< John 8 >

1 But Jesus went [with us disciples] to Olive [Tree] Hill [and we stayed near there that night].
Lakini Yesu akaenda katika Mlima wa Mizeituni.
2 Early the next morning, we returned to the Temple [courtyard]. Many people gathered around Jesus, so he sat down to teach them.
Alfajiri na mapema Yesu akaja tena Hekaluni, watu wote wakakusanyika, akakaa akaanza kuwafundisha.
3 Then men who taught the [Jewish] laws and some of [SYN] the Pharisee [religious group] brought a woman to him. She was seized {[They] had [arranged to] seize her} while she was having sex with a man who was not her husband. They made her stand up in front of the group [that was listening to Jesus].
Walimu wa sheria na Mafarisayo wakamleta mwanamke mmoja aliyefumaniwa akizini. Wakamsimamisha katikati ya umati wa watu wote.
4 Then they said to Jesus, “Teacher, this woman was seized {[we] seized this woman} while she was having sex with a man who is not her husband.
Wakamwambia Yesu, “Mwalimu, huyu mwanamke amekutwa akizini.
5 Moses commanded us in the laws that [he gave us] that we should throw stones at such women [and kill them]. So what do you say [we should do]?”
Katika sheria, Mose alituamuru kuwapiga kwa mawe wanawake wa namna hii, mpaka wafe. Sasa wewe wasemaje?”
6 They asked this question as a trap so that they could accuse him. [If he said that they should not kill her, they would shame him for disobeying the law of Moses. If he said that they should kill her, they could accuse him to the Roman governor]. But Jesus bent down and wrote something on the ground with his finger.
Walimuuliza swali hili kama mtego ili wapate sababu ya kumshtaki. Lakini Yesu akainama akaanza kuandika ardhini kwa kidole chake.
7 While they continued to question him, he stood up and said to them, “Whichever one of you has never sinned can be the first one to start throwing stones at her.”
Walipoendelea kumuulizauliza akainuka, akawaambia, “Kama kuna mtu yeyote miongoni mwenu ambaye hana dhambi na awe wa kwanza kumtupia jiwe.”
8 Then he stooped down and wrote [some more] on the ground.
Akainama tena na kuandika ardhini.
9 After they heard what he said, those [who were questioning him] went away, one by one, the older ones first [and then the younger ones, knowing they were all sinners]. Finally only Jesus was there, along with the woman.
Waliposikia haya, wakaanza kuondoka mmoja mmoja, wakianzia wazee, hadi Yesu akabaki peke yake na yule mwanamke akiwa amesimama mbele yake.
10 Jesus stood up and asked her, “Woman, where are they? Has no one said you must die for your sin?”
Yesu akainuka na kumwambia, “Wako wapi wale waliokuwa wanakuhukumu kuwa mwenye hatia?”
11 She said, “No, sir, no one.” Then Jesus said, “I do not condemn you either. Go [home] now, and do not continue your sinful [life] any longer!”]
Yule mwanamke akajibu, “Hakuna hata mmoja Bwana.” Yesu akamwambia, “Hata mimi sikuhukumu. Nenda zako, kuanzia sasa usitende dhambi tena.”]
12 Jesus spoke to the people again. He said, “I am [like] a light [MET] for [all the people in] [MTY] the world. [Just like a light reveals what has been in the darkness] [MET], [I reveal God’s truth to them]. Those who walk in the darkness [are unaware of what is around them]. But those who become my disciples will always be aware [of God’s truth] [MET]. They will have my light [which shows them how to have eternal] life.”
Kisha Yesu akasema nao tena akawaambia, “Mimi ni nuru ya ulimwengu. Mtu yeyote akinifuata hatatembea gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.”
13 So the Pharisees said to him, “You are just telling about yourself! [Since there is no one else to verify these things that you say about yourself], [we] do not [need to accept that] what you say is true.”
Mafarisayo wakamwambia, “Ushuhuda wako haukubaliki kwa kuwa unajishuhudia mwenyewe.”
14 Jesus replied, “Even if I were the [only one to] say these things about myself, what I say is true, because I know that I came from [heaven], and I know that I am going [back to heaven]. But you do not know where I came from or where I am going.
Yesu akawajibu, “Hata kama najishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu ni kweli kwa sababu najua nilikotoka na ninakokwenda. Lakini ninyi hamjui nilikotoka wala ninakokwenda.
15 You judge people according to human standards. [The reason] that I am [here is] not (to condemn people/to say that I will punish people) [for their sins].
Ninyi mnahukumu kwa kufuata vipimo vya kibinadamu, mimi simhukumu mtu yeyote.
