< Luke 1 >

1 My noble [friend] Theophilus, many people saw the things that [Jesus] did while he was with us, from the time when he started [MTY] [his ministry]. They served God [by teaching people] the message [about the Lord Jesus]. Many of those who heard what they taught wrote down for us accounts of the things that [Jesus did from the time when] he began [his ministry].
Kwa kuwa watu wengi wamekaa ili kuandika habari za mambo yaliyotukia katikati yetu,
2
kama vile yalivyokabidhiwa kwetu na wale waliokuwa mashahidi walioyaona na watumishi wa Bwana,
3 I myself have studied these accounts carefully. So I decided that it would be good for me also to write for you [(sg)] an accurate account of these matters.
mimi nami baada ya kuchunguza kila kitu kwa uangalifu kuanzia mwanzo, niliamua kukuandikia habari za mambo hayo, ewe mtukufu Theofilo,
4 I want you to know the truth about what you have been taught {what others have taught you}.
ili upate kujua ukweli kuhusu yale uliyofundishwa.
5 When King Herod [the Great ruled] Judea [district], there was a [Jewish] priest named Zechariah. He belonged to the [group of priests called] the Abijah group. He and his wife Elizabeth were both descended from the [first priest of Israel], Aaron.
Wakati wa Herode mfalme wa Uyahudi, palikuwa na kuhani mmoja jina lake Zekaria, ambaye alikuwa wa ukoo wa kikuhani wa Abiya. Elizabeti mkewe alikuwa pia mzao wa Aroni.
6 [God considered that] both of them were righteous, because they constantly completely obeyed everything that God had commanded.
Zekaria na Elizabeti mkewe wote walikuwa watu wanyofu mbele za Mungu, wakizishika amri zote za Bwana na maagizo yote bila lawama.
7 But they had no children, because Elizabeth had been unable to bear children. Furthermore, she and her husband were very old.
Lakini walikuwa hawana watoto, kwa sababu Elizabeti alikuwa tasa; nao wote wawili walikuwa wazee sana.
8 One day [Zechariah’s] group was doing their work [in the Temple in Jerusalem], and he was serving as a priest in God’s presence.
Siku moja ilipokuwa zamu ya kikundi cha Zekaria, yeye akifanya kazi ya ukuhani Hekaluni mbele za Mungu,
9 Following their custom, [the other priests] chose him by lot to enter the Lord’s temple and burn incense.
alichaguliwa kwa kura kwa kufuata desturi za ukuhani, kuingia Hekaluni mwa Bwana ili kufukiza uvumba.
10 While he was burning the incense, many people were outside [in the courtyard], praying.
Nao wakati wa kufukiza uvumba ulipowadia, wale wote waliokuwa wamekusanyika ili kuabudu walikuwa nje wakiomba.
11 Then an angel whom God had [sent] appeared to him. The angel was standing at the right side of the place [where the priests burned] incense.
Ndipo malaika wa Bwana, akiwa amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia uvumba, akamtokea Zekaria.
12 When Zechariah saw the angel, he was startled and became very afraid.
Zekaria alipomwona huyo malaika, akafadhaika sana, akajawa na hofu.
13 But the angel said to him, “Zechariah, do not be afraid! When you [(sg)] prayed [asking God for a son] (OR, [that God would send the Messiah]), God heard what you prayed. [So] your wife Elizabeth shall bear a son. You must name him John.
Lakini malaika akamwambia, “Usiogope, Zekaria, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Mkeo Elizabeti atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utamwita jina lake Yohana.
14 He will cause you to be very happy, and many other people will also be happy because he is born.
Yeye atakuwa furaha na shangwe kwako, nao watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
15 God will consider him to be very important. He must never drink wine or any other alcoholic drink, [in order that he will be completely dedicated to God]. He will be controlled by the Holy Spirit {The Holy Spirit will control him} from before he is born.
Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele za Bwana, kamwe hataonja mvinyo wala kinywaji chochote cha kulevya, naye atajazwa Roho Mtakatifu hata kabla ya kuzaliwa kwake.
