< John 1 >
1 In the beginning was the Word, and the Word was with God, and the Word was God.
Hapo mwanzo alikuwako Neno, huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.
2 This one was in the beginning with God.
Tangu mwanzo huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu.
3 All things were made through him, and without him there was not one thing made that has been made.
Vitu vyote viliumbwa kwa yeye, wala pasipo yeye hakuna chochote kilichoumbwa ambacho kimeumbwa.
4 In him was life, and the life was the light of men.
Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima na huo uzima ulikuwa nuru ya watu.
5 The light shines in the darkness, and the darkness did not overcome it.
Nuru hungʼaa gizani nalo giza halikuishinda.
6 There was a man who was sent from God, whose name was John.
Alikuja mtu mmoja aliyetumwa kutoka kwa Mungu, jina lake Yohana.
7 He came as a witness to testify about the light, that all might believe through him.
Alikuja kama shahidi apate kuishuhudia hiyo nuru, ili kwa kupitia kwake watu wote waweze kuamini.
8 John was not the light, but came that he might testify about the light.
Yeye mwenyewe hakuwa ile nuru, bali alikuja kuishuhudia hiyo nuru.
9 The true light, which gives light to all men, was coming into the world.
Kwamba nuru halisi, imwangaziayo kila mtu ilikuwa inakuja ulimwenguni.
10 He was in the world, and the world was made through him, and the world did not know him.
Huyo Neno alikuwako ulimwenguni na ingawa ulimwengu uliumbwa kupitia kwake, haukumtambua.
11 He came to his own, and his own did not receive him.
Alikuja kwa walio wake, lakini wao hawakumpokea.
12 But to as many as received him, who believed in his name, he gave the right to become children of God.
Bali wote waliompokea, aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake.
13 These were not born of blood, nor of the will of the flesh, nor of the will of man, but of God.
Hawa ndio wasiozaliwa kwa damu, wala kwa mapenzi ya mwili au kwa mapenzi ya mtu, bali kwa mapenzi ya Mungu.
14 The Word became flesh and lived among us. We have seen his glory, glory as of the one and only who came from the Father, full of grace and truth.
Neno alifanyika mwili, akakaa miongoni mwetu, nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba, amejaa neema na kweli.
15 John testified about him and cried out, saying, “This was the one of whom I said, 'He who comes after me is greater than I am, for he was before me.'”
Yohana alishuhudia habari zake, akapaza sauti, akisema, “Huyu ndiye yule niliyewaambia kwamba, ‘Yeye ajaye baada yangu ni mkuu kuniliko mimi, kwa kuwa alikuwepo kabla yangu.’”
16 For from his fullness we have all received grace after grace.
Kutokana na ukamilifu wake, sisi sote tumepokea neema juu ya neema.
17 For the law was given through Moses. Grace and truth came through Jesus Christ.
Kwa kuwa sheria ilitolewa kwa mkono wa Mose, lakini neema na kweli imekuja kupitia Yesu Kristo.
18 No one has seen God at any time. The one and only God, who is at the side of the Father, he has made him known.
Hakuna mtu yeyote aliyemwona Mungu wakati wowote, ila ni Mungu Mwana pekee, aliye kifuani mwa Baba ndiye ambaye amemdhihirisha.
19 This is the testimony of John when the Jews sent priests and Levites to him from Jerusalem to ask him, “Who are you?”
Huu ndio ushuhuda wa Yohana wakati Wayahudi walipowatuma makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu kumuuliza, “Wewe ni nani?”
20 He confessed—he did not deny, but confessed—”I am not the Christ.”
Yohana alikiri waziwazi pasipo kuficha akasema, “Mimi si Kristo.”
21 So they asked him, “What are you then? Are you Elijah?” He said, “I am not.” They said, “Are you the prophet?” He answered, “No.”
Wakamuuliza, “Wewe ni nani basi? Je, wewe ni Eliya?” Yeye akajibu, “Hapana, mimi siye.” “Je, wewe ni yule Nabii?” Akajibu, “Hapana.”
