, bringing you before kings and governors because of my name.
“Lakini kabla yote hayajatokea, watawakamata ninyi na kuwatesa. Watawatia mikononi mwa wakuu wa masinagogi na kuwafunga magerezani. Nanyi mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya Jina langu.
13 It will lead to an opportunity for your testimony.
Hii itawapa nafasi ya kushuhudia.
14 Therefore resolve in your hearts not to prepare your defense ahead of time,
Lakini kusudieni mioyoni mwenu msisumbuke awali kuhusu mtakalosema mbele ya mashtaka.
15 for I will give you words and wisdom that all your adversaries will not be able to resist or contradict.
Kwa maana nitawapa maneno na hekima ambayo hakuna hata adui yenu mmoja atakayeweza kushindana nayo wala kuipinga.
16 But you will be delivered up also by parents, brothers, relatives, and friends, and they will put some of you to death.
Mtasalitiwa hata na wazazi, ndugu, jamaa na marafiki, na baadhi yenu watawaua.
17 You will be hated by everyone because of my name.
Mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya Jina langu.
18 But not a hair of your head will perish.
Lakini hapatakuwa na unywele mmoja wa kichwa chenu utakaoangamia.
19 In your endurance you will gain your souls.
Kwa kuvumilia mtaokoa roho zenu.
20 When you see Jerusalem surrounded by armies, then know that its destruction is near.
“Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, basi fahamuni kwamba kuharibiwa kwake kumekaribia.
21 Then let those in Judea flee to the mountains, let those who are in the city leave it, and those who are out in the country must not enter the city.
Wakati huo, wale walio Uyahudi wakimbilie milimani, walio mjini Yerusalemu watoke humo, nao wale walioko mashambani wasiingie mjini.
22 For these are days of vengeance, so that all the things that are written will be fulfilled.
Kwa sababu huu utakuwa ni wakati wa adhabu ili kutimiza yote yaliyoandikwa.
23 Woe to them who are pregnant and to them who are nursing in those days! For there will be great distress upon the land, and wrath to this people.
Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo! Kutakuwa na dhiki kuu katika nchi na ghadhabu juu ya hawa watu.
24 They will fall by the edge of the sword, and they will be led captive into all the nations, and Jerusalem will be trampled by the Gentiles until the times of the Gentiles are fulfilled.
Wataanguka kwa makali ya upanga, na wengine watachukuliwa kuwa mateka katika mataifa yote. Nao mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa Mataifa hadi muda wa hao watu wa Mataifa utimie.
25 There will be signs in the sun, in the moon, and in the stars, and on the earth. The nations will be in distress, anxious because of the roar of the sea and waves.
“Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Hapa duniani, mataifa yatakuwa katika dhiki na fadhaa kutokana na ngurumo na misukosuko ya bahari.
26 There will be men fainting from fear and from expectation of the things which are coming upon the world. For the powers of the heavens will be shaken.
Watu watazimia roho kutokana na hofu kuu na kuyaona yale mambo yanayotokea duniani, kwa maana nguvu za angani zitatikisika.
27 Then they will see the Son of Man coming in a cloud with power and great glory.
Wakati huo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni pamoja na uweza na utukufu mkuu.
28 But when these things begin to happen, stand up and lift up your heads, because your deliverance is coming near.”
Mambo haya yatakapoanza kutendeka, simameni na mkaviinue vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umekaribia.”
29 Jesus told them a parable, “Look at the fig tree, and all the trees.
Akawaambia mfano huu: “Uangalieni mtini na miti mingine yote.
30 When they sprout buds, you see for yourselves and know that summer is already near.
Inapochipua majani, ninyi wenyewe mnaweza kuona na kutambua wenyewe ya kuwa wakati wa kiangazi umekaribia.
31 So also, when you see these things happening, you know that the kingdom of God is near.
Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yakitukia, mnatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
32 Truly I say to you, this generation will not pass away until all these things take place.
“Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia.
33 Heaven and earth will pass away, but my words will never pass away.
Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.”
34 But pay attention to yourselves, so that your hearts are not burdened with the effects of drinking and intoxication, and the worries of life, and then that day will close on you suddenly like a trap.
“Jihadharini mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na fadhaa za maisha haya, nayo siku ile ikawakuta ninyi bila kutazamia kama vile mtego unasavyo.
35 For it will come upon everyone living on the face of the whole earth.
Kwa maana kama vile mtego unasavyo, ndivyo siku hiyo itakavyowapata wanadamu wote waishio katika uso wa dunia yote.
36 But be alert at all times, praying that you may be strong enough to escape all these things that will take place, and to stand before the Son of Man.”
Kesheni daima na mwombe ili mweze kuokoka na yale yote yatakayotokea na kusimama mbele ya Mwana wa Adamu.”
37 So during the days he was teaching in the temple, and at night he went out and stayed on the Mount of Olives.
Kila siku Yesu alikuwa akifundisha Hekaluni, na jioni ilipofika, alikwenda zake kwenye Mlima wa Mizeituni na kukaa huko usiku kucha.
38 All of the people came early in the morning to hear him in the temple.
Nao watu wote walikuja asubuhi na mapema Hekaluni ili kumsikiliza.

< Luke 21 >