16 He will [persuade] many people in Israel to turn away [from their sins and please] the Lord their God.
Naye atawageuza wengi wa wana wa Israeli warudi kwa Bwana Mungu wao.
17 As [God’s] Spirit enables him [to preach] powerfully as [the prophet] Elijah did, he will precede [the Messiah]. He will cause parents [SYN] to act [peacefully] toward their children [again]. He will cause [many] people who do not obey [God to hear and obey] the wise things that righteous people [tell them]. He will do this in order to help [many] people to be ready when the Lord [comes].”
Naye atatangulia mbele za Bwana katika roho na nguvu ya Eliya, ili kuigeuza mioyo ya baba kuwaelekea watoto wao, na wasiotii warejee katika hekima ya wenye haki, ili kuliweka tayari taifa lililoandaliwa kwa ajili ya Bwana.”
18 Then Zechariah said to the angel, “I am very old, and my wife is also so old [that she cannot bear a child. So] (I cannot [believe] that what you [(sg)] said [will happen]!/how can I [believe] that what you [(sg)] said [will happen]?) [RHQ]”
Zekaria akamuuliza malaika, “Jambo hilo linawezekanaje? Mimi ni mzee na mke wangu pia ana umri mkubwa.”
19 Then the angel said to him, “I am [God’s chief angel], Gabriel! [I do what God tells me, because] I constantly am in God’s presence! I was sent {[He] sent me} to tell you [(sg)] something good [that is going to happen to you].
Malaika akamjibu, akamwambia, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele za Mungu, nami nimetumwa kwako ili nikuambie habari hizi njema.
20 What I have told you will certainly happen at the time [God decides], but you did not believe what I told you. So now [God will make] you will be unable to talk until the day [your son is born]”!
Basi sasa kwa kuwa hujaamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati wake, utakuwa bubu hadi siku ile mambo haya yatakapotukia.”
21 While [Zechariah and the angel] were talking, the people [in the courtyard] were waiting for Zechariah [to come out]. They wondered, “Why is he staying in the Temple for such a long time?”
Wakati huo watu walikuwa wanamngojea Zekaria nje huku wakishangaa kukawia kwake mle Hekaluni.
22 When Zechariah came out, he was not able to speak to the people. Because he could not talk, he made motions with his hands [to try to convey what had happened]. Then they realized that he had seen (a vision [from God]/something that [God] showed him) while he was in the Temple.
Alipotoka akawa hawezi kusema nao, wao wakatambua kuwa ameona maono ndani ya Hekalu. Lakini kwa kuwa alikuwa bubu, akawa anawaashiria kwa mikono.
23 When Zechariah’s time to work [as a priest in the Temple] was finished, he [left Jerusalem and] returned to his home.
Muda wake wa kuhudumu Hekaluni ulipomalizika, akarudi nyumbani kwake.
24 Some time later his wife Elizabeth became pregnant [EUP]. She did not leave their house for five months, [because she knew that people would laugh at her if she told them that she was pregnant].
Baada ya muda usio mrefu, Elizabeti mkewe akapata mimba, naye akajitenga kwa miezi mitano.
25 But she thought, “God has enabled me to become pregnant. He has pitied me and I will no longer be ashamed [because I have no children]!”
Akasema, “Hili ndilo Bwana alilonitendea aliponiangalia kwa upendeleo na kuniondolea aibu yangu mbele ya watu.”
26 When Elizabeth had been [pregnant] [EUP] [for almost] six months, the angel Gabriel was sent by God {God sent the angel Gabriel} [again].
Mwezi wa sita baada ya Elizabeti kupata mimba, Mungu alimtuma malaika Gabrieli aende Galilaya katika mji wa Nazareti,
27 [This time] he went to Nazareth [town] in Galilee [district], to a virgin whose name was Mary. It had been {[Her parents] had} promised that she would marry a man named Joseph, who was descended from [King] David.
kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu mmoja jina lake Yosefu wa nyumba ya Daudi. Jina la huyu mwanamwali bikira ni Maria.