22 Then they said to him, “Who are you, so that we may give an answer to those who sent us? What do you say about yourself?”
Ndipo wakasema, “Basi tuambie wewe ni nani ili tupate jibu la kuwapelekea wale waliotutuma. Wewe wasemaje juu yako mwenyewe?”
23 He said, “I am a voice, crying in the wilderness: 'Make the way of the Lord straight,' just as Isaiah the prophet said.”
Akawajibu kwa maneno ya nabii Isaya, akisema, “Mimi ni sauti ya mtu aliaye nyikani, ‘Yanyoosheni mapito ya Bwana.’”
24 Now some from the Pharisees were sent,
Basi walikuwa wametumwa watu kutoka kwa Mafarisayo
25 and they asked him and said to him, “Why do you baptize then if you are not the Christ nor Elijah nor the prophet?”
wakamuuliza, “Kama wewe si Kristo, wala si Eliya na wala si yule Nabii, kwa nini basi unabatiza?”
26 John answered them, saying, “I baptize with water. But among you stands someone you do not know.
Yohana akawajibu, “Mimi ninabatiza kwa maji, lakini katikati yenu yupo mtu msiyemjua.
27 He is the one who comes after me, the strap of whose sandal I am not worthy to untie.”
Yeye ajaye baada yangu, sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake.”
28 These things were done in Bethany on the other side of the Jordan, where John was baptizing.
Mambo haya yote yalitukia huko Bethania, ngʼambo ya Mto Yordani, mahali Yohana alipokuwa akibatiza.
29 The next day John saw Jesus coming to him and said, “Look, there is the Lamb of God, who takes away the sin of the world!
Siku iliyofuata, Yohana alimwona Yesu akimjia akasema, “Tazama, Mwana-Kondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu!
30 This is the one of whom I said, 'The one who comes after me is more than me, for he was before me.'
Huyu ndiye yule niliyewaambia kwamba, ‘Mtu anakuja baada yangu ambaye ni mkuu kuniliko mimi, kwa kuwa alikuwepo kabla yangu.’
31 I did not know him, but it was so that he could be revealed to Israel that I came baptizing with water.”
Mimi mwenyewe sikumfahamu, lakini sababu ya kuja nikibatiza kwa maji ni ili yeye apate kufunuliwa kwa Israeli.”
32 John testified, saying, “I saw the Spirit descending like a dove from heaven, and it stayed upon him.
Kisha Yohana akatoa ushuhuda huu: “Nilimwona Roho akishuka kutoka mbinguni kama hua, akakaa juu yake.
33 I did not recognize him, but he who sent me to baptize in water said to me, 'Upon whom you shall see the Spirit descending and remaining on him, he is the one baptizing in the Holy Spirit.'
Mimi nisingemtambua, lakini yeye aliyenituma nibatize kwa maji alikuwa ameniambia, ‘Yule mtu utakayemwona Roho akimshukia na kukaa juu yake, huyo ndiye atakayebatiza kwa Roho Mtakatifu.’
34 I have both seen and testified that this is the Son of God.”
Mimi mwenyewe nimeona jambo hili na ninashuhudia kuwa huyu ndiye Mwana wa Mungu.”
35 Again, the next day, as John was standing with two of his disciples,
Siku iliyofuata, Yohana alikuwa huko tena pamoja na wanafunzi wake wawili.
36 they saw Jesus walking by, and John said, “Look, the Lamb of God!”
Alipomwona Yesu akipita, akasema, “Tazama, Mwana-Kondoo wa Mungu!”
37 His two disciples heard him say this and they followed Jesus.
Wale wanafunzi wawili walipomsikia Yohana akisema haya, wakamfuata Yesu.
38 Then Jesus turned and saw them following him and said to them, “What do you want?” They replied, “Rabbi (which translated means teacher), where are you staying?”
