< Job 31 >

1 I have made a covenant with my eyes; how then should I look with desire on a virgin?
“Nimefanya agano na macho yangu yasimtazame msichana kwa kumtamani.
2 For what is the portion from God above, the inheritance from the Almighty on high?
Kwa kuwa fungu la mwanadamu ni gani kutoka kwa Mungu juu, urithi wake kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu Aliye juu?
3 I used to think that calamity is for unrighteous people, and that disaster is for doers of wickedness.
Je, si uharibifu kwa watu waovu, maangamizi kwa wale watendao mabaya?
4 Does not God see my ways and count all my steps?
Je, yeye hazioni njia zangu na kuihesabu kila hatua yangu?
5 If I have walked with falsehood, if my foot has hurried to deceit,
“Kama nimeishi katika uongo au mguu wangu umekimbilia udanganyifu,
6 let me be weighed in an even balance so that God will know my integrity.
Mungu na anipime katika mizani za uaminifu, naye atajua kwamba sina hatia:
7 If my step has turned aside from the way, if my heart has gone after my eyes, if any spot has stuck to my hands,
kama hatua zangu zimepotoka kutoka kwenye njia, kama moyo wangu umeongozwa na macho yangu, au kama mikono yangu imetiwa unajisi,
8 then let me sow, and let another eat, and let my crops be uprooted.
basi wengine na wale nilichokipanda, nayo yale yote niliyootesha na yangʼolewe.
9 If my heart has been deceived by a woman, if I have lain in wait at my neighbor's door,
“Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke, au kama nimevizia mlangoni mwa jirani yangu,
10 then let my wife grind grain for another, and let others bow down on her.
basi mke wangu na asage nafaka ya mwanaume mwingine, nao wanaume wengine walale naye.
11 For that would be a terrible crime; indeed, it would be a crime to be punished by judges.
Kwa kuwa hilo lingekuwa aibu, naam, dhambi ya kuhukumiwa.
12 For that is a fire that consumes as far as Abaddon, and it would burn all my harvest to the root.
Ni moto uwakao kwa Uharibifu; ungekuwa umengʼoa mavuno yangu.
13 If I ignored the plea for justice from my male or female servant when they argued with me,
“Kama ningewanyima haki watumishi wangu wanaume au vijakazi wangu, walipokuwa na manungʼuniko dhidi yangu,
14 what then would I do when God rises up to accuse me? When he comes to judge me, how would I answer him?
nitafanya nini Mungu atakaponikabili? Nitamjibu nini nitakapoitwa kutoa hesabu?
15 Did the one who made me in the womb not make them also? Did not the same one mold us all in the womb?
Je, yeye aliyeniumba tumboni mwa mama yangu, si ndiye aliwaumba? Je, si ni yeye huyo mmoja aliyetuumba sote ndani ya mama zetu?
16 If I have withheld poor people from their desire, or if I have caused the eyes of the widow to grow dim from crying,
“Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, au kuyaacha macho ya wajane yadhoofike,
17 or if I have eaten my morsel alone and not allowed those without fathers to eat it also—
kama nimekula chakula changu mwenyewe, bila kuwashirikisha yatima;
18 because from my youth the orphan grew up with me as with a father, and I have guided his mother, a widow, from my own mother's womb.
lakini tangu ujana wangu nimemlea yatima kama ambavyo baba angefanya, nami tangu kuzaliwa kwangu nimewaongoza wajane:
19 If I have seen anyone perish for lack of clothing, or if I have seen that a needy man had no clothing;
kama nilimwona yeyote akiteseka kwa kukosa nguo, au mtu mhitaji asiye na mavazi
20 if his heart has not blessed me because he has not been warmed with the wool of my sheep,
ambaye wala moyo wake haukunibariki kwa kumpatia joto kwa mavazi ya manyoya ya kondoo zangu,
21 if I have lifted up my hand against fatherless people because I saw my support in the city gate, then bring charges against me!
na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima, nikijua kuwa nina ushawishi mahakamani,
22 If I have done these things, then let my shoulder fall from the shoulder blade, and let my arm be broken from its joint.
basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu, nao na uvunjike kutoka kiungio chake.