16 But if I did judge [people], what I decided would be correct, because I am not the [only] one [who will decide those things]. I and the one who sent me will both decide.
Lakini hata kama nikihukumu, uamuzi wangu ni sahihi kwa sababu sitoi hukumu yangu peke yangu, bali niko pamoja na Baba, aliyenituma.
17 It is written {[Moses] wrote} in your law that if [at least] two people testify that [some event has happened], [people should consider] that what they say is true.
Imeandikwa katika Sheria yenu kwamba, ushahidi wa watu wawili ni thabiti.
18 I am telling you about myself, and the other one who is telling you about me is [my] Father who sent me. [So you should believe that what we declare is true].”
Mimi najishuhudia mwenyewe, naye Baba aliyenituma hunishuhudia.”
19 Then they asked him, “[If you have a] father whom [we can question about you], where is he?” Jesus replied, “You do not know [who] I [really am]. If you knew who I [really am], you would know who my Father is also.”
Ndipo wakamuuliza, “Huyo Baba yako yuko wapi?” Yesu akawajibu, “Ninyi hamnifahamu mimi ni nani, wala hammfahamu Baba yangu. Kama mngenifahamu mimi, mngemfahamu na Baba yangu.”
20 He said these things when he was in the Temple [courtyard], near the place where the people put their offerings. [This was also very close to the place where the Jewish council met]. But no one seized him to arrest him, because it was not yet time [MTY] [for him to suffer and die].
Yesu alisema maneno haya alipokuwa akifundisha katika chumba cha hazina Hekaluni. Lakini hakuna mtu aliyemkamata kwa kuwa saa yake ilikuwa haijawadia.
21 Jesus also said to them, “I [will soon be] going away. Then [at the end of your life] you will seek me, but you will die [without God forgiving] your sins. Where I will go, you will not be able to come.”
Yesu akawaambia tena, “Ninaenda zangu, nanyi mtanitafuta, lakini mtakufa katika dhambi zenu. Niendako mimi ninyi hamwezi kuja.”
22 So the Jewish [leaders] said among themselves, “Is he going to kill himself? Is that the reason that he said, ‘Where I go, you will not be able to come’?”
Ndipo wale Wayahudi wakasema, “Je, atajiua? Je, hii ndiyo sababu amesema, ‘Niendako mimi ninyi hamwezi kuja’?”
23 But Jesus continued by saying to them, “You were born here in this world, but I came from heaven. You belong to those who are opposed to God [MTY]. I do not belong to them.
Akawaambia, “Ninyi mmetoka chini, mimi nimetoka juu. Ninyi ni wa ulimwengu huu, mimi si wa ulimwengu huu.
24 I told you that you will die [without God forgiving] your sins. If you do not believe that I am [who I say that I am], you will die [without God forgiving] your sins.”
Niliwaambia kuwa mtakufa katika dhambi zenu, kwa maana msipoamini ya kwamba ‘Mimi Ndiye,’ mtakufa katika dhambi zenu.”
25 So they said to him, “You! Who do you think you are?” Jesus said to them, “Ever since I began [teaching], I have been telling you who I am!
Wakamuuliza, “Wewe ni nani?” Naye Yesu akawajibu, “Mimi ndiye yule ambaye nimekuwa nikiwaambia tangu mwanzo.
26 I could judge you and say that [you are guilty of] many things. But instead, [I will say only] what the one who sent me tells me to say. [What he says] is true, and I tell the people in the world [MTY] what I have heard from him.”
Nina mambo mengi ya kusema juu yenu na mengi ya kuwahukumu. Lakini yeye aliyenituma ni wa kweli, nami nanena na ulimwengu niliyoyasikia kutoka kwake.”
27 They did not understand that he was talking about his Father [in heaven].
Hawakuelewa kuwa alikuwa akiwaambia juu ya Baba yake wa Mbinguni.
28 So Jesus said, “I am the one who came down from heaven, but when you lift me up [on a cross to kill me], you will know who I am. You will also know that I do not do anything with my own [authority]. Instead, I say just what [my] Father has taught me.
Kisha Yesu akawaambia, “Mtakapokwisha kumwinua juu Mwana wa Adamu, ndipo mtakapojua kuwa, ‘Mimi ndiye yule niliyesema na kwamba mimi sitendi jambo lolote peke yangu bali ninasema yale tu ambayo Baba yangu amenifundisha.
29 He is the one who sent me, and he helps me. Because I always do the things that please him, he has never abandoned me.”
Yeye aliyenituma yu pamoja nami, hajaniacha, kwa kuwa siku zote nafanya mapenzi yake.’”
