< Exodus 3 >

1 Moses/I was taking care of the sheep that belonged to his/my father-in-law Jethro, the priest of the Midian [people]. He/I led the flock across the desert and came to Horeb, [the mountain that was later called Sinai], the (mountain that [had been dedicated to] God/taboo mountain).
Basi Mose alikuwa anachunga mifugo ya Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani. Mose akapeleka mifugo mbali nyuma ya jangwa, naye akafika Horebu, mlima wa Mungu.
2 [One day] Yahweh (appeared/revealed himself) to him/me, [looking like] an angel. The angel appeared in a flame of fire in the middle of a bush [that was burning]. Moses/I looked at it, and he/I was surprised that the bush was burning, but it was not burning up.
Huko malaika wa Bwana akamtokea Mose katika mwali wa moto kutoka kichakani. Mose akaona kwamba ingawa kile kichaka kilikuwa kinawaka moto, kilikuwa hakiteketei.
3 Moses/I thought, “I will go closer and try to see this strange sight! Why is the bush not burning up?”
Ndipo Mose akawaza, “Nitageuka sasa nione kitu hiki cha ajabu, nami nione ni kwa nini kichaka hiki hakiteketei.”
4 When Yahweh saw that he/I had come closer, he called to Moses/me from the middle of the bush, saying, “Moses! Moses!” He/I replied, “[Yes], here I am.”
Bwana alipoona kuwa amegeuka ili aone, Mungu akamwita kutoka ndani ya kile kichaka, “Mose! Mose!” Naye Mose akajibu, “Mimi hapa.”
5 Yahweh said, “Do not come closer! [Because I am God], the ground on which you are standing is holy/taboo. So take off your sandals [to show respect to me].”
Mungu akamwambia, “Usikaribie zaidi. Vua viatu vyako, kwa maana mahali unaposimama ni patakatifu.”
6 Then he said, “I am God, whom your ancestors Abraham, Isaac, and Jacob [worshiped].” So Moses/I covered his/my face, because he/I was afraid [that God would kill him/me] if he/I looked at him.
Kisha akamwambia, “Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo.” Mose aliposikia hayo, akafunika uso wake kwa sababu aliogopa kumtazama Mungu.
7 Then Yahweh said, “I have seen how cruelly [they are treating] my people in Egypt. I have heard them (wailing/crying out) [for help] because of what the slave-drivers [are forcing them to do]. I know how my people are suffering.
Bwana akamwambia, “Hakika nimeona mateso ya watu wangu katika Misri. Nimesikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao, nami naguswa na mateso yao.
8 So I have come down [from heaven] to rescue them from the Egyptians [SYN]. I have come to bring them up from that land [to the highlands in Canaan]. I will bring them to a land that is good/fertile and that has plenty of space. It will be very good for raising livestock and growing crops [MTY]. It is the land where the descendants of Canaan, Heth, Amor, Periz, Hiv, and Jebus [live].
Basi nimeshuka niwaokoe kutoka mkono wa Wamisri, niwatoe na kuwapandisha kutoka nchi hiyo, niwapeleke katika nchi nzuri na kubwa, nchi itiririkayo maziwa na asali, nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
9 Truly I have now heard my Israeli people crying [PRS]. I have seen how the Egyptians oppress them.
Sasa kilio cha Waisraeli kimenifikia, nami nimeona jinsi Wamisri wanavyowatesa.
10 So you go [back] to Egypt. I am sending you to the king, in order that [he may permit] you to bring my people, the Israeli people, out of Egypt.”
Basi, sasa nenda. Ninakutuma kwa Farao ili kuwatoa watu wangu Waisraeli kutoka Misri.”
11 But Moses/I replied, “I am not a well-known person [RHQ]! (I cannot go to the king and [ask him to permit me] to bring the Israeli people out of Egypt!/How can I go to the king and [ask him to allow me to] bring the Israeli people out of Egypt?)” [RHQ]
Lakini Mose akamwambia Mungu, “Mimi ni nani hata niende kwa Farao kuwatoa Waisraeli nchini Misri?”
12 God replied, “I will be with you. And when you bring [my] people out of Egypt, all of you will worship me [right] here on this mountain. That will prove that I am the one who sent you [to them].”
Naye Mungu akasema, “Mimi nitakuwa pamoja nawe. Hii itakuwa ishara kwako kwamba ni Mimi nimekutuma: Hapo utakapokuwa umewatoa watu Misri, mtamwabudu Mungu katika mlima huu.”