28 The angel greeted her and said, “(The Lord/God) is with you [(sg)] and you will be greatly blessed {[has decided to] greatly bless you}!”
Naye malaika akaja kwake akamwambia: “Salamu, wewe uliyebarikiwa, Bwana yu pamoja nawe!”
29 But Mary was very confused [when she heard] that. She wondered what [the angel meant] by these words.
Maria akafadhaishwa sana na maneno haya, akajiuliza moyoni, “Salamu hii ni ya namna gani?”
30 Then the angel said to her, “Mary, God is very pleased with you [(sg)], so do not be afraid.
Ndipo malaika akamwambia, “Usiogope, Maria, umepata kibali kwa Mungu.
31 You will become pregnant and bear a son, and you must name him Jesus.
Tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanaume na utamwita jina lake Yesu.
32 He will become great. He will be called {[People will] call him} (the Son of God/the man who is also God). God, the Lord, will make him a king [MTY] as his ancestor [King] David was.
Yeye atakuwa mkuu, naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
33 He will be the King of [the] Jews, the descendants [MTY] of [your ancestor] Jacob, forever. He will rule as king forever!” (aiōn g165)
Ataimiliki nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn g165)
34 Then Mary said to the angel, “I am a virgin, so how can I [have a baby]?”
Maria akamuuliza huyo malaika, “Maadamu mimi ni bikira, jambo hili litawezekanaje?”
35 The angel replied, “The Holy Spirit will come to you; the power of God [MTY/EUP] will overshadow you [and enable you to become pregnant]. So the child [you will] bear will be completely set apart {give himself completely} to obey God, and he will be called {[people] will say that he is} (the Son of God/the man who is also God).
Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, nazo nguvu zake Yeye Aliye Juu Sana zitakufunika kama kivuli. Kwa hiyo mtoto atakayezaliwa atakuwa mtakatifu, naye ataitwa Mwana wa Mungu.
36 [I also need to tell you something else]. Your cousin Elizabeth is very old, and it was thought {[people] said} that she could not bear any children. But she has been [pregnant] [EUP] [for almost] six months, and will bear a son!
Tazama, jamaa yako Elizabeti amechukua mimba katika uzee wake, na huu ni mwezi wake wa sita, yeye aliyeitwa tasa.
37 [You should not be surprised at that], because God can do everything!”
Kwa maana kwa Mungu hakuna lisilowezekana.”
38 Then Mary said, “All right, I want to serve (the Lord/God), so may what you [(sg)] have said about me come true!” Then the angel left her.
Maria akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa Bwana. Na iwe kwangu kama ulivyosema.” Kisha malaika akaondoka, akamwacha.
39 Very soon after that, Mary got ready and went quickly to a town in the highlands of Judea [district] where Zechariah lived.
Wakati huo Maria akajiandaa, akaharakisha kwenda katika mji mmoja kwenye vilima vya Uyahudi.
40 She entered his house and greeted [his wife] Elizabeth.
Akaingia nyumbani kwa Zekaria na kumsalimu Elizabeti.
41 As soon as Elizabeth heard Mary greet her, the baby moved inside [Elizabeth’s] womb. The Holy Spirit took complete control of Elizabeth,
Naye Elizabeti aliposikia salamu ya Maria, mtoto aliyekuwa tumboni mwake akaruka. Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu,
42 and she said loudly [to Mary], “[God] has blessed you [more than] he has blessed [any other] woman, and [he has] blessed the child you will bear!
akapaza sauti kwa nguvu akasema, “Umebarikiwa wewe miongoni mwa wanawake, naye mtoto utakayemzaa amebarikiwa.
43 (I am not worthy that [God would allow you] to visit me!/Why is [God allowing you] to visit me?) [RHQ] You will be the mother of my Lord!