23 For I dreaded destruction from God; because of his majesty, I was not able to do those things.
Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu, nami kwa kuuogopa utukufu wake sikuweza kufanya mambo kama hayo.
24 If I have made gold my hope, and if I have said to fine gold, 'You are what I am confident in';
“Kama nimeweka tumaini langu kwenye dhahabu, au kuiambia dhahabu safi, ‘Wewe ndiwe salama yangu,’
25 if I have rejoiced because my wealth was great, because my hand had gotten many possessions, then bring charges against me!
kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu, ustawi ambao mikono yangu ilikuwa imepata,
26 If I have seen the sun when it shone, or the moon walking in its brightness,
kama nimelitazama jua katika kungʼaa kwake au mwezi ukienda kwa fahari yake,
27 and if my heart has been secretly attracted, so that my mouth has kissed my hand in worship of them—
hivyo moyo wangu kushawishiwa kwa siri, au kubusu mkono wangu kwa kuviheshimu,
28 this also would be a crime to be punished by judges, for I would have denied the God who is above.
basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa, kwa kuwa ningekuwa si mwaminifu kwa Mungu aishiye juu sana.
29 If I have rejoiced at the destruction of anyone who hated me or congratulated myself when disaster overtook him, then bring charges against me!
“Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu, au kutazama kwa furaha taabu iliyomjia,
30 Indeed, I have not even allowed my mouth to sin by asking for his life with a curse.
lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi kwa kuomba laana dhidi ya maisha yake;
31 If the men of my tent have never said, 'Who can find one who has not been filled with Job's food?'
kama watu wa nyumbani mwangu kamwe hawakusema, ‘Ni nani ambaye hajashibishwa na nyama ya Ayubu?’
32 (even the foreigner has never had to stay in the city square, because I have always opened my doors to the traveler), and if that is not so, then bring charges against me!
Lakini hakuna mgeni aliyelala njiani, kwa maana mlango wangu ulikuwa wazi kwa msafiri;
33 If, like mankind, I have hidden my sins by hiding my guilt inside my tunic
kama nimeifunika dhambi yangu kama wanadamu wengine wafanyavyo, kwa kuficha hatia yangu moyoni mwangu,
34 (because I feared the great multitude, because the contempt of families terrified me, so that I kept silent and would not go outside), then bring charges against me!
kwa sababu ya kuogopa umati wa watu, na hivyo kuwa na hofu ya kudharauliwa na jamaa, nikanyamaza kimya nisitoke nje ya mlango:
35 Oh, if only I had someone to hear me! See, here is my signature; let the Almighty answer me! If only I had the indictment that my opponent has written!
(“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia! Tazama sasa ninatia sahihi kwenye utetezi wangu: Mwenyezi na anijibu; mshtaki wangu na aweke mashtaka yake kwenye maandishi.
36 Surely I would carry it openly on my shoulder; I would put it on like a crown.
Hakika ningeyavaa begani mwangu, ningeyavaa kama taji.
37 I would declare to him an accounting for my steps; as a confident prince I would go up to him.
Ningempa hesabu ya kila hatua yangu, ningemwendea kama mwana wa mfalme.)
38 If my land ever cries out against me, and its furrows weep together,
“Kama nchi yangu inalia dhidi yangu, na mifereji yake yote imelowana kwa machozi,
39 if I have eaten its harvest without paying for it or have caused its owners to lose their lives,
kama nimekula mazao yake bila malipo, au kuvunja mioyo ya wapangaji wake,
40 then let thorns grow instead of wheat and weeds instead of barley.” The words of Job are finished.
basi miiba na iote badala ya ngano, na magugu badala ya shayiri.” Mwisho wa maneno ya Ayubu.

< Job 31 >