30 As Jesus was saying these things, many people believed that he [was] ([from God/the Messiah]).
Wengi waliomsikia Yesu akisema maneno haya wakamwamini.
31 Then Jesus said to the Jews who now said they believed in him, “If you continue to [live in accordance with] my message, you will truly be my disciples.
Kisha Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, “Kama mkidumu katika maneno yangu, mtakuwa wanafunzi wangu kweli kweli.
32 Then you will know [God’s] truth, and as a result of [your believing his] truth, he [PRS] will free you [from being controlled by the one who has made you his slaves].”
Ndipo mtaijua kweli nayo kweli itawaweka huru.”
33 They replied to him, “We are descendants of Abraham. We have never been anyone’s slaves. So why do you say [we will] be freed [from being someone’s slaves]?”
Wao wakamjibu, “Sisi tu wazao wa Abrahamu, nasi hatujawa watumwa wa mtu yeyote. Wawezaje kusema kwamba tutawekwa huru?”
34 Jesus replied, “Listen carefully to what I am going to tell you. All those who continue to sin are [forced to obey] their sinful desires [MET], [just like] a slave [is forced to obey his master].
Yesu akajibu, “Amin, amin nawaambia, kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi.
35 A slave is not a permanent member of a family. But a son is a member of a family forever. [Similarly, you say you are members of God’s family because you are descendants of Abraham, but really, because you are like slaves of your sinful desires, you are no longer permanent members of God’s family]. (aiōn g165)
Mtumwa hakai nyumbani anakotumika siku zote, lakini mwana hukaa nyumbani daima. (aiōn g165)
36 So if you allow me to free you, you will truly be free.
Hivyo Mwana akiwaweka huru mtakuwa huru kweli kweli.
37 I know that you are Abraham’s descendants. But you are trying to kill me because [you are not] allowing [PRS] my message to continue [to change] your inner being.
Ninajua ya kuwa ninyi ni wazao wa Abrahamu, lakini mnatafuta wasaa wa kuniua kwa sababu ndani yenu hamna nafasi ya neno langu.
38 I am telling you what I saw when I was with [my] Father. But you do the things that you have heard from your father.”
Ninasema yale niliyoyaona mbele za Baba yangu, nanyi inawapa kufanya yale mliyosikia kutoka kwa baba yenu.”
39 They replied to him, “Abraham is our ancestor.” Jesus said to them, “If you were Abraham’s descendants, [your character would be like Abraham’s character, and] you would do [good] things like Abraham did.
Wakajibu, “Baba yetu ni Abrahamu.” Yesu akawaambia, “Kama mngekuwa wazao wa Abrahamu mngefanya mambo yale aliyofanya Abrahamu.
40 I have been telling you the truth that I heard from God, but you are trying to kill me. Abraham did not do things like that.
Lakini sasa ninyi mnatafuta kuniua, mtu ambaye nimewaambia kweli ile niliyosikia kutoka kwa Mungu, Abrahamu hakufanya jambo la namna hii.
41 No! You are doing the things that your [real] father does.” They said to him, “[We do not know about you, but] we are not illegitimate children. And [spiritually], we have only one Father. That is God, and you do not know who your father is!”
Ninyi mnafanya mambo afanyayo baba yenu.” Wakamjibu, “Sisi hatukuzaliwa kwa uzinzi. Tunaye Baba mmoja, Mungu pekee.”
42 Jesus said to them, “If God were your father, you would love me, because I came from God, and now I have come here [to this world]. My coming was not (because I [appointed] myself/with my own [authority]). He sent me.
Yesu akawaambia, “Kama Mungu angekuwa Baba yenu, mngenipenda, kwa maana nilitoka kwa Mungu na sasa niko hapa. Sikuja kwa ajili yangu mwenyewe, ila yeye alinituma.
43 (And I will tell you why you do not understand what I say./Do you know why you do not understand what I say?) [RHQ] It is because you do not want to accept my message.
Kwa nini hamwelewi ninayowaambia? Ni kwa sababu hamwezi kusikia nisemacho.
44 You belong to your father, (the devil/Satan), and you desire to do what he wants. He has [caused people to become] murderers from the time when [people] first [sinned]. He has abandoned [God’s] truth because he is a liar by his nature. Whenever he lies, he is speaking according to his [nature], because he is a liar and is the one who originates [MET] all lies.
Ninyi ni watoto wa baba yenu ibilisi, nanyi mnataka kutimiza matakwa ya baba yenu. Yeye alikuwa muuaji tangu mwanzo, wala hakushikana na kweli maana hamna kweli ndani yake. Asemapo uongo husema yaliyo yake mwenyewe kwa maana yeye ni mwongo na baba wa huo uongo.