Lakini ni kwa nini mimi nimepata upendeleo kiasi hiki, hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
44 [I realize this because] as soon as I heard you greet me, the baby inside my womb moved because he was so happy [that you had come].
Mara tu niliposikia sauti ya salamu yako, mtoto aliyeko tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
45 [God] is pleased with you [because] you believed that what (the Lord/God) told you would come true.”
Amebarikiwa yeye aliyeamini kwamba lile Bwana alilomwambia litatimizwa.”
46 Then Mary [praised God by] saying/singing: “, how I [SYN] praise (the Lord/God)!
Naye Maria akasema: “Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
47 I am happy because God is the one who saves me.
nayo roho yangu inamfurahia Mungu Mwokozi wangu,
48 I was only his lowly servant girl, but he did not forget me. So from now on, everyone will say that God was pleased with me,
kwa kuwa ameangalia kwa fadhili unyonge wa mtumishi wake. Hakika tangu sasa vizazi vyote vitaniita aliyebarikiwa,
49 because they will hear about the things that God [MTY], the mighty one, has done for me. He [MTY] is awesome!
kwa maana yeye Mwenye Nguvu amenitendea mambo ya ajabu: jina lake ni takatifu.
50 He acts mercifully toward all those who respect him.
Rehema zake huwaendea wale wamchao, kutoka kizazi hadi kizazi.
51 He shows people that he [MTY] is very powerful. He scatters those who think proudly.
Kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu kwa mkono wake; amewatawanya wale wenye kiburi ndani ya mioyo yao.
52 He does not let mighty kings rule [MTY] any more, but he honors people who are oppressed (OR, humble).
Amewashusha watawala toka kwenye viti vyao vya enzi, lakini amewainua wanyenyekevu.
53 He gives good things to eat to those who are hungry, but he sends away the rich people without giving them anything.
Amewashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
54 And now he has remembered what he promised. So he has helped me and all the other people of [MTY] Israel who serve him.
Amemsaidia mtumishi wake Israeli, kwa kukumbuka ahadi yake ya kumrehemu
55 He promised to Abraham and all our other ancestors who descended from him that he would act mercifully toward them forever.” (aiōn g165)
Abrahamu na uzao wake milele, kama alivyowaahidi baba zetu.” (aiōn g165)
56 Mary stayed with Elizabeth for about three months. Then she returned to her home.
Maria akakaa na Elizabeti karibu miezi mitatu, kisha akarudi nyumbani kwake.
57 When it was time for Elizabeth to give birth to her child, she bore a son.
Ulipowadia wakati wa Elizabeti kujifungua, alizaa mtoto mwanaume.
58 Her neighbors and relatives heard how (the Lord/God) had greatly blessed her [by enabling her to bear a child], so they were happy along with [Elizabeth].
Majirani zake na jamii zake wakasikia jinsi Bwana alivyomfanyia rehema kuu, nao wakafurahi pamoja naye.
59 Seven days later they gathered together for the [ceremony for] circumcising the baby [to show that he belonged to God]. They wanted to give the baby the same name as his father, Zechariah.
Siku ya nane wakaja kumtahiri mtoto, wakataka yule mtoto aitwe Zekaria, ambalo ndilo jina la baba yake.
60 But his mother said, “No, [his name will not be Zechariah]. His name will be John!”
Lakini mama yake akakataa na kusema, “Hapana! Jina lake ataitwa Yohana.”
61 [So] they said to her, “[John] is not the name of any of your [(dl)] relatives, [so you(dl) should not give him that name]!”
Wakamwambia, “Hakuna mtu yeyote katika jamaa yako mwenye jina kama hilo.”
62 Then they made motions with their hands to Zechariah, [for him] to indicate what name [he] wanted to be given {to give} to his son.
Basi wakamfanyia Zekaria baba yake ishara ili kujua kwamba yeye angependa kumpa mtoto jina gani.
63 [So] he signaled that they [should give him] a tablet [to write on. When they gave him one], he wrote [on it], “His name is John.” All those [who were there] were surprised!