Yesu akageuka, akawaona wakimfuata akawauliza, “Mnataka nini?” Wakamwambia, “Rabi,” (maana yake Mwalimu), “Unaishi wapi?”
39 He said to them, “Come and see.” Then they came and saw where he was staying; they stayed with him that day, for it was about the tenth hour.
Yesu akawajibu, “Njooni, nanyi mtapaona!” Hivyo wakaenda na kupaona mahali alipokuwa anaishi, wakakaa naye siku ile, kwa kuwa ilikuwa yapata saa kumi.
40 One of the two who heard John speak and then followed Jesus was Andrew, the brother of Simon Peter.
Andrea nduguye Simoni Petro, alikuwa mmoja wa wale wawili waliosikia yale Yohana aliyokuwa amesema, naye ndiye alimfuata Yesu.
41 He first found his own brother Simon and said to him, “We have found the Messiah” (which translated is: Christ).
Kitu cha kwanza Andrea alichofanya ni kumtafuta Simoni nduguye na kumwambia, “Tumemwona Masiya” (yaani, Kristo).
42 He brought him to Jesus, and Jesus looked at him and said, “You are Simon son of John. You will be called Cephas” (which is translated Peter).
Naye akamleta kwa Yesu. Yesu akamwangalia na kusema, “Wewe ni Simoni mwana wa Yohana. Utaitwa Kefa” (ambalo limetafsiriwa Petro).
43 The next day, when Jesus wanted to leave to go to Galilee, he found Philip and said to him, “Follow me.”
Siku iliyofuata Yesu aliamua kwenda Galilaya. Akamkuta Filipo, akamwambia, “Nifuate.”
44 Now Philip was from Bethsaida, the city of Andrew and Peter.
Basi Filipo alikuwa mwenyeji wa Bethsaida, mji alikotoka Andrea na Petro.
45 Philip found Nathaniel and said to him, “He of whom Moses wrote in the law, and the prophets, we have found him: Jesus son of Joseph, from Nazareth.”
Filipo naye akamkuta Nathanaeli na kumwambia, “Tumemwona yeye ambaye Mose aliandika habari zake katika Sheria na ambaye pia manabii waliandika kumhusu, yaani, Yesu wa Nazareti, mwana wa Yosefu.”
46 Nathaniel said to him, “Can any good thing come out of Nazareth?” Philip said to him, “Come and see.”
Nathanaeli akauliza, “Nazareti! Je, kitu chochote chema chaweza kutoka Nazareti?” Filipo akamwambia, “Njoo uone.”
47 Jesus saw Nathaniel coming to him and said about him, “See, a true Israelite, in whom is no deceit!”
Yesu alipomwona Nathanaeli anakaribia, akanena habari zake akasema, “Tazama huyu ni Mwisraeli kweli kweli; hana hila ndani yake.”
48 Nathaniel said to him, “How do you know me?” Jesus answered and said to him, “Before Philip called you, when you were under the fig tree, I saw you.”
Nathanaeli akamuuliza, “Umenifahamuje?” Yesu akamjibu, “Nilikuona ulipokuwa bado uko chini ya mtini, kabla hata Filipo hajakuita.”
49 Nathaniel replied, “Rabbi, you are the Son of God! You are the King of Israel!”
Nathanaeli akamwambia, “Rabi, wewe ni Mwana wa Mungu! Wewe ni Mfalme wa Israeli!”
50 Jesus replied and said to him, “Because I said to you, 'I saw you underneath the fig tree,' do you believe? You will see greater things than this.”
Yesu akamwambia, “Unaamini kwa kuwa nilikuambia nilikuona ulipokuwa bado uko chini ya mtini? Basi utaona mambo makuu zaidi kuliko hilo.”
51 Then he said, “Truly, truly, I say to you, you will see the heavens opened, and the angels of God ascending and descending upon the Son of Man.”
Ndipo akawaambia, “Amin, amin nawaambia, ninyi mtaona mbingu ikifunguka na malaika wa Mungu wakipanda na kushuka juu ya Mwana wa Adamu.”