45 But because I tell you the truth, you do not believe me!
Lakini kwa sababu nimewaambia kweli hamkuniamini!
46 [Since I have never sinned], (none of you can show that I have sinned./can anyone among you show that I have sinned?) [RHQ] So, since I tell you the truth, (there is no good reason for your not believing me!/why is it that you do not believe me?) [RHQ]
Je, kuna yeyote miongoni mwenu awezaye kunithibitisha kuwa mwenye dhambi? Kama nawaambia yaliyo kweli, mbona hamniamini?
47 Those who belong to God habitually obey God’s message. You do not belong to God, so you do not obey his message.”
Yeye atokaye kwa Mungu husikia kile Mungu asemacho. Sababu ya ninyi kutosikia ni kwa kuwa hamtokani na Mungu.”
48 The Jewish [leaders] [SYN] replied to him, “(We are certainly right by saying that you [believe what is false as] the Samaritans [do]!/Are we not right by saying that you [believe what is false as] the Samaritans [do]?) [RHQ] And that (a demon/an evil spirit) [controls] you!”
Wayahudi wakamjibu Yesu, “Je, hatuko sahihi tunaposema ya kwamba wewe ni Msamaria na ya kwamba una pepo mchafu?”
49 Jesus replied, “A demon does not [control] me! I honor my Father, and you do not honor me!
Yesu akawajibu, “Mimi sina pepo mchafu, bali ninamheshimu Baba yangu, nanyi mnanidharau.
50 I am not trying to honor myself. There is someone else who desires [to honor me], and he is the one who will judge [whether it is I who am telling the truth or whether it is you who are telling the truth].
Lakini mimi sitafuti utukufu wangu mwenyewe, bali yuko anayetaka kunitukuza, naye ndiye mwamuzi.
51 But the truth is that anyone who obeys what I say will never die!” (aiōn g165)
Amin, amin nawaambia, mtu yeyote akilitii neno langu hataona mauti milele.” (aiōn g165)
52 Then the Jewish [leaders] [SYN], [thinking that he was talking about ordinary death and not about spiritual death], said to him, “Now we are sure that a demon [controls] you! Abraham and the prophets died [long ago]! But you say that anyone who obeys what you teach will never die! (aiōn g165)
Ndipo Wayahudi wakamwambia, “Sasa tumejua kwamba una pepo mchafu. Ikiwa Abrahamu alikufa na vivyo hivyo manabii, nawe unasema ‘Mtu akitii neno langu hatakufa milele.’ (aiōn g165)
53 (You are certainly not greater than our ancestor Abraham!/Do you think you are greater than our ancestor Abraham?) [RHQ] He died, and all the prophets died, so who do you think you are [by saying something like that]?”
Je, wewe ni mkuu kuliko baba yetu Abrahamu ambaye alikufa na manabii ambao nao pia walikufa? Hivi wewe unajifanya kuwa nani?”
54 Jesus replied, “If I were honoring myself, that would be worthless. My Father is the one who you say is your God. He is the one who honors me.
Yesu akawajibu, “Kama nikijitukuza utukufu wangu hauna maana. Baba yangu, huyo ambaye ninyi mnadai kuwa ni Mungu wenu, ndiye anitukuzaye mimi.
55 Although you do not know him, I know him [and have a close relationship with him]. If I said that I did not know him, I would be a liar like you are. But I know him, and I obey what he says.
Ingawa hamkumjua, mimi ninamjua. Kama ningesema simjui, ningekuwa mwongo kama ninyi, lakini mimi ninamjua na ninalitii neno lake.
56 Your ancestor Abraham was happy when he thought about what I would [do during] my life [MTY]. [It was as though] he saw that, and was happy.”
Baba yenu Abrahamu alishangilia kwamba angaliiona siku yangu, naye akaiona na akafurahi.”
57 Then the Jewish [leaders] [SYN] said to him, “You are not 50 years old yet! So (you certainly did not see him!/how could you have seen him?) [RHQ] [Because he died long ago]!”
Wayahudi wakamwambia, “Wewe hujatimiza hata miaka hamsini, wewe wasema umemwona Abrahamu?”
58 Jesus said to them, “The truth is that I existed before Abraham was born!”
Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia, kabla Abrahamu hajakuwako, ‘Mimi niko.’”
59 So, [because they were very angry about Jesus thus saying that he] ([had eternally existed/was equal with God]), they picked up stones to throw at him [to kill him]. But [Jesus] caused them not to be able to see him, and he left the Temple courtyard.
Ndipo wakaokota mawe ili kumpiga, lakini Yesu akajificha, naye akatoka Hekaluni.

< John 8 >