13 Moses/I said to God, “If I go to the Israeli people and say to them, ‘God, the one your ancestors [worshiped], has sent me to you,’ and they ask me, ‘What is his name?’, what shall I say to them?”
Mose akamwambia Mungu, “Ikiwa nitawaendea Waisraeli na kuwaambia, ‘Mungu wa baba zenu amenituma kwenu,’ nao wakiniuliza, ‘Jina lake ni nani?’ Nitawaambia nini?”
14 God replied, “I AM who I AM.” And he said, “Tell the Israeli people that the one who is [named] ‘I AM’ has sent me to you.”
Mungu akamwambia Mose, “Mimi niko ambaye niko. Hivyo ndivyo utakavyowaambia Waisraeli: ‘Mimi niko amenituma kwenu.’”
15 God also said to Moses/me, “Say this to the Israeli people: ‘Yahweh God, the one your ancestors [worshiped], the one that Abraham and Isaac and Jacob [worshiped], has sent me to you.’ This name, [Yahweh], will be my name forever. That is the name that [people in] all future generations [must use when they talk about/to] me.
Vilevile Mungu akamwambia Mose, “Waambie Waisraeli, ‘Bwana, Mungu wa baba zenu, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo amenituma kwenu.’ Hili ndilo Jina langu milele, Jina ambalo mtanikumbuka kwalo kutoka kizazi hadi kizazi.
16 Go [to Egypt] and gather together the elders/leaders of the Israeli people, and say to them, ‘Yahweh God, the one your ancestors [worshiped], the one Abraham, Isaac, and Jacob [worshiped], appeared to me. He said to him/me, “I have been watching closely what the Egyptian people have done to you.
“Nenda, ukawakusanye wazee wa Israeli, uwaambie, ‘Bwana, Mungu wa baba zenu, Mungu wa Abrahamu, Isaki na Yakobo, alinitokea akaniambia: Nimewatazama, nami nimeona mliyofanyiwa katika Misri.
17 I promise that I will rescue you from being oppressed in Egypt, and [I will take you] to the land where the descendants of Canaan, Heth, Amor, Periz, Hiv, and Jebus [live]. It is a land good for raising livestock and growing crops [MTY].”’
Nami nimeahidi kuwapandisha kutoka mateso yenu katika nchi ya Misri, niwapeleke nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi, nchi itiririkayo maziwa na asali.’
18 My people will do what you say. Then you and their leaders must go to the king of Egypt, and you must say to him, ‘Yahweh, who is God, the one we Hebrews [worship], has revealed himself to us. So now we ask you to allow us to travel for three days to [a place in] the desert, in order that there we may offer sacrifices to Yahweh, our God.’
“Wazee wa Israeli watakusikiliza. Kisha wewe na wazee mtakwenda kwa mfalme wa Misri na kumwambia, ‘Bwana, Mungu wa Waebrania ametutokea. Turuhusu twende safari ya siku tatu huko jangwani kutoa dhabihu kwa Bwana Mungu wetu.’
19 But I know that the king of Egypt will allow you to go only if he realizes I am [more] powerful [MTY] [than he is].
Lakini nafahamu kwamba mfalme wa Misri hatawaruhusu kwenda, mpaka mkono wenye nguvu umlazimishe.
20 So I will use my power [MTY] to strike/punish [the people of] Egypt [MTY] by performing many miracles there. Then he will allow you to leave.
Kwa hiyo nitaunyoosha mkono wangu na kuwapiga Wamisri kwa maajabu yote nitakayofanya miongoni mwao. Baada ya hayo, atawaruhusu mwondoke.
21 [When that happens], I will cause the people of Egypt to respect you. [The result will be that] when you leave Egypt, (you will not go empty-handed/they will give you many [valuable] things to take with you).
“Nami nitawapa hawa watu upendeleo mbele ya Wamisri, kwa hiyo mtakapoondoka nchini hamtaondoka mikono mitupu.
22 [At that time], each [Israeli] woman will ask her [Egyptian] neighbors and each [Egyptian] woman who is living in her (OR, her neighbor’s) house to [give her] some silver and gold jewelry and some [nice] clothes. [Each Egyptian woman will give them some], and you will put them on your sons and daughters [to take with you]. In that way you will (take away/confiscate) the wealth of the Egyptian people.”
Kila mwanamke Mwisraeli atamwomba jirani yake Mmisri na mwanamke yeyote anayeishi nyumbani kwake ampe vyombo vya fedha, dhahabu na nguo, ambavyo mtawavika wana wenu na binti zenu. Hivyo mtawateka nyara Wamisri.”

< Exodus 3 >