< Psalms 1 >
1 blessed [the] man which not to go: walk in/on/with counsel wicked and in/on/with way: conduct sinner not to stand: stand and in/on/with seat to mock not to dwell
Heri mtu yule ambaye haendi katika shauri la watu waovu, wala hasimami katika njia ya wenye dhambi, au kuketi katika baraza la wenye mizaha.
2 that if: except if: except in/on/with instruction LORD pleasure his and in/on/with instruction his to mutter by day and night
Bali huifurahia sheria ya Bwana, naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.
3 and to be like/as tree to transplant upon stream water which fruit his to give: give in/on/with time his and leaf his not to wither and all which to make: do to prosper
Mtu huyo ni kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji, ambao huzaa matunda kwa majira yake na majani yake hayanyauki. Lolote afanyalo hufanikiwa.
4 not so [the] wicked that if: except if: except like/as chaff which to drive him spirit: breath
Sivyo walivyo waovu! Wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
5 upon so not to arise: establish wicked in/on/with justice: judgement and sinner in/on/with congregation righteous
Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
6 for to know LORD way: journey righteous and way: journey wicked to perish
Kwa maana Bwana huziangalia njia za mwenye haki, bali njia ya waovu itaangamia.