Akaomba wampe kibao cha kuandikia na kwa mshangao wa kila mtu akaandika: “Jina lake ni Yohana.”
64 Immediately Zechariah was able to speak again [MTY], and he praised God.
Papo hapo kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake ukaachiwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
65 All their neighbors were amazed/awestruck! They told other people who lived all over the highlands of Judea about what had happened.
Majirani wote wakajawa na hofu ya Mungu, na katika nchi yote ya vilima vya Uyahudi watu walikuwa wakinena juu ya mambo haya yote.
66 Everyone who heard about it kept thinking about it. They were saying, “We wonder what will this child do [for God when] he [grows up] [RHQ]!” They wondered that because [from what had happened they were sure that] God would be helping that child [SYN] [in a powerful way].
Kila aliyesikia habari hizi alishangaa akauliza, “Je, mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
67 [After] Zechariah’s [son was born], Zechariah was completely directed by the Holy Spirit {the Holy Spirit completely directed Zechariah} as he spoke these words that came from God:
Zekaria, baba yake, akajazwa na Roho Mtakatifu, naye akatoa unabii, akisema:
68 “Praise the Lord, the God whom we(inc) people of Israel worship, because he has come to set us, his people, free from our enemies.
“Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.
69 He is sending us someone who will powerfully [MTY] save us, someone who is descended from [MTY] King David, who served God well.
Naye ametusimamishia pembe ya wokovu katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,
70 Long ago God caused his prophets to say that he would do that. (aiōn g165)
kama alivyonena kwa vinywa vya manabii wake watakatifu tangu zamani, (aiōn g165)
71 He will rescue us from our enemies, and he will save us from the power of all those who hate us.
kwamba atatuokoa kutoka kwa adui zetu, na kutoka mikononi mwao wote watuchukiao:
72 He will do this because he has not forgotten what he promised our ancestors; he made an agreement that he would act mercifully to us, their descendants.
ili kuonyesha rehema kwa baba zetu na kukumbuka Agano lake takatifu,
73 That is what he strongly promised our ancestor Abraham that he would do.
kiapo alichomwapia baba yetu Abrahamu:
74 God told him that we would be rescued {he would rescue us} from the power of our enemies, that he would enable us to serve him without being afraid,
kutuokoa kutoka mikononi mwa adui zetu, tupate kumtumikia yeye pasipo hofu
75 that he would cause us to be completely dedicated to him, and enable us to live righteously all of our lives.”
katika utakatifu na haki mbele zake, siku zetu zote.
76 [Then Zechariah said this to] his little son: “My child, you will be called {people will say that you are} a prophet whom God [MTY/EUP] has sent; you will begin your work before (the Lord/Messiah) comes; you will prepare people so that they will be ready for him. (OR, you will begin your work before the Messiah comes).
“Nawe mtoto wangu, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana; kwa kuwa utamtangulia Bwana na kuandaa njia kwa ajili yake,
77 You will tell God’s people how he will forgive them and save them from being punished for their sins.
kuwajulisha watu wake juu ya wokovu utakaopatikana kwa kusamehewa dhambi zao,
78 Our God will do that because he is very kind to us. Just like a new day begins when the sun rises [MET], God will do that new thing for us when the Messiah comes to us from heaven.
kwa ajili ya wingi wa rehema za Mungu wetu, nuru itokayo juu itatuzukia
79 People who do not know God [MET] are like those who sit in the darkness. They are afraid [MTY] that they will soon die. But when the Messiah tells us God’s message, it will be like causing such people to see a bright light. He will guide us [SYN] so that we will be living peacefully.”
ili kuwaangazia wale waishio gizani na katika uvuli wa mauti, kuiongoza miguu yetu katika njia ya amani.”
80 [Later], Zechariah’s son grew up and became spiritually strong. Then he lived in a desolate region until he began to preach to the Israeli people.
Yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu katika roho; akaishi nyikani hadi siku ile alipojionyesha hadharani kwa Waisraeli.

< Luke 1 >