< Job 26 >

1 and to answer Job and to say
Kisha Ayubu akajibu:
2 what? to help to/for not strength to save arm not strength
“Tazama jinsi ulivyomsaidia mtu asiye na uwezo! Jinsi ulivyouokoa mkono ulio dhaifu!
3 what? to advise to/for not wisdom and wisdom to/for abundance to know
Ni shauri gani ulilompa yeye asiye na hekima? Nayo ni busara gani kubwa uliyoonyesha!
4 [obj] who? to tell speech and breath who? to come out: come from you
Ni nani aliyekusaidia kutamka maneno hayo? Nayo ni roho ya nani iliyosema kutoka kinywani mwako?
5 [the] shade to twist: tremble from underneath: under water and to dwell them
“Wafu wako katika maumivu makuu, wale walio chini ya maji na wale waishio ndani yake.
6 naked hell: Sheol before him and nothing covering to/for Abaddon (Sheol h7585)
Mauti iko wazi mbele za Mungu; Uharibifu haukufunikwa. (Sheol h7585)
7 to stretch north upon formlessness to hang land: country/planet upon without what?
Hutandaza anga la kaskazini mahali patupu; naye huiningʼiniza dunia mahali pasipo na kitu.
8 to constrain water in/on/with cloud his and not to break up/open cloud underneath: under them
Huyafungia maji kwenye mawingu yake, hata hivyo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.
9 to grasp face: surface throne to spread upon him cloud his
Huufunika uso wa mwezi mpevu, akitandaza mawingu juu yake.
10 statute: allotment to mark upon face: surface water till limit light with darkness
Amechora mstari wa upeo juu ya uso wa maji, ameweka mpaka wa nuru na giza.
11 pillar heaven to tremble and to astounded from rebuke his
Nguzo za mbingu nazo zatetemeka, zinatishika anapozikemea.
12 in/on/with strength his to disturb [the] sea (and in/on/with understanding his *Q(k)*) to wound Rahab monster
Kwa nguvu zake aliisukasuka bahari; kwa hekima yake alimkata Rahabu vipande vipande.
13 in/on/with spirit: breath his heaven clearness to bore hand his serpent fleeing
Aliisafisha anga kwa pumzi yake; kwa mkono wake alimchoma joka aendaye mbio.
14 look! these end (way: conduct his *Q(K)*) and what? whisper word to hear: hear in/on/with him and thunder (might his *Q(K)*) who? to understand
Haya ni mambo madogo tu katika matendo yake; tazama jinsi ulivyo mdogo mnongʼono tunaousikia kumhusu! Ni nani basi awezaye kuelewa ngurumo za nguvu zake?”

< Job 26 >